< Job 33 >

1 Howbeit, Job, I pray thee, hear my speech, and hearken to all my words.
“Lakini Ayubu, sasa, sikiliza maneno yangu; zingatia kila kitu nitakachosema.
2 Behold now, I have opened my mouth, my tongue hath spoken in my mouth.
Karibu nitafungua kinywa changu; maneno yangu yapo katika ncha ya ulimi wangu.
3 My words [shall utter] the uprightness of my heart: and that which my lips know they shall speak sincerely.
Maneno yangu yanatoka katika moyo mnyofu; midomo yangu hunena kwa uaminifu yale niyajuayo.
4 The spirit of God hath made me, and the breath of the Almighty giveth me life.
Roho wa Mungu ameniumba; pumzi ya Mwenyezi hunipa uhai.
5 If thou canst, answer thou me; set [thy words] in order before me, stand forth.
Unijibu basi, kama unaweza; jiandae kunikabili mimi.
6 Behold, I am toward God even as thou art: I also am formed out of the clay.
Mimi ni kama wewe mbele za Mungu; mimi pia nimetolewa kwenye udongo.
7 Behold, my terror shall not make thee afraid, neither shall my pressure be heavy upon thee.
Huna sababu ya kuniogopa, wala mkono wangu haupaswi kukulemea.
8 Surely thou hast spoken in mine hearing, and I have heard the voice of [thy] words, [saying],
“Lakini umesema nikiwa ninakusikia, nami nilisikia maneno yenyewe:
9 I am clean, without transgression; I am innocent, neither is there iniquity in me:
‘Mimi ni safi na sina dhambi; mimi ni safi na sina hatia.
10 Behold, he findeth occasions against me, he counteth me for his enemy;
Lakini bado Mungu amepata dosari kwangu, naye ananiona kama adui yake.
11 He putteth my feet in the stocks, he marketh all my paths.
Ananifunga miguu kwa pingu, tena anaziangalia njia zangu zote kwa karibu.’
12 Behold, I will answer thee, in this thou art not just; for God is greater than man.
“Lakini mimi ninakuambia, katika jambo hili wewe una makosa, kwa maana Mungu ni mkuu kuliko mwanadamu.
13 Why dost thou strive against him? for he giveth not account of any of his matters.
Kwa nini unamlalamikia kwamba yeye hamjibu mwanadamu?
14 For God speaketh once, yea twice, [though man] regardeth it not.
Kwa kuwa Mungu husema, wakati huu kwa njia moja, au wakati mwingine kwa njia nyingine, ingawa mwanadamu anaweza asielewe.
15 In a dream, in a vision of the night, when deep sleep falleth upon men, in slumberings upon the bed;
Mungu husema na mwanadamu katika ndoto, katika maono ya usiku, wakati usingizi mzito uwaangukiapo wanadamu wasinziapo vitandani mwao,
16 Then he openeth the ears of men, and sealeth their instruction,
anaweza akasemea masikioni mwao, na kuwatia hofu kwa maonyo,
17 That he may withdraw man [from his] purpose, and hide pride from man;
ili kumgeuza mtu kutoka kwenye kutenda mabaya na kumwepusha na kiburi,
18 He keepeth back his soul from the pit, and his life from perishing by the sword.
kuiokoa nafsi yake na shimo, uhai wake usiangamizwe kwa upanga.
19 He is chastened also with pain upon his bed, and with continual strife in his bones:
Mtu anaweza kutiwa adabu kwa maumivu kitandani mwake, kwa dhiki za mfululizo katika mifupa yake,
20 So that his life abhorreth bread, and his soul dainty meat.
kiasi kwamba maisha yake yenyewe yanakataa chakula nayo nafsi yake ikakichukia kabisa hata chakula kizuri.
21 His flesh is consumed away, that it cannot be seen; and his bones that were not seen stick out.
Nyama ya mwili wake huisha kwa kukonda, nayo mifupa yake ambayo mwanzoni ilikuwa imefichika, sasa inatokeza nje.
22 Yea, his soul draweth near unto the pit, and his life to the destroyers.
Nafsi yake inakaribia kaburi, nao uhai wake karibu na wajumbe wa kifo.
23 If there be with him an angel, an interpreter, one among a thousand, to shew unto man what is right for him;
“Kama bado kuna malaika upande wake kama mtetezi, mmoja miongoni mwa elfu, wa kumwambia mwanadamu lililo jema kwake,
24 Then he is gracious unto him, and saith, Deliver him from going down to the pit, I have found a ransom.
kumwonea huruma na kusema, ‘Mwokoe asije akatumbukia shimoni; nimepata ukombozi kwa ajili yake’:
25 His flesh shall be fresher than a child’s; he returneth to the days of his youth:
ndipo nyama ya mwili wake hufanywa mpya kama ya mtoto; hurudishwa upya kama siku za ujana wake.
26 He prayeth unto God, and he is favourable unto him; so that he seeth his face with joy: and he restoreth unto man his righteousness.
Humwomba Mungu, akapata kibali kwake, huuona uso wa Mungu na kushangilia kwa furaha; Mungu humrudisha katika hali yake ya uadilifu.
27 He singeth before men, and saith, I have sinned, and perverted that which was right, and it profited me not:
Ndipo huja mbele za watu na kusema, ‘Nilitenda dhambi na kupotosha kilichokuwa haki, lakini sikuadhibiwa kama nilivyostahili.
28 He hath redeemed my soul from going into the pit, and my life shall behold the light.
Alinikomboa nafsi yangu nisitumbukie shimoni, nami nitaishi ili kuufurahia mwanga.’
29 Lo, all these things doth God work, twice, [yea] thrice, with a man,
“Mungu hufanya haya yote kwa mwanadamu; mara mbili hata mara tatu,
30 To bring back his soul from the pit, that he may be enlightened with the light of the living.
ili aigeuze nafsi yake toka shimoni, ili nuru ya uzima imwangazie.
31 Mark well, O Job, hearken unto me: hold thy peace, and I will speak.
“Ayubu, zingatia, nisikilize mimi; nyamaza, nami nitanena.
32 If thou hast any thing to say, answer me: speak, for I desire to justify thee.
Kama unalo lolote la kusema, unijibu; sema, kwa maana ninataka uonekane huna hatia.
33 If not, hearken thou unto me: hold thy peace, and I will teach thee wisdom.
Lakini kama huna la kusema, basi nisikilize mimi; nyamaza, nami nitakufundisha hekima.”

< Job 33 >