< Psalms 44 >

1 For the leader. Of the Korahites. A maskil. O God, we have heard with our ears, all our ancestors have told us of the work that you wrought in their day, your wonders in days of old,
Mungu, tumesikia kwa masikio yetu, baba zetu wametuambia kazi uliyofanya katika siku zao, siku za kale.
2 uprooting and crushing the nations, then planting and settling them. For it wasn’t their own sword that won them the land,
Uliwafukuza mataifa kwa mkono wako, lakini ukawafanya watu wetu kuishi humo; wewe uliwataabisha mataifa, lakini ukawaeneza watu wetu katika nchi.
3 it was not their own arm that brought them the victory. Yours was the hand and the arm, yours was the face that shone on them with favour.
Kwa maana hawakupata umiliki wa nchi kwa upanga wao, wala mkono wao wenyewe haukuwaokoa; bali mkono wako wakuume, mkono wako, na nuru ya uso wako, na kwa sababu uliwaridhia.
4 It was you, my king and my God, that ordained the victories of Jacob.
Mungu, wewe ni Mfalme wangu, amuru ushindi kwa ajili ya Yakobo.
5 Through you we can thrust back our foes, and by your name tread down our assailants:
Kwa uweza wako tutawaangusha chini maadui zetu; kwa jina lako tutatembea juu yao, wale wanao inuka dhidi yetu.
6 for not in my bow do I trust, nor can my sword win me the victory.
Kwa maana sitauamini upinde wangu, wala upanga wangu hautaniokoa.
7 Our victory comes from you, and confusion to those who hate us.
Bali wewe ndeye uliyetuokoa na adui zetu, na umewaaibisha wale watuchukiao.
8 In God we boast all the day long, and your name will we praise forever. (Selah)
Katika Mungu tumefanywa kujivuna siku zote, nasi tutalishukuru jina lako milele. (Selah)
9 Yet you have spurned and disgraced us, in not going forth with our armies,
Lakini sasa umetutupa na kutufedhehesha, na hauendi na majeshi yetu.
10 and in making us flee from the foe, so that those who hated us plundered us.
Umetufanya kuwakimbia maadui zetu; na wale watuchukiao huchukua vitu vyetu vya thamani kwa ajili yao wenyewe.
11 You have let us be eaten like sheep, you have scattered us over the world,
Umetufanya kama kondoo aliyeandaliwa kwa ajili ya chakula na umetutawanya kati ya mataifa.
12 sold your people for a pittance, and getting no gain from their price.
Wewe unawauza watu wako bure; kwa kufanya hivyo haukupata faida.
13 You have made us the butt of our neighbours, the derision and scorn of all round us.
Wewe umetufanya kukemewa na majirani zetu, kuchekwa, na kudhihakiwa na wale wanao tuzunguka.
14 O’er the world you have made us a byword, the nations at us shake their heads.
Umetufaya kituko kati ya mataifa, .......................................................
15 My disgrace is forever before me, my face is covered with shame,
Siku zote fedheha yangu iko mbele yangu, na aibu ya uso wangu imenifunika
16 at the words of blasphemer and scoffer, at the sight of the foe and the vengeful.
kwa sababu ya sauti yake iliyo kemea na kutukana, kwa sababu ya adui na kisasi.
17 All this has come upon us, yet we have not forgotten you nor falsely dealt with your covenant.
Yote haya yametupata sisi; bado hatukukusahau wewe wala kulikosea agano lako.
18 Our heart has not turned back, nor our steps declined from your way,
Mioyo yetu haikukengeuka; hatua zetu hazikuiacha njia yako.
19 that you thus should have crushed us down, and covered us over with gloom, in the place where the jackals roam.
Bali wewe umetuadhibu vikali katika mahali pa mbweha na kutufunika na uvuli wa mauti.
20 Had we forgotten the name of our God, or stretched out our hands to a god that was strange,
Ikiwa tumelisahau jina la Mungu wetu au kueneza mikono yetu kwa Mungu mgeni,
21 would God not have searched this out? For he knows the heart and its secrets.
Mungu asingeligundua hili? Kwa maana yeye anazijua siri za moyo.
22 But in your cause it is we are killed all the day, and counted as sheep for the slaughter.
Hakika, kwa ajili ya jina lako tutauawa siku zote; tunahesabiwa kuwa kondoo kwa ajili ya kuchinjwa.
23 Rouse yourself, why do you sleep Lord? Awake, cast us not off forever.
Bwana, amka, kwa nini unalala? Inuka, usitutupe moja kwa moja.
24 Why do you hide your face, forgetting our stress and our misery?
Kwa nini unaficha uso wako na kusahau mateso yetu na kukandamizwa kwetu?
25 For we have sunk down to the dust, our bodies cling to the ground.
Kwa maana tumeyeyushwa kwenye mavumbi; miili yetu imeshikamana na ardhi.
26 Arise, come to our help: for your love’s sake, ransom us.
Inuka utusaidie na utuokoe kwa ajili ya uaminifu wa agano lako.

< Psalms 44 >