< Ruth 4 >

1 Now Boaz went up to the gate, and sat him down there; and, behold, the near kinsman of whom Boaz spoke came by; unto whom he said: 'Ho, such a one! turn aside, sit down here.' And he turned aside, and sat down.
Boazi akakwea mpaka kwenye lango la mji, akaketi pale. Yule mtu wa jamaa aliyekuwa wa karibu wa kukomboa, ambaye Boazi alimtaja, akaja. Boazi akasema, “Njoo hapa, rafiki yangu. Karibu uketi.” Naye akakaribia, akaketi.
2 And he took ten men of the elders of the city, and said: 'Sit ye down here.' And they sat down.
Boazi akatwaa watu kumi miongoni mwa wazee wa mji, akawaambia, “Ketini hapa.” Nao wakaketi.
3 And he said unto the near kinsman: 'Naomi, that is come back out of the field of Moab, selleth the parcel of land, which was our brother Elimelech's;
Kisha akamwambia yule jamaa wa karibu wa kukomboa, “Naomi, aliyerudi hapa kutoka nchi ya Moabu, anauza sehemu ya ardhi iliyokuwa mali ya ndugu yetu Elimeleki.
4 and I thought to disclose it unto thee, saying: Buy it before them that sit here, and before the elders of my people. If thou wilt redeem it, redeem it; but if it will not be redeemed, then tell me, that I may know; for there is none to redeem it beside thee; and I am after thee.' And he said: 'I will redeem it.'
Nami niliwaza nikujulishe wewe na kukuambia uinunue mbele ya hawa waliopo hapa, na mbele ya wazee wa watu wangu. Kama wewe utaikomboa, haya fanya hivyo. Lakini kama hutaikomboa, uniambie, ili nijue. Kwa kuwa hakuna mtu mwingine mwenye haki ya kuikomboa ila wewe na baada yako ni mimi.” Naye akasema, “Nitaikomboa mimi.”
5 Then said Boaz: 'What day thou buyest the field of the hand of Naomi — hast thou also bought of Ruth the Moabitess, the wife of the dead, to raise up the name of the dead upon his inheritance?'
Ndipo Boazi akasema “Siku utakaponunua hiyo ardhi kutoka kwa Naomi na Ruthu, Mmoabu, itakubidi kumchukua pia huyo mjane, ili kudumisha jina la marehemu pamoja na mali yake.”
6 And the near kinsman said: 'I cannot redeem it for myself, lest I mar mine own inheritance; take thou my right of redemption on thee; for I cannot redeem it.' —
Aliposikia hili, yule jamaa wa karibu wa kukomboa akasema, “Basi mimi sitaweza kuikomboa, kwa sababu inaonekana nitauhatarisha urithi wangu. Wewe ikomboe mwenyewe. Mimi sitaweza.”
7 Now this was the custom in former time in Israel concerning redeeming and concerning exchanging, to confirm all things: a man drew off his shoe, and gave it to his neighbour; and this was the attestation in Israel. —
(Basi katika siku za kale huko Israeli, ili kukamilisha tendo la kukomboa na kukabidhiana mali, mmoja huvua kiatu chake na kumpatia mwingine. Hii ilikuwa ni njia ya kuhalalisha mabadilishano katika Israeli.)
8 So the near kinsman said unto Boaz: 'Buy it for thyself.' And he drew off his shoe.
Basi yule jamaa wa karibu wa kukomboa akamwambia Boazi, “Wewe inunue mwenyewe.” Naye huyo jamaa akavua kiatu chake.
9 And Boaz said unto the elders, and unto all the people: 'Ye are witnesses this day, that I have bought all that was Elimelech's, and all that was Chilion's and Mahlon's, of the hand of Naomi.
Kisha Boazi akawatangazia wazee na watu wote waliokuwepo, “Leo ninyi ni mashahidi kwamba mimi nimenunua kutoka kwa Naomi yote yaliyokuwa mali ya Elimeleki, Kilioni na Maloni.
