< Genesis 10 >

1 Now these are the generations of the sons of Noah, Shem, Ham, and Japheth: and unto them were sons born after the flood.
Hivi ndivyo vilikuwa vizazi vya wana wa Nuhu, ambao ni, Shemu, Hamu, na Yafethi. Wana wa kiume walizaliwa kwao baada ya gharika.
2 The sons of Japheth; Gomer, and Magog, and Madai, and Javan, and Tubal, and Meshech, and Tiras.
Wana wa Yafethi walikuwa Gomeri, Magogu, Madai, Yavani, Tubali, Masheki, na Tirasi.
3 And the sons of Gomer; Ashkenaz, and Riphath, and Togarmah.
Na wana wa Gomeri walikuwa Ashikenazi, Rifathi na Togama.
4 And the sons of Javan; Elishah, and Tarshish, Kittim, and Dodanim.
Wana wa Yavani walikuwa Elisha, Tarshishi, Kitimu, na Dodanimu.
5 By these were the isles of the Gentiles divided in their lands; every one after his tongue, after their families, in their nations.
Kutoka kwa hawa watu wa pwani waligawanyika na kwenda kwenye ardhi zao, kila mtu na lugha yake, kufuatana na koo zao, kwa mataifa yao.
6 And the sons of Ham; Cush, and Mizraim, and Phut, and Canaan.
Wana wa Hamu walikuwa Kushi, Misraimu, Putu, na Kanaani.
7 And the sons of Cush; Seba, and Havilah, and Sabtah, and Raamah, and Sabtechah: and the sons of Raamah; Sheba, and Dedan.
Wana wa Kushi walikuwa Seba, Havila, Sabta, Raama, na Sabteka. Wana wa Raama walikuwa Sheba na Dedani.
8 And Cush brings forth Nimrod: he began to be a mighty one in the earth.
Kushi akamzaa Nimrodi, ambaye alikuwa hodari wa kwanza juu ya nchi.
9 He was a mighty hunter before the LORD: wherefore it is said, Even as Nimrod the mighty hunter before the LORD.
Alikuwa mwindaji mkuu mbele ya Yahwe. Hii ndiyo sababu hunenwa, “Kama Nimrod mwindaji mkuu mbele za Yahwe.”
10 And the beginning of his kingdom was Babel, and Erech, and Accad, and Calneh, in the land of Shinar.
Miji ya kwanza ya ufalme wake ilikuwa Babeli, Ereku, Akadi na Kalne, katika ichi ya Shinari.
11 Out of that land went forth Asshur, and built Nineveh, and the city Rehoboth, and Calah,
Kutoka katika nchi ile alikwenda Ashuru na akajenga Ninawi, Rehoboth- iri na Kala,
12 And Resen between Nineveh and Calah: the same is a great city.
na Raseni ambao ulikuwa kati ya Ninawi na Kala. Ulikuwa mji mkubwa.
13 And Mizraim brings forth Ludim, and Anamim, and Lehabim, and Naphtuhim,
Misraimu akazaa Waludi, Waanami, Walehabi, na Wanaftuhi,
14 And Pathrusim, and Casluhim, (out of whom came Philistim, ) and Caphtorim.
Wapathrusi na Wakasluhi ( ambao kwao Wafilisti walitokea), na Wakaftori.
15 And Canaan brings forth Sidon his first born, and Heth,
Kanaani akamzaa Sidono, mwanawe wa kwanza, na Hethi,
16 And the Jebusite, and the Amorite, and the Girgasite,
pia na Myebusi, na Mwamori, Mgirgashi,
17 And the Hivite, and the Arkite, and the Sinite,
Mhivi, Mwarki, Msini,
18 And the Arvadite, and the Zemarite, and the Hamathite: and afterward were the families of the Canaanites spread abroad.
Mwarvadi, Msemari, na Mhamathi. Baadaye koo za wakanaani zikasambaa.
19 And the border of the Canaanites was from Sidon, as you come to Gerar, unto Gaza; as you go, unto Sodom, and Gomorrah, and Admah, and Zeboim, even unto Lasha.
Mpaka wa Wakanaani ulianzia Sidoni, katika mwelekeo wa Gerari, hata Gaza, na kama kuelekea Sodoma, Gomora, Adma, na Seboimu hata Lasha.
20 These are the sons of Ham, after their families, after their tongues, in their countries, and in their nations.
Hawa walikuwa wana wa Ham, kwa koo zao, kwa lugha zao, katika ardhi zao na katika mataifa yao.
21 Unto Shem also, the father of all the children of Eber, the brother of Japheth the elder, even to him were children born.
Pia walizaliwa wana kwa Shemu, ndugu yake mkubwa wa Yafethi. Shemu pia alikuwa baba yao na watu wote wa Eberi.
22 The children of Shem; Elam, and Asshur, and Arphaxad, and Lud, and Aram.
Wana wa Shemu walikuwa Elamu, Ashuru, Alfaksadi, Ludi, na Aramu.
23 And the children of Aram; Uz, and Hul, and Gether, and Mash.
Wana wa Aramu walikuwa ni Usi, Huli, Getheri, na Mashi.
24 And Arphaxad brings forth Salah; and Salah brings forth Eber.
Arfaksadi akamzaa Sela, na Sela akamzaa Eber.
25 And unto Eber were born two sons: the name of one was Peleg; for in his days was the earth divided; and his brother's name was Joktan.
Eberi akazaa wana wawili wa kiume. Jina la mmoja aliitwa Pelegi maana katika siku zake nchi iligawanyika. Jina la ndugu yake aliitwa Yoktani.
26 And Joktan brings forth Almodad, and Sheleph, and Hazarmaveth, and Jerah,
Yoktani akamzaa Almodadi, Shelefu, Hasarmawethi, Yera,
27 And Hadoram, and Uzal, and Diklah,
Hadoram, Uzali, Dikla,
28 And Obal, and Abimael, and Sheba,
Obali, Abimaeli, Sheba,
29 And Ophir, and Havilah, and Jobab: all these were the sons of Joktan.
Ofiri, Havila, na Yobabi. Hawa wote walikuwa wana wa Yoktani.
30 And their dwelling was from Mesha, as you go unto Sephar a mount of the east.
Mpaka wao ulikuwa unaanzia Mesha, hadi Sefari, mlima wa mashariki.
31 These are the sons of Shem, after their families, after their tongues, in their lands, after their nations.
Hawa walikuwa wana wa Shemu, kulingana na koo zao na lugha zao, katika ardhi zao kulingana na mataifa yao.
32 These are the families of the sons of Noah, after their generations, in their nations: and by these were the nations divided in the earth after the flood.
Hizi zilikuwa koo za wana wa Nuhu, kulingana na vizazi vyao, kwa mataifa yao. Kutokea kwa hawa mataifa yaligawanyika na kwenda juu ya nchi baada ya gharika.

< Genesis 10 >