< Isaiah 57 >

1 The righteous one, hath perished, And not a man, hath taken it to heart—Yea the men of lovingkindness, have been withdrawn No one considering, That from the presence of calamity, hath the righteous been withdrawn.
Mwenye haki hupotea, wala hakuna hata mmoja awazaye hilo moyoni mwake; watu wanaomcha Mungu huondolewa, wala hakuna hata mmoja anayeelewa kuwa wenye haki wameondolewa ili wasipatikane na maovu.
2 He entereth into peace, Let them rest upon their couches, —Each one who went on a straight path.
Wale waendao kwa unyofu huwa na amani; hupata pumziko walalapo mautini.
3 But, ye, …draw near hither, Ye sons of divination, —Ye seed of an adulterer when your mother committed unchastity!
“Lakini ninyi: Njooni hapa, ninyi wana wa wachawi, ninyi wazao wa wazinzi na makahaba!
4 Against whom would ye disport yourselves? Against whom would ye widen the mouth and lengthen the tongue, —Are not, ye, Children of transgression, A Seed of falsehood.
Mnamdhihaki nani? Ni nani mnayemcheka kwa dharau, na kumtolea ndimi zenu? Je, ninyi si watoto wa waasi, uzao wa waongo?
5 Who inflame yourselves With the terebinths, Under every green tree—Slaying the children, In the torrent-valleys, Under the clefts of the crags:
Mnawaka tamaa katikati ya mialoni na chini ya kila mti uliotanda matawi; mnawatoa kafara watoto wenu kwenye mabonde na chini ya majabali yenye mianya.
6 Among the smooth stones of the torrent—valley, is thy portion. They, they, are thy lot; Even to them, hast thou Poured out a drink-offering. Caused to ascend a gift. Over these things, can I cease to grieve?
“Sanamu zilizo katikati ya mawe laini ya mabondeni ndizo fungu lenu; hizo ndizo sehemu yenu. Naam, kwa hizo mmemimina sadaka za vinywaji, na kutoa sadaka za nafaka. Katika haya yote, niendelee kuona huruma?
7 On a mountain high and uplifted, hast thou set thy couch, —Even thither, hast thou gone up, to offer sacrifice;
Umeweka kitanda chako juu kwenye kilima kirefu kilichoinuka, huko ulikwenda kutoa dhabihu zako.
8 And behind the door and the post, hast thou set thy symbol, For, with another than me, hast thou uncovered thyself and gone up—Hast widened thy couch, And hast solemnised for thyself a covenant from them, Thou hast loved their couch a sign, hast thou seen;
Nyuma ya milango yako na miimo yako umeweka alama zako za kipagani. Kwa kuniacha mimi, ulifunua kitanda chako, umepanda juu yake na kukipanua sana; ulifanya patano na wale ambao unapenda vitanda vyao, nawe uliangalia uchi wao.
9 And hast gone to the king with oil, And hast multiplied thy perfumes, —And hast sent thy messengers afar, And…lowered thyself as far as hades! (Sheol h7585)
Ulikwenda kwa Moleki ukiwa na mafuta ya zeituni, na ukaongeza manukato yako. Ukawatuma wajumbe wako mbali sana, ukashuka kwenye kaburi lenyewe! (Sheol h7585)
10 With the length of thy journey, thou wast wearied, Thou didst not say, Hopeless! The reviving of thy power, thou didst find, For this cause, hast thou not become sick.
Ulikuwa umechoshwa na njia zako zote, lakini hukusema, ‘Hakuna tumaini.’ Ulipata uhuisho wa nguvu zako, kwa sababu hiyo hukuzimia.
11 Whom then hadst thou been anxious about and feared that thou shouldest speak falsely, When me, thou rememberedst not, caredst not for me? Did not, I, keep silence even from age-past times, Although me, thou wouldest not fear?
“Ni nani uliyemhofu hivyo na kumwogopa hata ukawa mwongo kwangu, wala hukunikumbuka au kutafakari hili moyoni mwako? Si ni kwa sababu nimekuwa kimya muda mrefu hata huniogopi?
12 I, will expose thy righteousness, —And thy works—but they will not profit thee!
Nitaifunua haki yako na matendo yako, nayo hayatakufaidi.
13 When thou makest outcry, let thy gathered throngs deliver thee! But all of them, shall A wind, catch up—A breath, take away! Whereas he that seeketh refuge in me, Shall inherit the land, And possess my holy mountain.
Utakapolia kwa kuhitaji msaada, sanamu zako ulizojikusanyia na zikuokoe! Upepo utazipeperusha zote, pumzi peke yake itazipeperusha, Lakini mtu atakayenifanya kimbilio lake, atairithi nchi na kuumiliki mlima wangu mtakatifu.”
14 And one said—Cast ye up—cast ye up, prepare ye a way, —Lift the stumbling-block out of the way of my people.
Tena itasemwa: “Jengeni, jengeni, itengenezeni njia! Ondoeni vikwazo katika njia ya watu wangu.”
15 For, thus, saith he that is high and lifted up—Inhabiting futurity, And, holy, is his name: A high and holy place, will I inhabit, Also with the crushed and lowly in spirit, To revive the spirit of the lowly, and To revive the heart of them who are crushed; —
Kwa maana hili ndilo asemalo Aliye juu, yeye aliyeinuliwa sana, yeye aishiye milele, ambaye jina lake ni Mtakatifu: “Ninaishi mimi mahali palipoinuka na patakatifu, lakini pia pamoja na yeye aliye na roho iliyotubu na mwenye roho ya unyenyekevu, ili kuzihuisha roho za wanyenyekevu na kuihuisha mioyo yao waliotubu.
16 For not age-abidingly, will I contend, Nor perpetually, will I be wroth, —For, spirit, before me, would faint, Even the breathing souls, which, I, had made.
Sitaendelea kulaumu milele, wala sitakasirika siku zote, kwa kuwa roho ya mwanadamu ingezimia mbele zangu: yaani pumzi ya mwanadamu niliyemuumba.
17 Because of his iniquitous gain, was I wroth—and smote him Hiding myself that I might be wroth, —But he went on turning aside in the way of his own heart.
Nilighadhibika na tamaa yake ya dhambi; nilimwadhibu, nikauficha uso wangu kwa hasira, na bado aliendelea katika njia zake za tamaa.
18 His ways, have I beheld, That I might heal him, —And guide him, And restore consolations to him and to his mourners:
Nimeziona njia zake, lakini nitamponya, nitamwongoza na kumrudishia upya faraja,
19 Creating the fruit of the lips—Prosperity! Prosperity! For him that is far off and for him that is near saith Yahweh, So should I heal him.
nikiumba sifa midomoni ya waombolezaji katika Israeli. Amani, amani, kwa wale walio mbali na kwa wale walio karibu,” asema Bwana. “Nami nitawaponya.”
20 But, the lawless, are like the sea when tossed, —For, rest, it cannot! But its waters toss out mire and dirt.
Bali waovu ni kama bahari ichafukayo, ambayo haiwezi kutulia, mawimbi yake hutupa takataka na matope.
21 No well-being, saith my God, to the lawless!
Mungu wangu asema, “Hakuna amani kwa waovu.”

< Isaiah 57 >