< Psalms 75 >

1 For the Chief Musician; [set to] Al-tashheth. A Psalm of Asaph, a Song. We give thanks unto thee, O God; we give thanks, for thy name is near: men tell of thy wondrous works.
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Usiharibu!” Zaburi ya Asafu. Wimbo. Ee Mungu, tunakushukuru, tunakushukuru wewe, kwa kuwa jina lako li karibu; watu husimulia matendo yako ya ajabu.
2 When I shall find the set time, I will judge uprightly.
Unasema, “Ninachagua wakati maalum; ni mimi nihukumuye kwa haki.
3 The earth and all the inhabitants thereof are dissolved: I have set up the pillars of it. (Selah)
Wakati dunia na watu wake wote inapotetemeka, ni mimi ninayezishikilia nguzo zake imara.
4 I said unto the arrogant, Deal not arrogantly: and to the wicked, Lift not up the horn:
Kwa wale wenye majivuno ninasema, ‘Msijisifu tena,’ kwa wale waovu, ‘Msiinue pembe zenu.
5 Lift not up your horn on high; speak not with a stiff neck.
Msiinue pembe zenu dhidi ya mbingu; msiseme kwa shingo zilizonyooshwa.’”
6 For neither from the east, nor from the west, nor yet from the south, [cometh] lifting up.
Hakuna yeyote atokaye mashariki wala magharibi au kutoka jangwani awezaye kumkweza mwanadamu.
7 But God is the judge: he putteth down one, and lifteth up another.
Bali Mungu ndiye ahukumuye: Humshusha huyu na kumkweza mwingine.
8 For in the hand of the LORD there is a cup, and the wine foameth; it is full of mixture, and he poureth out of the same: surely the dregs thereof, all the wicked of the earth shall wring them out, and drink them.
Mkononi mwa Bwana kuna kikombe kilichojaa mvinyo unaotoka povu uliochanganywa na vikolezo; huumimina, nao waovu wote wa dunia hunywa mpaka tone la mwisho.
9 But I will declare for ever, I will sing praises to the God of Jacob.
Bali mimi, nitatangaza hili milele; nitaimba sifa kwa Mungu wa Yakobo.
10 All the horns of the wicked also will I cut off; but the horns of the righteous shall be lifted up.
Nitazikatilia mbali pembe za waovu wote, bali pembe za wenye haki zitainuliwa juu.

< Psalms 75 >