< Psalms 4 >

1 For the Chief Musician; on stringed instruments. A Psalm of David. Answer me when I call, O God of my righteousness; thou hast set me at large [when I was] in distress: have mercy upon me, and hear my prayer.
Kwa mwimbishaji. Kwa ala za nyuzi za muziki. Zaburi ya Daudi. Nijibu nikuitapo, Ee Mungu wangu mwenye haki! Nipumzishe katika shida zangu; nirehemu, usikie ombi langu.
2 O ye sons of men, how long shall my glory be turned into dishonour? [how long] will ye love vanity, and seek after falsehood? (Selah)
Enyi watu, mtabadilisha utukufu wangu kuwa aibu mpaka lini? Mtapenda udanganyifu na kufuata miungu ya uongo mpaka lini?
3 But know that the LORD hath set apart him that is godly for himself: the LORD will hear when I call unto him.
Fahamuni hakika kwamba Bwana amewatenga wale wamchao kwa ajili yake; Bwana atanisikia nimwitapo.
4 Stand in awe, and sin not: commune with your own heart upon your bed, and be still. (Selah)
Katika hasira yako, usitende dhambi. Mkiwa vitandani mwenu, mtulie kimya mkiichunguza mioyo yenu.
5 Offer the sacrifices of righteousness, and put your trust in the LORD.
Toeni dhabihu zilizo haki; mtegemeeni Bwana.
6 Many there be that say, Who will shew us [any] good? LORD, lift thou up the light of thy countenance upon us.
Wengi wanauliza, “Ni nani awezaye kutuonyesha jema lolote?” Ee Bwana, tuangazie nuru ya uso wako.
7 Thou hast put gladness in my heart, more than [they have] when their corn and their wine are increased.
Wewe umejaza moyo wangu kwa furaha kubwa kuliko watu waliopata nafaka na divai kwa wingi.
8 In peace will I both lay me down and sleep: for thou, LORD, alone makest me dwell in safety.
Nitajilaza chini na kulala kwa amani, kwa kuwa wewe peke yako, Ee Bwana, waniwezesha kukaa kwa salama.

< Psalms 4 >