< Psalms 38 >

1 A Psalm of David. A lament. Reprove me not, Lord, in your anger, and chasten me not in your wrath;
Yahwe, usinikemee katika hasira yako; usiniadhibu katika ghadhabu yako.
2 for your arrows have sunk into me, and your hand lies heavy upon me.
Kwa kuwa mishale yako hunichoma, na mkono wako huniangusha chini.
3 In my flesh is no soundness because of your anger, no health in my bones, because of my sin.
Mwili wangu wote unaumwa kwa sababu ya hasira yako; kwa sababu ya dhambi zangu mifupa yangu haina afya.
4 For that my guilt is gone over my head: it weighs like a burden too heavy for me.
Kwa maana maovu yangu yamenielemea; yamekuwa mzigo mzito kwangu.
5 My wounds stink and fester, for my foolishness I am tormented.
Vidonda vyangu vimeoza na vinanuka kwa sababu ya upumbavu wa dhambi zangu.
6 Bent and bowed am I utterly, all the day going in mourning.
Nimepindika na kuwa mnyonge kila siku; ninaenenda katika maombolezo siku zote.
7 My loins are filled with burning, and in my flesh is no soundness.
Kwa maana ndani yangu, ninaungua; hakuna afya katika mwili wangu.
8 I am utterly crushed and numb; I cry louder than lion roars.
Nimedhohofika na kulemewa sana; ninaugua kwa sababu ya dhiki yangu.
9 Lord, you know all that I long for, my groans are not hidden from you.
Bwana, wewe unaielewa shauku ya ndani kabisa ya moyo wangu, na kuugua kwangu hakujifichika kwako.
10 My heart is throbbing, my strength has failed me. The light of my eyes – even it is gone from me.
Moyo wangu unapwita pwita, nguvu zangu zinaniisha, macho yangu yanafifia.
11 My dear ones and friends keep aloof, and my neighbours stand afar off.
Marafiki na ndugu zangu wamenitenga kwa sababu ya hali; majirani zangu hukaa mbali nami.
12 They who aim at my life lay their snares, they who seek my hurt speak of ruin, nursing treachery all the day long.
Wale wanaoutafuta uhai wangu hutega mitego kwa ajili yangu. Wao ambao hutafuta kunidhuru huongea maneno ya uharibifu na husema maneno ya uongo siku nzima.
13 But I turn a deaf ear and hear not; like the dumb I open not my mouth.
Lakini, niko kama mtu kiziwi na sisikii lolote; niko kama mtu bubu ambaye hasemi lolote.
14 I am like one without hearing, with no arguments in my mouth.
Niko kama mtu asiye sikia na mbaye hawezi kujibu.
15 For my hope, O Lord, is in you. You will answer, O Lord my God,
Hakika ninakungoja wewe, Yahwe; wewe utanijibu, Bwana Mungu wangu.
16 when I utter the hope that those who made scorn of my tottering feet may not rejoice over me.
Ninasema hivi ili kwamba maadui zangu wasije wakafurahia juu yangu. Ikiwa mguu wangu utateleza, watanifanyia mambo mabaya.
17 For I am ready to fall, my pain forsakes me never.
Kwa kuwa niko karibu mashakani, na niko katika maumivu ya mara kwa mara.
18 I acknowledge my guilt, I am anxious because of my sin:
Ninatubu makosa yangu; ninahuzunika kwa dhambi zangu.
19 My wanton assailants are strong, those who wrongfully hate me are many,
Lakini maadui zangu ni wengi; wale wanichukiao ni wengi.
20 who render me evil for good, and oppose me, because I make good my goal.
Wao wananilipa mabaya kwa mema; wanavurumiza shutuma kwangu ingawa nimefuata lililo jema.
21 Do not forsake me, O Lord; my God, be not far from me.
Usinitelekeze, Yahwe, Mungu wangu, usikae mbali nami.
22 Hasten to help me, O Lord my saviour.
Njoo haraka unisaidie, Bwana, wokovu wangu.

< Psalms 38 >