< Ruth 2 >

1 And Naomi had a kinsman of her husband's, a mighty man of valour, of the family of Elimelech, and his name was Boaz.
Basi Naomi alikuwa na jamaa wa upande wa mume wake, kutoka ukoo wa Elimeleki, mtu maarufu ambaye aliitwa Boazi.
2 And Ruth the Moabitess said unto Naomi: 'Let me now go to the field, and glean among the ears of corn after him in whose sight I shall find favour.' And she said unto her: 'Go, my daughter.'
Ruthu, Mmoabu, akamwambia Naomi, “Nitakwenda mashambani nikaokote mabaki ya nafaka nyuma ya yule nitakayepata kibali machoni pake.” Naomi akamwambia, “Nenda, binti yangu.”
3 And she went, and came and gleaned in the field after the reapers; and her hap was to light on the portion of the field belonging unto Boaz, who was of the family of Elimelech.
Basi akaenda, akaokota mabaki ya nafaka mashambani nyuma ya wavunaji. Ikatokea kwamba alijikuta anafanya kazi kwenye shamba lililokuwa mali ya Boazi, ambaye alitoka kwenye ukoo wa Elimeleki.
4 And, behold, Boaz came from Beth-lehem, and said unto the reapers: 'The LORD be with you.' And they answered him: 'The LORD bless thee.'
Papo hapo Boazi akarudi kutoka Bethlehemu, akawasalimu wavunaji, akasema, “Bwana awe nanyi!” Nao wakamjibu, “Bwana akubariki.”
5 Then said Boaz unto his servant that was set over the reapers: 'Whose damsel is this?'
Boazi akamuuliza msimamizi wa wavunaji, “Je, yule mwanamwali ni wa nani?”
6 And the servant that was set over the reapers answered and said: 'It is a Moabitish damsel that came back with Naomi out of the field of Moab;
Msimamizi akamjibu, “Ni yule Mmoabu aliyerudi kutoka nchi ya Moabu pamoja na Naomi.
7 and she said: Let me glean, I pray you, and gather after the reapers among the sheaves; so she came, and hath continued even from the morning until now, save that she tarried a little in the house.'
Yeye aliomba, ‘Tafadhali niruhusu niokote na kukusanya miongoni mwa miganda nyuma ya wavunaji.’ Naye ameshinda shambani tangu asubuhi pasipo kupumzika, isipokuwa kwa muda mfupi kivulini.”
8 Then said Boaz unto Ruth: 'Hearest thou not, my daughter? Go not to glean in another field, neither pass from hence, but abide here fast by my maidens.
Kisha Boazi akamwambia Ruthu, “Binti yangu, nisikilize. Usiende kuokota mabaki ya mavuno katika shamba lingine, na usiondoke hapa. Kaa hapa na hawa watumishi wangu wa kike.
9 Let thine eyes be on the field that they do reap, and go thou after them; have I not charged the young men that they shall not touch thee? and when thou art athirst, go unto the vessels, and drink of that which the young men have drawn.'
Angalia shamba wanaume wanamovuna, ufuate nyuma yao. Nimewaamuru wanaume hawa wasikuguse. Wakati wowote ukiona kiu, nenda kwenye mitungi ukanywe maji waliyoyateka wanaume hawa.”
10 Then she fell on her face, and bowed down to the ground, and said unto him: 'Why have I found favour in thy sight, that thou shouldest take cognizance of me, seeing I am a foreigner?'
Kwa ajili ya hili, akasujudu mpaka nchi, akamwambia, “Jinsi gani nimepata kibali machoni pako, hata ukanijali mimi mgeni?”
11 And Boaz answered and said unto her: 'It hath fully been told me, all that thou hast done unto thy mother-in-law since the death of thy husband; and how thou hast left thy father and thy mother, and the land of thy nativity, and art come unto a people that thou knewest not heretofore.
Boazi akamjibu, “Nimeambiwa yote uliyomtendea mama mkwe wako tangu mume wako alipofariki, na jinsi ulivyomwacha baba yako na mama yako na nchi yako ulimozaliwa, ukaja kuishi na watu ambao hukuwafahamu awali.
12 The LORD recompense thy work, and be thy reward complete from the LORD, the God of Israel, under whose wings thou art come to take refuge.'
Bwana na akulipe kwa yale uliyoyatenda. Ubarikiwe kwa wingi na Bwana, Mungu wa Israeli, ambaye umekimbilia mabawani mwake.”
