< Psalms 42 >

1 For the leader. A maskil of the Korahites. Like the hart which longs for brooks of water, I long for you, God.
Kama ayala ayatamanivyo maji ya mto. ndivyo hivyo ninakiu yako, Mungu.
2 I thirst for God, for my living God. When shall I enter in, and see the face of God?
Ninakiu yako Mungu, Mungu uliye hai, ni lini nitaonekana mbele zako?
3 My tears have been my food by day and by night; for they say to me all the day long, ‘Where is your God?’
Machozi yangu yamekuwa ni chakula changu mchana na usiku, wakati maadui zangu siku zote wanasema, “Yuko wapi Mungu wako?”
4 My heart floods with sorrow, as I call to mind: how I used to pass on with the throng, at their head, to the house of God, with glad shouts and giving of thanks, in the throng who kept festival.
Mambo haya niayakumbuka ninapoumimina roho yangu: nilipoenda na umati wa watu na kuwaongoza kwenye nyumba ya Mungu kwa sauti ya shangwe na kusifu, ni wengi tulisherekea.
5 Why am I downcast? Why this moaning within me? Hope in God; for yet will I praise him, my help, my God.
Roho yangu, kwa nini unainama? Kwa nini unahuzuni ndani yangu? Mtumaini Mungu, Kwa kuwa kwa mara nyingine nitamsifu yeye ambaye ni wokovu wangu.
6 I am sunk in my misery; I will therefore call you to mind from the land of Jordan and Hermon, the mountain Mizar.
Mungu wangu, roho yangu imeinama ndani yangu, kwa hiyo ninakukumbuka toka nchi ya Yordani, toka kwenye vilele vitatu vya mlima Hermoni, na toka mlima wa Mizari.
7 Flood is calling to flood at the noise of your cataracts; all your waves and your breakers have passed over me.
Kina huita kina kwenye kelele za maporomoko ya maji yako; mawimbi na mafuriko yako yote yako juu yangu.
8 In the day I cry to the Lord to summon his kindness; and the song that I sing in the night is a prayer to the living God.
Wakati wa mchana Yahwe ataamuru uaminifu wa agano lake; na usiku wimbo wake utakuwa nami, ombi kwa Mungu wa uhai wangu.
9 I say to God my rock, ‘Why have you forgotten me? Why must I walk so sadly, so hard pressed by the foe?’
Nami nitasema kwa Mungu wangu, mwamba wangu, “Kwa nini umenisahau? Kwa nini ninaenenda katika maombolezo kwa sababu ya ukandamizaji wa adui yangu?”
10 It pierces me to the heart to hear the enemy’s taunts, as all the day long they say to me, ‘Where is your God?’
Kama upanga mifupani pangu, maadui zangu wananikemea, siku zote wakiniambia, “Yuko wapi Mungu wako?”
11 Why am I downcast? Why this moaning within me? Hope in God; for yet will I praise him, my help, my God.
Roho yangu, kwa nini umeinama chini? Kwa nini unahuzuni ndani yangu? Mtumaini Mungu kwa kuwa nitamsifu tena yeye aliye wokovu wangu na Mungu wangu.

< Psalms 42 >