< Psalms 5 >

1 Give ear to my words, O LORD, consider my (meditation)
Sikiliza nikuitapo, Yahweh; tazama kuugua kwangu.
2 Hearken unto the voice of my cry, my King, and my God: for unto you will I pray.
Sikiliza sauti yangu nikuitapo, Ee Mfalme wangu na Mungu wangu, kwa kuwa ni kwako Bwana naomba.
3 My voice shall you hear in the morning, O LORD; in the morning will I direct my prayer unto you, and will look up.
Yahweh; sikia kilio changu asubuhi; na asubuhi nitaleta dua yangu kwako na kungoja kwa matarajio.
4 For you are not a God that has pleasure in wickedness: neither shall evil dwell with you.
Hakika wewe ni Mungu usiye kubaliana na uovu; watu waovu hawawezi kuwa wageni wako.
5 The foolish shall not stand in your sight: you hate all workers of iniquity.
Wenye kiburi hawata simama katika uwepo wako; wewe unawachukia wote wanaofanya maovu.
6 You shall destroy them that speak leasing: the LORD will detest the bloody and deceitful man.
Nawe utawaharibu waongo; Yahweh huwadharau vurugu na watu wadanganyifu.
7 But as for me, I will come into your house in the multitude of your mercy: and in your fear will I worship toward your holy temple.
Lakini kwangu mimi, kwa sababu ya ukuu na uaminifu wa agano lako, nitakuja nyumbani mwako; na kwa heshima nitakuinamia mbele ya hekalu lako takatifu.
8 Lead me, O LORD, in your righteousness because of mine enemies; make your way straight before my face.
Oh Bwana, uniongoze katika haki yako kwa sababu ya adui zangu; usawazishe njia yako mbele yangu.
9 For there is no faithfulness in their mouth; their inward part is very wickedness; their throat is an open tomb; they flatter with their tongue.
Kwa kuwa midomoni mwao hamna ukweli; utu wao wa ndani ni mwovu; makoo yao ni kaburi lililo wazi; husifu kinafiki kwa ulimi wao.
10 Destroy you them, O God; let them fall by their own counsels; cast them out in the multitude of their transgressions; for they have rebelled against you.
Mungu, wafanye kuwa na hatia; mipango yao iwe kuanguka kwao! Kwa ajili ya makosa yao mengi uwatoe nje, kwa kuwa wamekuasi wewe.
11 But let all those that put their trust in you rejoice: let them ever shout for joy, because you defend them: let them also that love your name be joyful in you.
Bali wale wanao kukimbilia wafurahi; uwafanye wapige kelele kwa shangwe siku zote kwa sababu unawapigania; uwafanye wenye furaha ndani yako, wale walipendao jina lako.
12 For you, LORD, will bless the righteous; with favour will you compass him as with a shield.
Kwa maana utawabariki wenye haki, Yahweh; utawazunguka kwa neema kama ngao.

< Psalms 5 >