13 Then she said: 'Let me find favour in thy sight, my LORD; for that thou hast comforted me, and for that thou hast spoken to the heart of thy handmaid, though I be not as one of thy handmaidens.'
Kisha Ruthu akasema, “Naomba niendelee kupata kibali machoni pako, bwana wangu. Kwa maana umenifariji na umezungumza kwa ukarimu na mjakazi wako, hata ingawa mimi si bora kama mmoja wa watumishi wako wa kike.”
14 And Boaz said unto her at meal-time: 'Come hither, and eat of the bread, and dip thy morsel in the vinegar.' And she sat beside the reapers; and they reached her parched corn, and she did eat and was satisfied, and left thereof.
Wakati wa chakula, Boazi akamwambia Ruthu, “Karibia hapa. Kula mkate na uchovye ndani ya siki.” Alipoketi pamoja na wavunaji, akampa nafaka zilizookwa. Akala kiasi alichotaka na kusaza.
15 And when she was risen up to glean, Boaz commanded his young men, saying: 'Let her glean even among the sheaves, and put her not to shame.
Alipoinuka ili kuokota mabaki ya nafaka, Boazi akawaagiza watu wake, “Hata kama atakusanya kati ya miganda, msimzuie.
16 And also pull out some for her of purpose from the bundles, and leave it, and let her glean, and rebuke her not.'
Badala yake, toeni masuke katika miganda, mwachieni ayaokote, na msimkemee.”
17 So she gleaned in the field until even; and she beat out that which she had gleaned, and it was about an ephah of barley.
Basi Ruthu akaokota masazo shambani hata jioni. Akatwanga ile shayiri aliyokusanya, ikajaa efa moja.
18 And she took it up, and went into the city; and her mother-in-law saw what she had gleaned; and she brought forth and gave to her that which she had left after she was satisfied.
Akaibeba na kuelekea mjini, naye mama mkwe wake akaona jinsi alivyoweza kuokota nafaka nyingi. Pia Ruthu akachukua kile alichobakiza baada ya kula na kushiba, akampa.
19 And her mother-in-law said unto her: 'Where hast thou gleaned to-day? and where wroughtest thou? blessed be he that did take knowledge of thee.' And she told her mother-in-law with whom she had wrought, and said: 'The man's name with whom I wrought to-day is Boaz.'
Basi mkwewe akamuuliza, “Je, umeokota wapi leo? Umefanya kazi wapi? Abarikiwe mtu yule aliyekujali.” Ndipo Ruthu akamwambia mama mkwe wake juu ya yule ambaye yeye alikuwa amefanyia kazi katika shamba lake. Akasema, “Yule mtu niliyefanyia kazi kwake leo, anaitwa Boazi.”
20 And Naomi said unto her daughter-in-law: 'Blessed be he of the LORD, who hath not left off His kindness to the living and to the dead.' And Naomi said unto her: 'The man is nigh of kin unto us, one of our near kinsmen.'
Naye Naomi akamwambia mkwewe, “Bwana ambariki! Hakuacha kuonyesha fadhili zake kwa walio hai na kwa waliokufa.” Pia akamwambia, “Huyo mtu ni mmoja wa jamaa yetu wa karibu anayestahili kutukomboa.”
21 And Ruth the Moabitess said: 'Yea, he said unto me: Thou shalt keep fast by my young men, until they have ended all my harvest.'
Kisha Ruthu, Mmoabu, akasema, “Hata aliniambia, ‘Kaa pamoja na watumishi wangu mpaka watakapomaliza kuvuna nafaka yangu yote.’”
22 And Naomi said unto Ruth her daughter-in-law: 'It is good, my daughter, that thou go out with his maidens, and that thou be not met in any other field.'
Kisha Naomi akamwambia Ruthu mkwewe, “Binti yangu, itakuwa vyema wewe ufuatane na wasichana wake, kwa sababu katika shamba la mtu mwingine wanaweza kukudhuru.”
23 So she kept fast by the maidens of Boaz to glean unto the end of barley harvest and of wheat harvest; and she dwelt with her mother-in-law.
Kwa hivyo Ruthu akafuatana na watumishi wa kike wa Boazi, akaokota mpaka mwisho wa mavuno ya shayiri na ya ngano. Naye aliishi na mama mkwe wake.

< Ruth 2 >