< Job 32 >

1 So these three men ceased to answer Job, because he was righteous in his own eyes.
Basi watu hawa watatu wakaacha kumjibu Ayubu, kwa kuwa alikuwa mwadilifu machoni pake mwenyewe.
2 Then was kindled the wrath of Elihu the son of Barachel the Buzite, of the family of Ram: against Job was his wrath kindled, because he justified himself rather than God.
Lakini Elihu mwana wa Barakeli, wa kabila la Buzi wa jamaa ya Ramu, akamkasirikia sana Ayubu, kwa sababu ya kujihesabia haki mwenyewe badala ya Mungu.
3 Also against his three friends was his wrath kindled, because they had found no answer, and yet had condemned Job.
Pia aliwakasirikia hao rafiki watatu wa Ayubu, kwa sababu hawakuweza kupata njia ya kuthibitisha ya kuwa hayo maneno ya Ayubu hayakuwa ya kweli, nao bado walikuwa wamemlaumu.
4 Now Elihu had waited to speak unto Job, because they were elder than he.
Basi Elihu alikuwa amesubiri kwanza waongee na Ayubu kwa sababu walikuwa na umri mkubwa kumliko yeye.
5 And when Elihu saw that there was no answer in the mouth of these three men, his wrath was kindled.
Lakini alipoona watu hao watatu hawakuwa na kitu zaidi cha kusema, hasira yake ikaamka.
6 And Elihu the son of Barachel the Buzite answered and said, I am young, and ye are very old; wherefore I held back, and durst not shew you mine opinion.
Basi Elihu mwana wa Barakeli wa kabila la Buzi akasema: “Mimi ni mdogo kwa umri, nanyi ni wazee; ndiyo sababu niliogopa, sikuthubutu kuwaambia kile ninachojua.
7 I said, Days should speak, and multitude of years should teach wisdom.
Nilifikiri, ‘Yafaa umri useme, nao wingi wa miaka ungefundisha hekima.’
8 But there is a spirit in man, and the breath of the Almighty giveth them understanding.
Lakini ni Roho iliyoko ndani ya mwanadamu, pumzi ya Mwenyezi, ndiyo impayo yeye ufahamu.
9 It is not the great that are wise, nor the aged that understand judgment.
Sio wazee peke yao walio na hekima, sio wenye umri mkubwa peke yao wanaofahamu lililo sawa.
10 Therefore I said, Hearken to me; I also will shew mine opinion.
“Kwa hiyo nasema: Nisikilizeni mimi; mimi nami nitawaambia lile ninalojua.
11 Behold, I waited for your words, I listened for your reasons, whilst ye searched out what to say.
Nilingojea mlipokuwa mnaongea, nilizisikiliza hoja zenu; mlipokuwa mkitafuta maneno ya kusema,
12 Yea, I attended unto you, and, behold, there was none that convinced Job, or that answered his words, among you.
niliwasikiliza kwa makini. Lakini hakuna hata mmoja wenu aliyethibitisha kwamba Ayubu amekosa; hakuna hata mmoja wenu aliyeweza kujibu hoja zake.
13 Beware lest ye say, We have found wisdom; God may vanquish him, not man:
Msiseme, ‘Tumepata hekima; Mungu na amthibitishe kuwa mwongo, wala si mwanadamu.’
14 For he hath not directed his words against me; neither will I answer him with your speeches.
Lakini Ayubu hajayapanga maneno yake dhidi yangu, nami sitamjibu kwa kutumia hoja zenu.
15 They are amazed, they answer no more: they have not a word to say.
“Wametiwa hofu na hawana la zaidi la kusema; maneno yamewaishia.
16 And shall I wait, because they speak not, because they stand still, and answer no more?
Je, ningoje sasa kwa sababu wamekuwa kimya, kwa vile sasa wanasimama bila kuwa na la kujibu?
17 I also will answer my part, I also will shew mine opinion.
Mimi nami nitakuwa na la kusema; mimi nami nitasema lile nilijualo.
18 For I am full of words; the spirit within me constraineth me.
Kwa kuwa nimejawa na maneno, nayo Roho iliyomo ndani yangu yanisukuma;
19 Behold, my belly is as wine which hath no vent; like new bottles it is ready to burst.
ndani yangu niko kama chupa iliyojazwa divai, kama kiriba kipya cha divai kilicho tayari kupasuka.
20 I will speak, that I may be refreshed; I will open my lips and answer.
Ni lazima niseme ili niweze kutulia; ni lazima nifumbue midomo yangu nipate kujibu.
21 Let me not, I pray you, respect any man’s person; neither will I give flattering titles unto any man.
Sitampendelea mtu yeyote, wala sitajipendekeza kwa mtu yeyote;
22 For I know not to give flattering titles; [else] would my Maker soon take me away.
kwa kuwa kama ningekuwa stadi wa kujipendekeza, Muumba wangu angeniondolea mbali kwa upesi.

< Job 32 >