< 2 Kings 1 >

1 Then Moab revolted against Israel, after the death of Ahab.
Baada ya kifo cha Mfalme Ahabu, nchi ya Moabu iliasi dhidi ya Israeli.
2 And Ahaziah fell through the lattice in his upper chamber, which was in Samaria, and became sick, —so he sent messengers, and said unto them—Go enquire of Baalzebub, god of Ekron, whether I shall recover from this sickness.
Basi Ahazia alikuwa ameanguka huko Samaria kutoka baraza ya chumba chake cha juu, akaumia. Hivyo akatuma wajumbe, akiwaambia, “Nendeni mkaulize kwa Baal-Zebubu, mungu wa Ekroni, mkaone kama nitapona kutokana na kuumia huku.”
3 But, the messenger of Yahweh, spake unto Elijah the Tishbite, Rise, go up to meet the messengers of the king of Samaria, —and say unto them—Is it, because there is no God in Israel, that, ye, are going to enquire of Baalzebub, god of Ekron?
Lakini malaika wa Bwana akamwambia Eliya, Mtishbi, “Panda ukakutane na wajumbe wa mfalme wa Samaria, uwaulize, ‘Je, ni kwa sababu hakuna Mungu katika Israeli ndiyo maana mnakwenda kumuuliza Baal-Zebubu, mungu wa Ekroni?’
4 Wherefore, Thus, saith Yahweh, From the bed whereunto thou hast gone up, shalt thou not come down, for thou shalt, surely die. And Elijah departed.
Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana, ‘Hutaondoka kwenye kitanda unachokilalia. Hakika utakufa!’” Hivyo Eliya akaenda.
5 And, when the messengers returned unto him, he said unto them—How is it that ye have returned?
Wajumbe waliporudi kwa mfalme, akawauliza, “Kwa nini mmerudi?”
6 And they said unto him—A man, came up to meet us, and said unto us—Go, return unto the king who sent you, and ye shall say unto him, Thus, saith Yahweh—Is it, because there is no God in Israel, that, thou, art sending to enquire of Baalzebub, god of Ekron? Therefore, from the bed whereunto thou hast gone up, shalt thou not come down, for thou shalt, surely die.
Wakamjibu, “Mtu fulani alikuja kukutana nasi, naye akatuambia, ‘Rudini kwa mfalme aliyewatuma na mkamwambie, “Hili ndilo asemalo Bwana: Je, ni kwa sababu hakuna Mungu katika Israeli ndiyo maana unawatuma watu kwenda kuuliza kwa Baal-Zebubu, mungu wa Ekroni? Kwa hiyo hutaondoka kwenye kitanda unachokilalia. Hakika utakufa!”’”
7 And he said unto them, What was the manner of the man who came up to meet you, —and spake unto you these words?
Mfalme akawauliza, “Alikuwa mtu wa namna gani ambaye mlikutana naye, akawaambia hili?”
8 And they said unto him—A hairy man, with a leathern girdle girt about his loins. And he said—Elijah the Tishbite, it was.
Wakamjibu, “Alikuwa mtu aliyekuwa na vazi la manyoya na mkanda wa ngozi kiunoni mwake.” Mfalme akasema, “Huyo alikuwa ni Eliya, Mtishbi.”
9 Then sent he unto him a captain of fifty, with his fifty, and he went up unto him, and lo! he abode on the top of the mountain, and he said unto him, O man of God! the king, hath said, Come down!
Ndipo mfalme akamtuma mkuu mmoja wa kikosi pamoja na kikosi chake cha askari hamsini kwa nabii Eliya. Yule mkuu wa kikosi akamwendea Eliya, aliyekuwa ameketi juu ya kilima, na kumwambia, “Mtu wa Mungu, mfalme anasema, ‘Shuka chini!’”
10 And Elijah responded and said unto the captain of fifty, If, then, a man of God, I am, let fire come down out of the heavens, and devour thee and thy fifty. So there came down fire out of the heavens, and devoured him and his fifty.
