< Genesis 16 >

1 Now Sarai Abram's wife bore him no children; and she had a handmaid, an Egyptian, whose name was Hagar.
Basi Sarai, mkewe Abramu, alikuwa hajamzalia watoto. Lakini alikuwa na mtumishi wa kike Mmisri jina lake Hagari,
2 And Sarai said unto Abram: 'Behold now, the LORD hath restrained me from bearing; go in, I pray thee, unto my handmaid; it may be that I shall be builded up through her.' And Abram hearkened to the voice of Sarai.
hivyo Sarai akamwambia Abramu, “Bwana amenizuilia kupata watoto. Nenda, ukakutane kimwili na mtumishi wangu wa kike, huenda nitaweza kupata watoto kupitia kwake.” Abramu akakubaliana na lile Sarai alilosema.
3 And Sarai Abram's wife took Hagar the Egyptian, her handmaid, after Abram had dwelt ten years in the land of Canaan, and gave her to Abram her husband to be his wife.
Hivyo baada ya Abramu kuishi katika nchi ya Kanaani miaka kumi, Sarai akamchukua mtumishi wake wa kike wa Kimisri, Hagari na kumpa mumewe awe mke wake.
4 And he went in unto Hagar, and she conceived; and when she saw that she had conceived, her mistress was despised in her eyes.
Akakutana kimwili na Hagari, naye akapata mimba. Hagari alipojua kuwa ana mimba, alianza kumdharau Sarai.
5 And Sarai said unto Abram: 'My wrong be upon thee: I gave my handmaid into thy bosom; and when she saw that she had conceived, I was despised in her eyes: the LORD judge between me and thee.'
Ndipo Sarai akamwambia Abramu, “Unawajibika na manyanyaso ninayoyapata. Nilimweka mtumishi wangu mikononi mwako, sasa kwa vile anajua kwamba ana mimba, ananidharau mimi. Bwana na aamue kati yako na mimi.”
6 But Abram said unto Sarai: 'Behold, thy maid is in thy hand; do to her that which is good in thine eyes.' And Sarai dealt harshly with her, and she fled from her face.
Abramu akamwambia, “Mtumishi wako yuko mikononi mwako. Mtendee lolote unalofikiri ni bora zaidi.” Ndipo Sarai akamtesa Hagari, hivyo akamtoroka.
7 And the angel of the LORD found her by a fountain of water in the wilderness, by the fountain in the way to Shur.
Malaika wa Bwana akamkuta Hagari karibu na chemchemi huko jangwani; ilikuwa chemchemi ile iliyokuwa kando ya barabara iendayo Shuri.
8 And he said: 'Hagar, Sarai's handmaid, whence camest thou? and whither goest thou?' And she said: 'I flee from the face of my mistress Sarai.'
Malaika akamwambia, “Hagari, mtumishi wa Sarai, umetokea wapi, na unakwenda wapi?” Akamjibu, “Ninamkimbia bibi yangu Sarai.”
9 And the angel of the LORD said unto her: 'Return to thy mistress, and submit thyself under her hands.'
Ndipo malaika wa Bwana akamwambia, “Rudi kwa bibi yako ukajishushe chini yake.”
10 And the angel of the LORD said unto her: 'I will greatly multiply thy seed, that it shall not be numbered for multitude.
Malaika akaendelea akasema, “Nitazidisha wazao wako, hivi kwamba watakuwa wengi mno wasiohesabika.”
11 And the angel of the LORD said unto her: 'Behold, thou art with child, and shalt bear a son; and thou shalt call his name Ishmael, because the LORD hath heard thy affliction.
Pia malaika wa Bwana akamwambia: “Wewe sasa una mimba nawe utamzaa mwana. Utamwita jina lake Ishmaeli, kwa sababu Bwana amesikia juu ya huzuni yako.
12 And he shall be a wild ass of a man: his hand shall be against every man, and every man's hand against him; and he shall dwell in the face of all his brethren.'
Atakuwa punda-mwitu katikati ya wanadamu, mkono wake utakuwa dhidi ya kila mtu na mkono wa kila mtu dhidi yake, naye ataishi kwa uhasama na ndugu zake wote.”
13 And she called the name of the LORD that spoke unto her, Thou art a God of seeing; for she said: 'Have I even here seen Him that seeth Me?'
Hagari akampa Bwana aliyezungumza naye jina hili: “Wewe ndiwe Mungu unionaye mimi,” kwa maana alisema, “Sasa nimemwona yeye anayeniona mimi.”
14 Wherefore the well was called 'Beer-lahai-roi; behold, it is between Kadesh and Bered.
Ndiyo sababu kisima kile kikaitwa Beer-Lahai-Roi, ambacho bado kipo huko hata leo kati ya Kadeshi na Beredi.
15 And Hagar bore Abram a son; and Abram called the name of his son, whom Hagar bore, Ishmael.
Hivyo Hagari akamzalia Abramu mwana, naye Abramu akamwita huyo mwana Hagari aliyemzalia, Ishmaeli.
16 And Abram was fourscore and six years old, when Hagar bore Ishmael to Abram.
Abramu alikuwa na umri wa miaka themanini na sita wakati Hagari alipomzalia Ishmaeli.

< Genesis 16 >