< Psalms 73 >

1 BOOK III A Psalm of Asaph. Surely God is good to Israel, even to such as are pure in heart.
Zaburi ya Asafu. Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale ambao mioyo yao ni safi.
2 But as for me, my feet were almost gone; my steps had well nigh slipped.
Bali kwangu mimi, miguu yangu ilikuwa karibu kuteleza; nilikuwa karibu mguu wangu kuachia uliposimama.
3 For I was envious at the arrogant, when I saw the prosperity of the wicked.
Kwa maana niliwaonea wivu wenye kujivuna nilipoona kufanikiwa kwa waovu.
4 For there are no pangs at their death, and their body is sound.
Wao hawana taabu, miili yao ina afya na nguvu.
5 In the trouble of man they are not; neither are they plagued like men.
Hawapati shida zinazowataabisha watu wengine, wala hawapati mapigo kama wanadamu wengine.
6 Therefore pride is as a chain about their neck; violence covereth them as a garment.
Kwa hiyo kiburi ni mkufu wao, wamejivika jeuri.
7 Their eyes stand forth from fatness; they are gone beyond the imaginations of their heart.
Uovu hutoka katika mioyo yao iliyokufa ganzi, majivuno maovu kutoka mioyoni mwao hauna kikomo.
8 They scoff, and in wickedness utter oppression; they speak as if there were none on high.
Hudhihaki na kusema kwa ukorofi, katika majivuno yao wanatishia kutesa.
9 They have set their mouth against the heavens, and their tongue walketh through the earth.
Vinywa vyao huweka madai hata kwa mbingu, nazo ndimi zao humiliki duniani.
10 Therefore His people return hither; and waters of fullness are drained out by them.
Kwa hiyo watu wao huwageukia na kunywa maji tele.
11 And they say: 'How doth God know? And is there knowledge in the Most High?'
Wanasema, “Mungu awezaje kujua? Je, Yeye Aliye Juu Sana anayo maarifa?”
12 Behold, such are the wicked; and they that are always at ease increase riches.
Hivi ndivyo walivyo waovu: siku zote hawajali, wanaongezeka katika utajiri.
13 Surely in vain have I cleansed my heart, and washed my hands in innocency;
Hakika nimeuweka moyo wangu safi bure, ni bure nimenawa mikono yangu nisiwe na hatia.
14 For all the day have I been plagued, and my chastisement came every morning.
Mchana kutwa nimetaabika, nimeadhibiwa kila asubuhi.
15 If I had said: 'I will speak thus', behold, I had been faithless to the generation of Thy children.
Kama ningesema, “Nitasema hivi,” ningelikuwa nimewasaliti watoto wako.
16 And when I pondered how I might know this, it was wearisome in mine eyes;
Nilipojaribu kuelewa haya yote, yalikuwa magumu kwangu kuelewa.
17 Until I entered into the sanctuary of God, and considered their end.
Mpaka nilipoingia patakatifu pa Mungu, ndipo nilipotambua mwisho wao.
18 Surely Thou settest them in slippery places; Thou hurlest them down to utter ruin.
Hakika unawaweka mahali pa utelezi, unawaangusha chini kwa uharibifu.
19 How are they become a desolation in a moment! They are wholly consumed by terrors.
Tazama jinsi wanavyoangamizwa ghafula, wanatoweshwa kabisa na vitisho!
20 As a dream when one awaketh, so, O Lord, when Thou arousest Thyself, Thou wilt despise their semblance.
Kama ndoto mtu aamkapo, hivyo wakati uinukapo, Ee Bwana, utawatowesha kama ndoto.
21 For my heart was in a ferment, and I was pricked in my reins.
Wakati moyo wangu ulipohuzunishwa, na roho yangu ilipotiwa uchungu,
22 But I was brutish, and ignorant; I was as a beast before Thee.
nilikuwa mpumbavu na mjinga, nilikuwa mnyama mkatili mbele yako.
23 Nevertheless I am continually with Thee; Thou holdest my right hand.
Hata hivyo niko pamoja nawe siku zote, umenishika mkono wangu wa kuume.
24 Thou wilt guide me with Thy counsel, and afterward receive me with glory.
Unaniongoza kwa shauri lako, hatimaye utaniingiza katika utukufu.
25 Whom have I in heaven but Thee? And beside Thee I desire none upon earth.
Nani niliye naye mbinguni ila wewe? Dunia haina chochote ninachokitamani ila wewe.
26 My flesh and my heart faileth; but God is the rock of my heart and my portion for ever.
Mwili na moyo wangu vyaweza kushindwa, bali Mungu ni nguvu ya moyo wangu na fungu langu milele.
27 For, lo, they that go far from Thee shall perish; Thou dost destroy all them that go astray from Thee.
Wale walio mbali nawe wataangamia, unawaangamiza wote wasio waaminifu kwako.
28 But as for me, the nearness of God is my good; I have made the Lord GOD my refuge, that I may tell of all Thy works.
Lakini kwangu mimi, ni vyema kuwa karibu na Mungu. Nimemfanya Bwana Mwenyezi kimbilio langu; nami nitayasimulia matendo yako yote.

< Psalms 73 >