< Psalms 2 >

1 Why do the nations rage, and the peoples imagine a vain thing?
Kwa nini mataifa wanashauriana kufanya mabaya, na kabila za watu kula njama bure?
2 The kings of the earth set themselves, and the rulers take counsel together, against the LORD, and against his anointed, [saying],
Wafalme wa dunia wanajipanga na watawala wanajikusanya pamoja dhidi ya Bwana na dhidi ya Mpakwa Mafuta wake.
3 Let us break their bands asunder, and cast away their cords from us.
Wanasema, “Tuvunje minyororo yao na kuvitupilia mbali vifungo vyao.”
4 He that sitteth in the heavens shall laugh: the Lord shall have them in derision.
Yeye atawalaye mbinguni hucheka, Bwana huwadharau.
5 Then shall he speak unto them in his wrath, and vex them in his sore displeasure:
Kisha huwakemea katika hasira yake na kuwaogopesha katika ghadhabu yake, akisema,
6 Yet I have set my king upon my holy hill of Zion.
“Nimemtawaza Mfalme wangu juu ya Sayuni, mlima wangu mtakatifu.”
7 I will tell of the decree: the LORD said unto me, Thou art my son; this day have I begotten thee.
Nitatangaza amri ya Bwana: Yeye aliniambia, “Wewe ni Mwanangu, leo mimi nimekuzaa.
8 Ask of me, and I will give thee the nations for thine inheritance, and the uttermost parts of the earth for thy possession.
Niombe, nami nitayafanya mataifa kuwa urithi wako, miisho ya dunia kuwa milki yako.
9 Thou shalt break them with a rod of iron; thou shalt dash them in pieces like a potter’s vessel.
Utawatawala kwa fimbo ya chuma na kuwavunjavunja kama chombo cha mfinyanzi.”
10 Now therefore be wise, O ye kings: be instructed, ye judges of the earth.
Kwa hiyo, ninyi wafalme, kuweni na hekima; mwonyeke, enyi watawala wa dunia.
11 Serve the LORD with fear, and rejoice with trembling.
Mtumikieni Bwana kwa hofu na mshangilie kwa kutetemeka.
12 Kiss the son, lest he be angry, and ye perish in the way, for his wrath will soon be kindled. Blessed are all they that put their trust in him.
Mbusu Mwana, asije akakasirika nawe ukaangamizwa katika njia yako, kwa maana hasira yake inaweza kuwaka ghafula. Heri wote wanaomkimbilia.

< Psalms 2 >