< 1 Chronicles 15 >

1 And he made him houses, in the city of David, —and prepared a place for the ark of God, and pitched for it a tent.
Baada ya Daudi kujijengea nyumba zake katika Mji wa Daudi, akatengeneza sehemu kwa ajili ya Sanduku la Mungu, kisha akasimamisha hema kwa ajili yake.
2 Then, said David, None must carry the ark of God, save the Levites, —for, of them, did Yahweh make choice, to bear the ark of Yahweh, and to attend it, unto times age-abiding.
Kisha Daudi akasema, “Hakuna mtu yeyote anayeruhusiwa kulibeba Sanduku la Mungu isipokuwa Walawi peke yao, kwa sababu Bwana aliwachagua kulibeba Sanduku la Bwana na kuhudumu mbele zake milele.”
3 So David convoked all Israel, unto Jerusalem, —to bring up the ark of Yahweh, unto the place thereof, which he had prepared for it.
Daudi akawakusanya Israeli wote huko Yerusalemu ili kulipandisha Sanduku la Bwana na kulileta hadi kwenye sehemu aliyokuwa ametengeneza kwa ajili yake.
4 And David gathered together the sons of Aaron, and the Levites:
Kisha Daudi akawakusanya pamoja wazao wa Aroni na Walawi:
5 Of the sons of Kohath, Uriel the chief, and his brethren, one hundred and twenty;
Kutoka wazao wa Kohathi, Urieli kiongozi na ndugu zake 120,
6 of the sons of Merari, Asaiah the chief, and his brethren, two hundred and twenty;
Kutoka wazao wa Merari, Asaya kiongozi na ndugu zake 220.
7 of the sons of Gershom, Joel the chief, and his brethren, one hundred and thirty;
Kutoka wazao wa Gershoni, Yoeli kiongozi na ndugu zake 130.
8 of the sons of Elizaphan, Shemaiah the chief, and his brethren, two hundred;
Kutoka wazao wa Elisafani, Shemaya kiongozi na ndugu zake 200.
9 of the sons of Hebron, Eliel the chief, and his brethren, eighty;
Kutoka wazao wa Hebroni, Elieli kiongozi na ndugu zake 80.
10 of the son of Uzziel, Amminadab the chief, and his brethren, a hundred and twelve.
Kutoka wazao wa Uzieli, Aminadabu kiongozi na ndugu zake 112.
11 Then called David, for Zadok and for Abiathar, the priests, —and for the Levites, for Uriel, Asaiah and Joel, Shemaiah and Eliel, and Amminadab;
Kisha Daudi akawaita makuhani Sadoki na Abiathari, pamoja na Walawi Urieli, Asaya, Yoeli, Shemaya, Elieli na Aminadabu.
12 and said unto them, Ye, are the chiefs of the fathers of the Levites, —Hallow yourselves, ye and your brethren, so shall ye bring up the ark of Yahweh—God of Israel, into [the place] I have prepared for it.
Akawaambia, “Ninyi ndio viongozi wa jamaa za Walawi. Ninyi pamoja na Walawi wenzenu inawapasa mjitakase na kulipandisha Sanduku la Bwana, Mungu wa Israeli hadi mahali ambapo nimetengeneza kwa ajili yake.
13 Because, at the first, ye, did not [bring it], Yahweh our God brake forth against us, because we sought him not in the appointed way.
Ilikuwa ni kwa sababu hii, ninyi Walawi, hamkulipandisha Sanduku la Bwana mara ya kwanza, hata ikasababisha Bwana Mungu wetu kuwaka hasira dhidi yetu. Hatukumuuliza jinsi ya kufanya ili tupate kulileta jinsi alivyoagiza.”
14 So the priests and the Levites hallowed themselves, —to bring up the ark of Yahweh, God of Israel.
Kwa hiyo makuhani pamoja na Walawi wakajitakasa ili kulipandisha Sanduku la Bwana, Mungu wa Israeli.
15 And the sons of the Levites bare the ark of God, just as Moses commanded, according to the word of Yahweh, —on their shoulder, with the staves upon them.
Nao Walawi wakalichukua Sanduku la Mungu mabegani mwao wakitumia mipiko, kama vile Mose alivyoamuru sawasawa na neno la Bwana.
16 And David spake to the chiefs of the Levites, to station their brethren the singers, with instruments of song, harps and lyres, and cymbals, —sounding aloud at the lifting up of the voice, for joy.
Daudi akawaambia viongozi wa Walawi kuwaweka ndugu zao waimbaji ili waimbe nyimbo za shangwe, wakiwa na vyombo vya uimbaji: zeze, vinubi na matoazi.
