< Genesis 11 >

1 And the whole earth was of one language, and of one speech.
Sasa nchi yote ilikuwa inatumia lugha moja na ilikua na usemi mmoja.
2 And it came to pass, as they journeyed from the east, that they found a plain in the land of Shinar; and they dwelt there.
Ikawa waliposafiri upande wa mashariki, wakaona eneo tambarare katika nchi ya Shinari na wakakaa pale.
3 And they said one to another, Go to, let us make brick, and burn them thoroughly. And they had brick for stone, and bitumen had they for mortar.
Wakasemezana, “Haya njoni, tufanye matofari na tuyachome kikamilifu.” Walikuwa na matofari badala ya mawe na lami kama chokaa.
4 And they said, Go to, let us build us a city and a tower, whose top may reach unto heaven; and let us make us a name, lest we be scattered abroad upon the face of the whole earth.
Wakasema, “njoni, na tujenge mji sisi wenyewe na mnara ambao kilele chake kitafika angani, na tujifanyie jina. Kama hatutafanya, basi tutatawanyika katika uso wa nchi yote.”
5 And the LORD came down to see the city and the tower, which the children of men built.
Kwa hiyo Yahwe akashuka kuona mji na mnara ambao wazao wa Ibrahimu walikuwa wamejenga.
6 And the LORD said, Behold, the people is one, and they have all one language; and this they begin to do: and now nothing will be restrained from them, which they have imagined to do.
Yahwe akasema, “Tazama, watu hawa ni taifa moja na lugha moja, na wameanza kufanya hivi! Hivikaribuni halitashindikana jambo watakalo kusudia kulifanya.
7 Go to, let us go down, and there confound their language, that they may not understand one another's speech.
Njoni, tushuke na tuvuruge lugha yao pale, ili kwamba wasielewane.”
8 So the LORD scattered them abroad from thence upon the face of all the earth: and they left off to build the city.
Kwa hiyo Yahwe akawatawanya kutoka pale kwenda pande zote za uso wa nchi na wakaacha kujenga mji.
9 Therefore is the name of it called Babel; because the LORD did there confound the language of all the earth: and from thence did the LORD scatter them abroad upon the face of all the earth.
Kwa hiyo, jina lake ukaitwa Babeli, kwa sababu hapo Yahwe alivuruga lugha ya nchi yote na tangu pale Yahwe akawatawanya ng'ambo juu ya uso wa nchi yote.
10 These are the generations of Shem: Shem was an hundred years old, and brings forth Arphaxad two years after the flood:
Hivi ndivyo vilikuwa vizazi vya Shemu. Shemu alikuwa na umri wa miaka mia moja, na akamzaa Alfaksadi miaka miwili baada ya gharika.
11 And Shem lived after he brings forth Arphaxad five hundred years, and brings forth sons and daughters.
Shemu akaishi miaka miatano baada ya kumzaa Alfaksadi. Pia akazaa wana wengine wa kiume na wa kike.
12 And Arphaxad lived five and thirty years, and brings forth Salah:
Wakati Alfaksadi alipokuwa ameishi miaka thelathini na mitano akamzaa Shela.
13 And Arphaxad lived after he brings forth Salah four hundred and three years, and brings forth sons and daughters.
Alfaksadi aliishi miaka 403 baada ya kumzaa Shela. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
14 And Salah lived thirty years, and brings forth Eber:
Wakati Shela alipokuwa ameishi miaka thelathini, akamzaa Eberi.
15 And Salah lived after he brings forth Eber four hundred and three years, and brings forth sons and daughters.
Shela aliishi miaka 403 baada ya kumzaa Eberi. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
16 And Eber lived four and thirty years, and brings forth Peleg:
Wakati Eberi alipokuwa ameishi miaka thelathini na minne, akamzaa Pelegi.
17 And Eber lived after he brings forth Peleg four hundred and thirty years, and brings forth sons and daughters.
Eberi aliishi miaka 430 baada ya kumzaa Pelegi. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
18 And Peleg lived thirty years, and brings forth Reu:
Wakati Pelegi alipokuwa ameishi miaka thelathini, akamzaa Reu.
19 And Peleg lived after he brings forth Reu two hundred and nine years, and brings forth sons and daughters.
Pelegi aliishi miaka 209 baada ya kumza a Reu. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
20 And Reu lived two and thirty years, and brings forth Serug:
Wakati Reu alipokuwa ameishi miaka thelathini na miwili, alimzaa Serugi.
21 And Reu lived after he brings forth Serug two hundred and seven years, and brings forth sons and daughters.
Reu aliishi miaka207 baada ya kumzaa Seregu. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
22 And Serug lived thirty years, and brings forth Nahor:
Wakati Seregu alipokuwa ameishi miaka thelathini, akamzaa Nahori.
23 And Serug lived after he brings forth Nahor two hundred years, and brings forth sons and daughters.
Seregu aliishi miaka mia mbili baada ya kumzaa Nahori. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
24 And Nahor lived nine and twenty years, and brings forth Terah:
Wakati Nahori alipokuwa ameishi miaka ishirini na tisa, akamzaa Tera.
25 And Nahor lived after he brings forth Terah an hundred and nineteen years, and brings forth sons and daughters.
Nahori aliishi mika 119 baada ya kumzaa Tera. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
26 And Terah lived seventy years, and brings forth Abram, Nahor, and Haran.
Baada ya Tera kuishi miaka sabini, akamzaa Abram, Nahori, na Haran.
27 Now these are the generations of Terah: Terah brings forth Abram, Nahor, and Haran; and Haran brings forth Lot.
Hivi ndivyo vilikuwa vizazi vya Tera. Tera alimzaa Abram, Nahori, na Harani, na Harani akamzaa Lutu.
28 And Haran died before his father Terah in the land of his nativity, in Ur of the Chaldees.
Harani akafa machoni pa baba yake Tera katika nchi aliyozaliwa, katika Ur wa Wakaldayo.
29 And Abram and Nahor took them wives: the name of Abram's wife was Sarai; and the name of Nahor's wife, Milcah, the daughter of Haran, the father of Milcah, and the father of Iscah.
Abram na Nahori wakajitwalia wake. Mke wa Abram aliitwa Sarai na mke wa Nahori aliitwa Milka, binti wa Harani, aliyekuwa baba wa Milka na Iska.
30 But Sarai was barren; she had no child.
Sasa Sarai alikuwa Tasa; hakuwa na mtoto.
31 And Terah took Abram his son, and Lot the son of Haran his son's son, and Sarai his daughter in law, his son Abram's wife; and they went forth with them from Ur of the Chaldees, to go into the land of Canaan; and they came unto Haran, and dwelt there.
Tera akamtwaa Abram mwanawe, Lutu mwana wa mwanawe Harani, na Sarai mkwewe, mke wa mwanawe Abram, na kwa pamoja wakatoka Ur wa Wakaldayo, kwenda katika nchi ya Kanaani. Lakini walipofika Harani wakakaa pale.
32 And the days of Terah were two hundred and five years: and Terah died in Haran.
Tera akaishi miaka 205 kisha akafa hapao Harani.

< Genesis 11 >