< Psalms 48 >

1 A Song; a Psalm of the sons of Korah. Great is the LORD, and highly to be praised, in the city of our God, His holy mountain,
Wimbo. Zaburi ya wana wa Kora. Bwana ni mkuu, anayestahili kusifiwa sana, katika mji wa Mungu wetu, mlima wake mtakatifu.
2 Fair in situation, the joy of the whole earth; even mount Zion, the uttermost parts of the north, the city of the great King.
Ni mzuri katika kuinuka kwake juu sana, furaha ya dunia yote. Kama vilele vya juu sana vya Safoni ni Mlima Sayuni, mji wa Mfalme Mkuu.
3 God in her palaces hath made Himself known for a stronghold.
Mungu yuko katika ngome zake; amejionyesha mwenyewe kuwa ngome yake.
4 For, lo, the kings assembled themselves, they came onward together.
Wakati wafalme walipounganisha nguvu, waliposonga mbele pamoja,
5 They saw, straightway they were amazed; they were affrighted, they hasted away.
walimwona nao wakashangaa, wakakimbia kwa hofu.
6 Trembling took hold of them there, pangs, as of a woman in travail.
Kutetemeka kuliwashika huko, maumivu kama ya mwanamke mwenye utungu wa kuzaa.
7 With the east wind Thou breakest the ships of Tarshish.
Uliwaangamiza kama meli za Tarshishi zilizovunjwa na upepo wa mashariki.
8 As we have heard, so have we seen in the city of the LORD of hosts, in the city of our God — God establish it for ever. (Selah)
Kama tulivyokuwa tumesikia, ndivyo tulivyoona katika mji wa Bwana Mwenye Nguvu Zote, katika mji wa Mungu wetu: Mungu ataufanya uwe salama milele.
9 We have thought on Thy lovingkindness, O God, in the midst of Thy temple.
Ee Mungu, hekaluni mwako tunatafakari upendo wako usiokoma.
10 As is Thy name, O God, so is Thy praise unto the ends of the earth; Thy right hand is full of righteousness.
Ee Mungu, kama jina lako lilivyo, sifa zako zinafika hadi miisho ya dunia, mkono wako wa kuume umejazwa na haki.
11 Let mount Zion be glad, let the daughters of Judah rejoice, because of Thy judgments.
Mlima Sayuni unashangilia, vijiji vya Yuda vinafurahi kwa sababu ya hukumu zako.
12 Walk about Zion, and go round about her; count the towers thereof.
Tembeeni katika Sayuni, uzungukeni mji, hesabuni minara yake;
13 Mark ye well her ramparts, traverse her palaces; that ye may tell it to the generation following.
yatafakarini vyema maboma yake, angalieni ngome zake, ili mpate kusimulia habari zake kwa kizazi kijacho.
14 For such is God, our God, for ever and ever; He will guide us eternally.
Kwa kuwa huyu Mungu ni Mungu wetu milele na milele; atakuwa kiongozi wetu hata mwisho.

< Psalms 48 >