< Job 38 >

1 Then the LORD answered Job out of the whirlwind, and said,
Kisha Bwana akamjibu Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli. Akasema:
2 Who is this that darkeneth counsel by words without knowledge?
“Nani huyu atiaye mashauri yangu giza kwa maneno yasiyo na maarifa?
3 Gird up now thy loins like a man; for I will demand of thee, and declare thou unto me.
Jikaze kama mwanaume; nitakuuliza swali, nawe unijibu.
4 Where wast thou when I laid the foundations of the earth? declare, if thou hast understanding.
“Ulikuwa wapi nilipoweka misingi ya dunia? Niambie, kama unafahamu.
5 Who determined the measures thereof, if thou knowest? or who stretched the line upon it?
Ni nani aliyeweka alama vipimo vyake? Hakika wewe unajua! Ni nani aliyenyoosha kamba ya kupimia juu yake?
6 Whereupon were the foundations thereof fastened? or who laid the corner stone thereof;
Je, misingi yake iliwekwa juu ya nini, au ni nani aliyeweka jiwe la pembeni,
7 When the morning stars sang together, and all the sons of God shouted for joy?
wakati nyota za asubuhi zilipoimba pamoja, na malaika wote walipokuwa wakipiga kelele kwa furaha?
8 [Or who] shut up the sea with doors, when it brake forth, [as if] it had issued out of the womb;
“Ni nani aliyeifungia bahari milango ilipopasuka kutoka tumbo,
9 When I made the cloud the garment thereof, and thick darkness a swaddlingband for it,
nilipoyafanya mawingu kuwa vazi lake, na kuyafungia katika giza nene,
10 And prescribed for it my decree, and set bars and doors,
nilipoamuru mipaka yake, na kuiweka milango yake na makomeo mahali pake,
11 And said, Hitherto shalt thou come, but no further; and here shall thy proud waves be stayed?
niliposema, ‘Unaweza kufika mpaka hapa wala si zaidi; hapa ndipo mawimbi yako yenye kiburi yatakapokomea’?
12 Hast thou commanded the morning since thy days [began, and] caused the dayspring to know its place;
“Umepata kuiamrisha asubuhi ipambazuke, au kuyaonyesha mapambazuko mahali pake,
13 That it might take hold of the ends of the earth, and the wicked be shaken out of it?
yapate kushika miisho ya dunia, na kuwakungʼuta waovu waliomo?
14 It is changed as clay under the seal; and [all things] stand forth as a garment:
Dunia hubadilika kama udongo wa mfinyanzi chini ya lakiri; sura yake hukaa kama ile ya vazi.
15 And from the wicked their light is withholden, and the high arm is broken.
Waovu huzuiliwa nuru yao, nao mkono wao ulioinuliwa huvunjwa.
16 Hast thou entered into the springs of the sea? or hast thou walked in the recesses of the deep?
“Je, umepata kufika kwenye chemchemi za bahari? Au kutembea mahali pa ndani pa vilindi?
17 Have the gates of death been revealed unto thee? or hast thou seen the gates of the shadow of death?
Umewahi kuonyeshwa malango ya mauti? Umewahi kuiona milango ya uvuli wa mauti?
18 Hast thou comprehended the breadth of the earth? declare, if thou knowest it all.
Je, wewe unafahamu ukubwa wa dunia? Niambie kama unajua haya yote.
19 Where is the way to the dwelling of light, and as for darkness, where is the place thereof;
“Njia ya kufika kwenye makao ya nuru ni ipi? Nako maskani mwa giza ni wapi?
20 That thou shouldest take it to the bound thereof, and that thou shouldest discern the paths to the house thereof?
Je, unaweza kuvirudisha kwenye makao yake? Unajua njia za kufika maskani mwake?
21 [Doubtless], thou knowest, for thou wast then born, and the number of thy days is great!
Hakika unajua, kwa kuwa ulikuwa umeshazaliwa! Kwani umeishi miaka mingi!