17 So the Levites caused to stand, Heman son of Joel, and, of his brethren, Asaph, son of Berechiah, —and, of the sons of Merari their brethren, Ethan, son of Kushaiah;
Basi Walawi wakawaweka Hemani mwana wa Yoeli; kutoka miongoni mwa ndugu zake, Asafu mwana wa Berekia; kutoka miongoni mwa ndugu zao Wamerari, Ethani mwana wa Kushaiya;
18 and, with them, their brethren of the second degree, —Zechariah, Ben, and Jaaziel, and Shemiramoth, and Jehiel and Unni, Eliab, and Benaiah, and Maaseiah, and Mattithiah, and Eliphelehu, and Mickneiah, and Obed-edom and Jeiel, the door-keepers.
hawa ndio waliochaguliwa kuwa wasaidizi wao: Zekaria, Yaazieli, Shemiramothi, Yehieli, Uni, Eliabu, Benaya, Maaseya, Matithia, Elifelehu, Mikneya, pamoja na mabawabu Obed-Edomu na Yehieli.
19 And, the singers, Heman, Asaph and Ethan, with cymbals of bronze, were to sound aloud;
Waimbaji Hemani, Asafu na Ethani walichaguliwa kupiga matoazi ya shaba;
20 and Zechariah, and Aziel, and Shemiramoth, and Jehiel, and Unni, and Eliab, and Maaseiah and Benaiah, —with harps, over the trebles;
Zekaria, Azieli, Shemiramothi, Yehieli, Uni, Eliabu, Maaseya na Benaya walikuwa wapiga zeze kufuatana na sauti ya alamothi,
21 and Mattithiah, Eliphelehu, and Mikneiah, and Obed-edom, and Jeiel and Azaziah, —with lyres over the bass, to take the lead.
na Matithia, Elifelehu, Mikneya, Obed-Edomu, Yehieli na Azazia walikuwa wapiga vinubi, wakiongozwa kwa kufuata sauti ya sheminithi.
22 And, Chenaniah the leader of the Levites, in the service, used to give instructions in the service, because skilful was he.
Kenania kiongozi wa Walawi alikuwa msimamizi wa uimbaji; huu ndio uliokuwa wajibu wake kwa sababu alikuwa stadi katika hilo.
23 And, Berechiah and Elkanah, were door-keepers to the ark.
Berekia na Elikana walikuwa mabawabu kwa ajili ya Sanduku.
24 And, Shebaniah, and Joshaphat, and Nethanel, and Amasai, and Zechariah, and Benaiah, and Eliezer, the priests, were blowing with the trumpets, before the ark of God, —and, Obed-edom and Jehiah, were door-keepers, to the ark.
Shebania, Yoshafati, Nethaneli, Amasai, Zekaria, Benaya na Eliezeri, makuhani, walikuwa wapiga tarumbeta mbele ya Sanduku la Mungu. Obed-Edomu na Yehiya waliwekwa pia kuwa mabawabu wa Sanduku.
25 Thus, it was, David and the elders of Israel, and the rulers of thousands, who were going, to bring up the ark of the covenant of Yahweh, out of the house of Obed-edom, with joy.
Basi Daudi pamoja na wazee wa Israeli na majemadari wa vikosi vya elfu wakaenda ili kulipandisha Sanduku la Agano la Bwana kutoka nyumba ya Obed-Edomu kwa shangwe.
26 And so it was that, when God helped the Levites, who were bearing the ark of the covenant of Yahweh, they sacrificed seven bullocks and seven rams.
Kwa sababu Mungu alikuwa amewasaidia Walawi waliokuwa wanalichukua Sanduku la Agano la Bwana, mafahali saba na kondoo dume saba walitolewa dhabihu.
27 Now, David, was wrapped about with a robe of byssus, with all the Levites who were bearing the ark, and the singers, and Chenaniah the leader of the service rendered by the singers, —but, upon David, was an ephod of white linen.
Basi Daudi alikuwa amevaa joho la kitani safi, kama walivyokuwa wamevaa Walawi wote waliokuwa wanalichukua lile Sanduku, waimbaji nao walivaa vivyo hivyo, pamoja na Kenania aliyekuwa anaongoza nyimbo za waimbaji. Daudi alivaa pia kisibau cha kitani safi.
28 So, all Israel, were bringing up the ark of the covenant of Yahweh, with shouting, and with sound of the horn, and with trumpets, and with cymbals, —sounding aloud, with harps, and lyres.
Hivyo Israeli wote wakalipandisha Sanduku la Agano la Bwana kwa shangwe, wakipiga pembe za kondoo dume, tarumbeta, matoazi, wakipiga zeze na vinubi.
29 And so it was that, when the ark of the covenant of Yahweh came in as far as the city of David, —and Michal daughter of Saul looked forth through the window, and saw King David, dancing and playing, that she despised him in her heart.
Sanduku la Agano la Bwana lilipokuwa linaingia katika Mji wa Daudi, Mikali binti Sauli akachungulia dirishani. Naye alipomwona Mfalme Daudi akicheza na kusherehekea, akamdharau moyoni mwake.

< 1 Chronicles 15 >