< Psalms 71 >

1 In Thee, O LORD, have I taken refuge; let me never be ashamed.
Ee Bwana, nimekukimbilia wewe, usiache nikaaibika kamwe.
2 Deliver me in Thy righteousness, and rescue me; incline Thine ear unto me, and save me.
Kwa haki yako uniponye na kuniokoa, unitegee sikio lako uniokoe.
3 Be Thou to me a sheltering rock, whereunto I may continually resort, which Thou hast appointed to save me; for Thou art my rock and my fortress.
Uwe kwangu mwamba wa kimbilio, mahali nitakapokimbilia kila wakati; toa amri ya kuniokoa, kwa kuwa wewe ni mwamba wangu na ngome yangu.
4 O my God, rescue me out of the hand of the wicked, out of the grasp of the unrighteous and ruthless man.
Ee Mungu wangu uniokoe kutoka kwenye mkono wa mwovu, kutoka kwenye makucha ya watu wabaya na wakatili.
5 For Thou art my hope; O Lord GOD, my trust from my youth.
Kwa kuwa umekuwa tumaini langu, Ee Bwana Mwenyezi, tegemeo langu tangu ujana wangu.
6 Upon Thee have I stayed myself from birth; Thou art He that took me out of my mother's womb; my praise is continually of Thee.
Tangu kuzaliwa nimekutegemea wewe, ulinitoa tumboni mwa mama yangu. Nitakusifu wewe daima.
7 I am as a wonder unto many; but Thou art my strong refuge.
Nimekuwa kama kioja kwa wengi, lakini wewe ni kimbilio langu imara.
8 My mouth shall be filled with Thy praise, and with Thy glory all the day.
Kinywa changu kimejazwa sifa zako, nikitangaza utukufu wako mchana kutwa.
9 Cast me not off in the time of old age; when my strength faileth, forsake me not.
Usinitupe wakati wa uzee, wala usiniache nguvu zangu zinapopungua.
10 For mine enemies speak concerning me, and they that watch for my soul take counsel together,
Kwa maana adui zangu wananisengenya, wale wanaonivizia kuniua wafanya hila.
11 Saying: 'God hath forsaken him; pursue and take him; for there is none to deliver.'
Wanasema, “Mungu amemwacha, mkimbilieni mkamkamate, kwani hakuna wa kumwokoa.”
12 O God, be not far from me; O my God, make haste to help me.
Ee Mungu, usiwe mbali nami, njoo haraka kunisaidia, Ee Mungu wangu.
13 Let them be ashamed and consumed that are adversaries to my soul; let them be covered with reproach and confusion that seek my hurt.
Washtaki wangu na waangamie kwa aibu, wale wanaotaka kunidhuru na wafunikwe kwa dharau na fedheha.
14 But as for me, I will hope continually, and will praise Thee yet more and more.
Lakini mimi, nitatumaini siku zote, nitakusifu zaidi na zaidi.
15 My mouth shall tell of Thy righteousness, and of Thy salvation all the day; for I know not the numbers thereof.
Kinywa changu kitasimulia haki yako, wokovu wako mchana kutwa, ingawa sifahamu kipimo chake.
16 I will come with Thy mighty acts, O Lord GOD; I will make mention of Thy righteousness, even of Thine only.
Ee Bwana Mwenyezi, nitakuja na kutangaza matendo yako makuu, nitatangaza haki yako, yako peke yako.
17 O God, Thou hast taught me from my youth; and until now do I declare Thy wondrous works.
Ee Mungu, umenifundisha tangu ujana wangu, hadi leo ninatangaza matendo yako ya ajabu.
18 And even unto old age and hoary hairs, O God, forsake me not; until I have declared Thy strength unto the next generation, Thy might to every one that is to come.
Ee Mungu, usiniache, hata niwapo mzee wa mvi, mpaka nitangaze uwezo wako kwa kizazi kijacho, nguvu zako kwa wote watakaokuja baadaye.
19 Thy righteousness also, O God, which reacheth unto high heaven; Thou who hast done great things, O God, who is like unto Thee?
Ee Mungu, haki yako imefika juu katika mbingu, wewe ambaye umefanya mambo makuu. Ee Mungu, ni nani aliye kama wewe?
20 Thou, who hast made me to see many and sore troubles, wilt quicken me again, and bring me up again from the depths of the earth.
Ingawa umenifanya nipate taabu, nyingi na chungu, utanihuisha tena, kutoka vilindi vya dunia utaniinua tena.
21 Thou wilt increase my greatness, and turn and comfort me.
Utaongeza heshima yangu na kunifariji tena.
22 I also will give thanks unto Thee with the psaltery, even unto Thy truth, O my God; I will sing praises unto Thee with the harp, O Thou Holy One of Israel.
Ee Mungu wangu, nitakusifu kwa kinubi kwa ajili ya uaminifu wako; Ee Uliye Mtakatifu wa Israeli, nitakuimbia sifa kwa zeze.
23 My lips shall greatly rejoice when I sing praises unto Thee; and my soul, which Thou hast redeemed.
Midomo yangu itapaza sauti kwa furaha ninapokuimbia sifa, mimi, ambaye umenikomboa.
24 My tongue also shall tell of Thy righteousness all the day; for they are ashamed, for they are abashed, that seek my hurt.
Ulimi wangu utasimulia matendo yako ya haki mchana kutwa, kwa maana wale waliotaka kunidhuru, wameaibishwa na kufadhaishwa.

< Psalms 71 >