< Psalms 76 >

1 For the Chief Musician; on stringed instruments. A Psalm of Asaph, a Song. In Judah is God known: his name is great in Israel.
Kwa mwimbishaji. Kwa ala za nyuzi za muziki. Zaburi ya Asafu. Wimbo. Katika Yuda, Mungu anajulikana, jina lake ni kuu katika Israeli.
2 In Salem also is his tabernacle, and his dwelling place in Zion.
Hema lake liko Salemu, makao yake katika Sayuni.
3 There he brake the arrows of the bow; the shield, and the sword, and the battle. (Selah)
Huko alivunja mishale imetametayo, ngao na panga, silaha za vita.
4 Glorious art thou [and] excellent, from the mountains of prey.
Wewe unangʼaa kwa mwanga, mwenye fahari zaidi ya milima yenye utajiri wa wanyama pori.
5 The stouthearted are spoiled, they have slept their sleep; and none of the men of might have found their hands.
Mashujaa hulala wametekwa nyara, hulala usingizi wao wa mwisho; hakuna hata mmoja wa watu wa vita anayeweza kuinua mikono yake.
6 At thy rebuke, O God of Jacob, both chariot and horse are cast into a dead sleep.
Kwa kukemea kwako, Ee Mungu wa Yakobo, farasi na gari la vita vilikaa kimya.
7 Thou, even thou, art to be feared: and who may stand in thy sight when once thou art angry?
Wewe peke yako ndiye wa kuogopwa. Ni nani awezaye kusimama mbele yako unapokasirika?
8 Thou didst cause sentence to be heard from heaven; the earth feared, and was still,
Kutoka mbinguni ulitamka hukumu, nayo nchi ikaogopa, ikawa kimya:
9 When God arose to judgment, to save all the meek of the earth. (Selah)
wakati wewe, Ee Mungu, ulipoinuka kuhukumu, kuwaokoa wote walioonewa katika nchi.
10 Surely the wrath of man shall praise thee: the residue of wrath shalt thou gird upon thee.
Hakika ghadhabu yako dhidi ya wanadamu inakuletea sifa, na masalia ya ghadhabu yako unajifunga mshipi.
11 Vow, and pay unto the LORD your God: let all that be round about him bring presents unto him that ought to be feared.
Wekeni nadhiri kwa Bwana Mungu wenu na kuzitimiza; nchi zote za jirani na walete zawadi kwa Yule astahiliye kuogopwa.
12 He shall cut off the spirit of princes: he is terrible to the kings of the earth.
Huvunja roho za watawala; anaogopwa na wafalme wa dunia.

< Psalms 76 >