Eliya akamjibu yule mkuu wa kikosi, “Ikiwa mimi ni mtu wa Mungu, moto na ushuke kutoka mbinguni ukuteketeze wewe na watu wako hamsini!” Ndipo moto ukashuka kutoka mbinguni na kuwateketeza yule mkuu wa kikosi pamoja na watu wake.
11 Then he again sent unto him another captain of fifty, with his fifty. And he also spake and said unto him, O man of God! thus, saith the king, Haste thee, come down!
Aliposikia hili, mfalme akatuma kwa Eliya mkuu wa kikosi mwingine na askari wake hamsini. Yule mkuu wa kikosi akamwambia Eliya, “Mtu wa Mungu, hili ndilo asemalo mfalme, ‘Shuka chini mara moja!’”
12 And Elijah responded and said unto them—If, a man of God, I am, let fire come down out of the heavens, and devour thee and thy fifty. And there came down a fire of God, out of the heavens, and devoured him and his fifty.
Eliya akajibu, “Ikiwa mimi ni mtu wa Mungu, moto na ushuke kutoka mbinguni ukuteketeze wewe na watu wako hamsini!” Ndipo moto wa Mungu ukashuka kutoka mbinguni, ukamteketeza yeye na watu wake hamsini.
13 Then he again sent a third captain of fifty, with his fifty, —and the third captain of fifty ascended and came near, and bowed down upon his knees before Elijah, and made supplication unto him, and said unto him, O man of God! let my life, I pray thee, and the lives of these thy fifty servants, be precious in thine eyes.
Hivyo mfalme akatuma mkuu wa kikosi wa tatu na watu wake hamsini. Huyu mkuu wa kikosi wa tatu akapanda na kupiga magoti mbele ya Eliya, akiomba, “Mtu wa Mungu, tafadhali niachie uhai wangu na uhai wa hawa watu hamsini, watumishi wako!
14 Lo! there hath come down fire out of the heavens, and devoured the captains of the former fifties, with their fifties, —now, therefore, let my life be precious in thine eyes.
Tazama, moto umeshuka kutoka mbinguni na kuwateketeza wale wakuu wa vikosi viwili vya kwanza pamoja na watu wao. Lakini sasa niachie uhai wangu!”
15 And the messenger of Yahweh said unto Elijah, Go down with him, do not fear because of him, So he arose, and went down with him, unto the king;
Malaika wa Bwana akamwambia Eliya, “Shuka pamoja naye, usimwogope.” Hivyo Eliya akainuka na kushuka pamoja naye kwa mfalme.
16 and said unto him—Thus, saith Yahweh—For that thou didst send messengers to enquire of Baalzebub, god of Ekron, was it because there was no God in Israel, for whose word thou couldst enquire? Therefore, from the bed whereunto thou hast gone up, shalt thou not come down, for thou shalt, surely die.
Akamwambia mfalme, “Hili ndilo asemalo Bwana: Je, ni kwa sababu hakuna Mungu katika Israeli wa kumuuliza habari, ndiyo maana ukatuma wajumbe kuuliza Baal-Zebubu, mungu wa Ekroni? Kwa sababu umefanya hili, kamwe hutaondoka kwenye kitanda unachokilalia. Hakika utakufa!”
17 And he died, according to the word of Yahweh which, Elijah, had spoken, and Jehoram reigned in his stead, in the second year of Jehoram son of Jehoshaphat king of Judah, —because he had no son.
Hivyo akafa, sawasawa na lile neno la Bwana ambalo Eliya alikuwa amesema. Kwa kuwa Ahazia hakuwa na mwana, Yoramu akawa mfalme baada yake katika mwaka wa pili wa Yehoramu mwana wa Yehoshafati mfalme wa Yuda.
18 Now, the rest of the story of Ahaziah, the things that he did, are, they, not written in the book of the Chronicles of the Kings of Israel?
Kwa matukio mengine ya utawala wa Ahazia na yale aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?

< 2 Kings 1 >