< Job 39 >

1 Knowest thou the season when the Wild Goats of the crags beget? The bringing forth of the hinds, canst thou observe?
Je unajua ni wakati gani mbuzi mwitu huzaa watoto wao katika miamba? Je waweza kuwangalia paa wakati wanapozaa watoto wao?
2 Canst thou count the months they fulfil? Or knowest thou the time when they give birth?
Waweza kuhesabu miezi ya kuchukua mimba? Je unaujua muda ambao huzaa watoto wao?
3 They kneel down, their young, they bring forth; their pains, they throw off;
Wanainama chini na kuzaa watoto wao, na kisha maumivu yao ya uzazi yanaishi.
4 Their young become strong, they grow up in the open field, they go out, and return not unto them.
Watoto wao huwa na nguvu na kukua katika uwanda wa wazi; hutoka nje na hawarudi tena.
5 Who hath sent forth the Wild Ass free? And, the bands of the swift-runner, who hath loosed?
Ni nani huwaacha punda mwitu waende huru? Je nani amevilegeza vifungo vya punda wepesi,
6 Whose house I have made the waste plain, and his dwellings, the land of salt:
ni nyumba ya nani nimeifanya katika Araba, au nyumba yake katika nchi ya chumvi?
7 He laugheth at the throng of the city, The shoutings of the driver, he heareth not;
Hucheka kwa dharau katika kelele katika mji; hasikilizi kelele za mwongozaji.
8 He espieth the mountains, his pasture-ground, and, after every green thing, maketh search.
Hutembeatembea juu ya milima kama malisho yake; huko hutafuta kila mmea ulio wa kijani kwa ajili ya kula.
9 Will the Wild-Ox be pleased to be thy servant? or lodge for the night by thy crib?
Je nyati atakuwa na furaha kukutumikia? Je atakubali kukaa katika zizi lako?
10 Canst thou bind the wild-ox, so that—with the ridge—shall run his cord? Or will he harrow the furrows after thee?
Waweza kumwongoza nyati kulima mtaro kwa kamba? Je atachimba bonde kwa ajili yako?
11 Wilt thou trust in him, because of the greatness of his strength? Wilt thou leave unto him thy toil?
Je waweza kumtumaini kwasababu ya nguvu zake nyingi? Je waweza kumwachia kazi yako ili aifanye?
12 Wilt thou put faith in him, that he will bring back thy seed? and that, corn for thy threshing-floor, he will gather?
Je waweza kumtegemea akuletee nyumbani nafaka, au kukusanya nafaka katika uwanda wako wa kupuria?
13 The wing of the Ostrich that waveth itself joyfully, Is it the pinion of lovingkindness or the plumage?
Mabawa ya mbuni hupunga kwa majivuno, bali je mabawa na manyoya yana upendo?
14 For she leaveth—to the earth—her eggs, and, on the dust, she letteth them be warmed;
Kwa maana huuacha mayai yake katika nchi, na huyaacha yapate joto katika mavumbi;
15 And hath forgotten, that, a foot, may crush them, —or, the wild beast, tread on them!
husahau kuwa mguu waweza kuyaharibu au kwamba mnyama mwitu aweza kuyakanyaga.
16 Dealing hardly with her young, as none-of-hers, In vain, her labour, without dread.
Huyatendea vibaya makinda yake kana kwamba si yake; haogopi kwamba kazi yake yaweza kupotea bure,
17 For GOD hath suffered her to forget wisdom, and given her no share in understanding.
kwasababu Mungu amemnyima hekima na hajampa ufahamu wowote.
18 What time, on high, she vibrateth her wings, she laugheth at the horse and his rider.
Na wakati anapokimbia kwa haraka, huwacheka kwa dharau farasi na mpanda farasi wake.
19 Couldst thou give—to the Horse—strength? Couldst thou clothe his neck with the quivering mane?
Je umempa farasi nguvu zake? Je umeivika shingo yake kwa manyoya?
20 Couldst thou cause him to leap like a locust? The majesty of his snort, is a terror!
Je umemfanya aruke kama panzi? Enzi ya mlio wake ni wa kutisha.
21 He diggeth into the plain, and rejoiceth in vigour, he goeth forth to meet armour;
Hurarua kwa nguvu na kufurahia katika nguvu zake; hukimbia upesi kukutana na silaha.
22 He laugheth at dread, and is not dismayed, neither turneth he back, from the face of the sword;
Huidharau hofu na hashangazwi; huwa harudi nyuma kutoka katika upanga.
23 Against him, whiz [the arrows of] the quiver, the flashing head of spear and javelin;
Podo hugongagonga ubavuni mwake, pamoja na mkuki unaong'aa na fumo.
24 With stamping and rage, he drinketh up the ground, —he will not stand still when the horn soundeth;
Huimeza nchi kwa hasira na ghadhabu; katika sauti ya tarumbeta, hawezi kusimama sehemu moja.
25 As oft as the horn soundeth, he saith, Aha! And, from afar, he scenteth the battle, —the thunder of commanders and the war-cry.
Wakati wowote tarumbeta inapolia, husema, 'Ooh! Huisikia harufu ya vita kutoka mbali - vishindo vya radi za makamanda na makelele.
26 Is it, by thine understanding, that the Bird of Passage betaketh him to his pinions? spreadeth out his wings to the south?
Je ni kwa hekima yako kwamba mwewe hupaa juu, na ya kuwa huyanyosha mabawa yake kwa upande wa kusini?
27 Or, at thy bidding, that the Eagle mounteth, and that he setteth on high his nest?
Je ni kwa agizo lako kwamba tai huruka juu na kufanya kiota chake katika sehemu za juu?
28 The crag, he inhabiteth, and so lodgeth himself, on the tooth of the crag, and high fort;
Huishi katika majabali na hufanya makao yake katika vilele vya majabali, na ngomeni.
29 From thence, he searcheth out food, far away, his eyes do pierce;
Kutoka huko hutafuta mawindo; macho yake huyaona mawindo kutoka mbali.
30 And, his young brood, suck up blood, and, where the slain are, there, is he.
Makinda yake hunywa damu pia; na pale walipo watu wafu, ndipo na yeye alipo.

< Job 39 >