10 Moreover Ruth the Moabitess, the wife of Mahlon, have I acquired to be my wife, to raise up the name of the dead upon his inheritance, that the name of the dead be not cut off from among his brethren, and from the gate of his place; ye are witnesses this day.'
Nimemchukua pia Ruthu, Mmoabu, mjane wa Maloni, awe mke wangu, ili kuendeleza jina la marehemu pamoja na mali zake, ili jina lake marehemu lisitoweke miongoni mwa jamaa yake, wala katika kumbukumbu za mji wake. Leo hivi ninyi ni mashahidi!”
11 And all the people that were in the gate, and the elders, said: 'We are witnesses. The LORD make the woman that is come into thy house like Rachel and like Leah, which two did build the house of Israel; and do thou worthily in Ephrath, and be famous in Beth-lehem;
Kisha wazee pamoja na watu wote waliokuwa langoni wakasema, “Sisi ni mashahidi. Bwana na amfanye mwanamke huyu aingiaye nyumbani mwako kuwa kama Raheli na kama Lea, wale wanawake wawili ambao pamoja waliijenga nyumba ya Israeli. Nawe ufanikiwe katika Efrathi na uwe mashuhuri katika Bethlehemu.
12 and let thy house be like the house of Perez, whom Tamar bore unto Judah, of the seed which the LORD shall give thee of this young woman.'
Kupitia kwa watoto ambao Bwana atakupa kutokana na huyu mwanamwali, jamaa yako na ifanane na ya Peresi, ambaye Tamari alimzalia Yuda.”
13 So Boaz took Ruth, and she became his wife; and he went in unto her, and the LORD gave her conception, and she bore a son.
Basi Boazi akamwoa Ruthu, naye akawa mke wake. Alipoingia kwake, Bwana akamjalia Ruthu, naye akapata mimba, akamzaa mtoto wa kiume.
14 And the women said unto Naomi: 'Blessed be the LORD, who hath not left thee this day without a near kinsman, and let his name be famous in Israel.
Wanawake wakamwambia Naomi: “Ahimidiwe Bwana, asiyekuacha bila kuwa na jamaa wa karibu wa kukomboa. Na awe mashuhuri katika Israeli yote!
15 And he shall be unto thee a restorer of life, and a nourisher of thine old age; for thy daughter-in-law, who loveth thee, who is better to thee than seven sons, hath borne him.'
Atakurejeshea uhai wako na kukuangalia katika siku za uzee wako. Kwa maana mkweo ambaye anakupenda, na ambaye kwako ni bora zaidi ya watoto wa kiume saba, ndiye alimzaa.”
16 And Naomi took the child, and laid it in her bosom, and became nurse unto it.
Basi Naomi akamchukua yule mtoto, akampakata na akawa mlezi wake.
17 And the women her neighbours gave it a name, saying: 'There is a son born to Naomi'; and they called his name Obed; he is the father of Jesse, the father of David.
Wanawake waliokuwa jirani zake wakasema, “Naomi ana mtoto wa kiume.” Wakamwita jina lake Obedi. Yeye ndiye baba yake Yese, aliye baba yake Daudi.
18 Now these are the generations of Perez: Perez begot Hezron;
Hivi ndivyo vizazi vya Peresi: Peresi alimzaa Hesroni,
19 and Hezron begot Ram, and Ram begot Amminadab;
Hesroni akamzaa Ramu, Ramu akamzaa Aminadabu,
20 and Amminadab begot Nahshon, and Nahshon begot Salmon;
Aminadabu akamzaa Nashoni, Nashoni akamzaa Salmoni,
21 and Salmon begot Boaz, and Boaz begot Obed;
Salmoni akamzaa Boazi, Boazi akamzaa Obedi,
22 and Obed begot Jesse, and Jesse begot David.
Obedi akamzaa Yese, na Yese akamzaa Daudi.

< Ruth 4 >