< Psalms 56 >

1 For the Leader; upon Jonath-elem-rehokim. A Psalm of David; Michtam; when the Philistines took him in Gath. Be gracious unto me, O God, for man would swallow me up; all the day he fighting oppresseth me.
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Njiwa mkimya wa mbali.” Utenzi wa Daudi. Baada ya kukamatwa na Wafilisti huko Gathi. Ee Mungu unihurumie, maana watu wananifuatia vikali; mchana kutwa wanazidisha mashambulizi yao.
2 They that lie in wait for me would swallow me up all the day; for they are many that fight against me, O Most High,
Wasingiziaji wangu wananifuatia mchana kutwa, wengi wananishambulia kwa kiburi chao.
3 In the day that I am afraid, I will put my trust in Thee.
Wakati ninapoogopa, nitakutumaini wewe.
4 In God — I will praise His word — in God do I trust, I will not be afraid; what can flesh do unto me?
Katika Mungu, ambaye neno lake ninalisifu, katika Mungu ninatumaini; sitaogopa. Mwanadamu apatikanaye na kufa, atanitenda nini?
5 All the day they trouble mine affairs; all their thoughts are against me for evil.
Mchana kutwa wanayageuza maneno yangu, siku zote wanapanga shauri la kunidhuru.
6 They gather themselves together, they hide themselves, they mark my steps; according as they have waited for my soul.
Wananifanyia hila, wanajificha, wanatazama hatua zangu, wakiwa na shauku ya kuutoa uhai wangu.
7 Because of iniquity cast them out; in anger bring down the peoples, O God.
Wasiepuke kwa vyovyote, Ee Mungu, katika hasira yako yaangushe mataifa.
8 Thou has counted my wanderings; put Thou my tears into Thy bottle; are they not in Thy book?
Andika maombolezo yangu, orodhesha machozi yangu katika gombo lako: je, haya hayapo katika kumbukumbu zako?
9 Then shall mine enemies turn back in the day that I call; this I know, that God is for me.
Ndipo adui zangu watarudi nyuma ninapoita msaada. Kwa hili nitajua kwamba Mungu yuko upande wangu.
10 In God — I will praise His word — in the LORD — I will praise His word —
Katika Mungu, ambaye neno lake ninalisifu, katika Bwana, ambaye neno lake ninalisifu,
11 In God do I trust, I will not be afraid; what can man do unto me?
katika Mungu ninatumaini, sitaogopa. Mwanadamu anaweza kunitenda nini?
12 Thy vows are upon me, O God; I will render thank-offerings unto Thee.
Ee Mungu, nina nadhiri kwako, nitakutolea wewe sadaka zangu za shukrani.
13 For thou hast delivered my soul from death; hast Thou not delivered my feet from stumbling? that I may walk before God in the light of the living.
Kwa kuwa umeniokoa toka kwenye mauti na miguu yangu kwenye kujikwaa, ili niweze kuenenda mbele za Mungu katika nuru ya uzima.

< Psalms 56 >