22 Hast thou entered the treasuries of the snow, or hast thou seen the treasuries of the hail,
“Je, umeshawahi kuingia katika ghala za theluji, au kuona ghala za mvua ya mawe,
23 Which I have reserved against the time of trouble, against the day of battle and war?
ambazo nimeziweka akiba kwa ajili ya wakati wa taabu, na kwa ajili ya wakati wa vita na mapigano?
24 By what way is the light parted, or the east wind scattered upon the earth?
Ni ipi njia iendayo mahali umeme wa radi unapotawanyiwa, au mahali upepo wa mashariki unaposambaziwa juu ya dunia?
25 Who hath cleft a channel for the waterflood, or a way for the lightning of the thunder;
Ni nani aliyepasua mifereji kwa ajili ya maji mengi ya mvua yaendayo kasi na njia ya umeme wa radi,
26 To cause it to rain on a land where no man is; on the wilderness, wherein there is no man;
ili kusababisha mvua kunyeshea mahali pasipokaliwa na mtu, jangwa lisilo na yeyote ndani yake,
27 To satisfy the waste and desolate [ground]; and to cause the tender grass to spring forth?
ili kuitosheleza nchi ya ukiwa na jangwa, na majani yaanze kumea ndani yake?
28 Hath the rain a father? or who hath begotten the drops of dew?
Je, mvua ina baba? Ni nani baba azaaye matone ya umande?
29 Out of whose womb came the ice? and the hoary frost of heaven, who hath gendered it?
Barafu inatoka tumbo la nani? Ni nani azaaye ukungu kutoka mbinguni,
30 The waters are hidden as [with] stone, and the face of the deep is frozen.
wakati maji yawapo magumu kama jiwe, wakati uso wa vilindi vya maji unapoganda?
31 Canst thou bind the cluster of the Pleiades, or loose the bands of Orion?
“Je, waweza kuufunga mnyororo wa Kilimia? Waweza kulegeza kamba za Orioni?
32 Canst thou lead forth the Mazzaroth in their season? or canst thou guide the Bear with her train?
Waweza kuyaongoza makundi ya nyota kwa majira yake, au kuongoza Dubu na watoto wake?
33 Knowest thou the ordinances of the heavens? canst thou establish the dominion thereof in the earth?
Je, unajua sheria zinazotawala mbingu? Waweza kuweka utawala wa Mungu duniani?
34 Canst thou lift up thy voice to the clouds, that abundance of waters may cover thee?
“Waweza kuiinua sauti yako mpaka mawinguni, na kujifunika mwenyewe na gharika ya maji?
35 Canst thou send forth lightnings, that they may go, and say unto thee, Here we are?
Je, wewe hutuma umeme wa radi kwenye njia zake? Je, hutoa taarifa kwako kukuambia, ‘Sisi tuko hapa’?
36 Who hath put wisdom in the inward parts? or who hath given understanding to the mind?
Ni nani aliyeujalia moyo hekima au kuzipa akili ufahamu?
37 Who can number the clouds by wisdom? or who can pour out the bottles of heaven,
Nani mwenye hekima ya kuyahesabu mawingu? Ni nani awezaye kuinamisha magudulia ya mbinguni
38 When the dust runneth into a mass, and the clods cleave fast together?
wakati mavumbi yawapo magumu, na mabonge ya udongo kushikamana pamoja?
39 Wilt thou hunt the prey for the lioness? or satisfy the appetite of the young lions,
“Je, utamwindia simba jike mawindo, na kuwashibisha simba wenye njaa
40 When they couch in their dens, [and] abide in the covert to lie in wait?
wakati wao wamejikunyata mapangoni mwao, au wakivizia kichakani?
41 Who provideth for the raven his food, when his young ones cry unto God, [and] wander for lack of meat?
Ni nani ampaye kunguru chakula wakati makinda yake yanamlilia Mungu, yakizungukazunguka kwa ajili ya kukosa chakula?

< Job 38 >