< Genesis 15 >

1 After these things the word of the LORD came unto Abram in a vision, saying: 'Fear not, Abram, I am thy shield, thy reward shall be exceeding great.'
Baada ya jambo hili, neno la Bwana likamjia Abramu katika maono: “Usiogope, Abramu. Mimi ni ngao yako, na thawabu yako kubwa sana.”
2 And Abram said: 'O Lord GOD, what wilt Thou give me, seeing I go hence childless, and he that shall be possessor of my house is Eliezer of Damascus?'
Lakini Abramu akasema, “Ee Bwana Mwenyezi, utanipa nini na mimi sina hata mtoto na atakayerithi nyumba yangu ni huyu Eliezeri Mdameski?”
3 And Abram said: 'Behold, to me Thou hast given no seed, and, lo, one born in my house is to be mine heir.'
Abramu akasema, “Hukunipa watoto, hivyo mtumishi katika nyumba yangu ndiye atakuwa mrithi wangu.”
4 And, behold, the word of the LORD came unto him, saying: 'This man shall not be thine heir; but he that shall come forth out of thine own bowels shall be thine heir.'
Ndipo neno la Bwana lilipomjia: “Mtu huyu hatakuwa mrithi wako, bali mwana atakayetoka katika viuno vyako mwenyewe ndiye atakayekuwa mrithi wako.”
5 And He brought him forth abroad, and said: 'Look now toward heaven, and count the stars, if thou be able to count them'; and He said unto him: 'So shall thy seed be.'
Akamtoa nje na kusema, “Tazama juu kuelekea mbinguni na uhesabu nyota, kama hakika utaweza kuzihesabu.” Ndipo akamwambia, “Hivyo ndivyo uzao wako utakavyokuwa.”
6 And he believed in the LORD; and He counted it to him for righteousness.
Abramu akamwamini Bwana, naye kwake hili likahesabiwa kuwa haki.
7 And He said unto him: 'I am the LORD that brought thee out of Ur of the Chaldees, to give thee this land to inherit it.'
Pia akamwambia, “Mimi ndimi Bwana, niliyekutoa toka Uru ya Wakaldayo nikupe nchi hii uimiliki.”
8 And he said: 'O Lord GOD, whereby shall I know that I shall inherit it?'
Lakini Abramu akasema, “Ee Bwana Mwenyezi, nitawezaje kujua kwamba nitapata kuimiliki?”
9 And He said unto him: 'Take Me a heifer of three years old, and a she-goat of three years old, and a ram of three years old, and a turtle-dove, and a young pigeon.'
Ndipo Bwana akamwambia, “Niletee mtamba wa ngʼombe, mbuzi na kondoo dume, kila mmoja wa miaka mitatu, pamoja na hua na kinda la njiwa.”
10 And he took him all these, and divided them in the midst, and laid each half over against the other; but the birds divided he not.
Abramu akamletea hivi vyote, akampasua kila mnyama vipande viwili, akavipanga kila kimoja kuelekea mwenzake, lakini hata hivyo ndege, hakuwapasua vipande viwili.
11 And the birds of prey came down upon the carcasses, and Abram drove them away.
Kisha ndege walao nyama wakatua juu ya mizoga, lakini Abramu akawafukuza.
12 And it came to pass, that, when the sun was going down, a deep sleep fell upon Abram; and, lo, a dread, even a great darkness, fell upon him.
Wakati jua lilipokuwa linatua, Abramu akashikwa na usingizi mzito, giza nene na la kutisha likaja juu yake.
13 And He said unto Abram: 'Know of a surety that thy seed shall be a stranger in a land that is not theirs, and shall serve them; and they shall afflict them four hundred years;
Kisha Bwana akamwambia, “Ujue hakika kwamba wazao wako watakuwa wageni kwenye nchi ambayo si yao, nao watafanywa watumwa na kuteswa kwa miaka mia nne.
14 and also that nation, whom they shall serve, will I judge; and afterward shall they come out with great substance.
Lakini nitaliadhibu taifa lile watakalolitumikia kama watumwa, na baadaye watatoka huko na mali nyingi.
15 But thou shalt go to thy fathers in peace; thou shalt be buried in a good old age.
Wewe, hata hivyo utakwenda kwa baba zako kwa amani na kuzikwa katika uzee mwema.
16 And in the fourth generation they shall come back hither; for the iniquity of the Amorite is not yet full.'
Katika kizazi cha nne wazao wako watarudi hapa, kwa maana dhambi ya Waamori bado haijafikia kipimo kilichojaa.”
17 And it came to pass, that, when the sun went down, and there was thick darkness, behold a smoking furnace, and a flaming torch that passed between these pieces.
Wakati jua lilipokuwa limezama na giza limeingia, tanuru la moshi na mwali wa moto unaowaka vikatokea na kupita kati ya vile vipande vya nyama.
18 In that day the LORD made a covenant with Abram, saying: 'Unto thy seed have I given this land, from the river of Egypt unto the great river, the river Euphrates;
Siku hiyo Bwana akafanya Agano na Abramu, na kumwambia, “Nitawapa wazao wako nchi hii, kuanzia Kijito cha Misri hadi mto ule mkubwa, Frati,
19 the Kenite, and the Kenizzite, and the Kadmonite,
yaani nchi ya Wakeni, Wakenizi, Wakadmoni,
20 and the Hittite, and the Perizzite, and the Rephaim,
Wahiti, Waperizi, Warefai,
21 and the Amorite, and the Canaanite, and the Girgashite, and the Jebusite.'
Waamori, Wakanaani, Wagirgashi na Wayebusi.”

< Genesis 15 >