< Exodus 12 >

1 And the LORD spoke unto Moses and Aaron in the land of Egypt, saying:
Bwana akamwambia Mose na Aroni katika nchi ya Misri,
2 'This month shall be unto you the beginning of months; it shall be the first month of the year to you.
“Mwezi huu utakuwa mwanzo wa miezi kwenu, yaani mwezi wa kwanza wa mwaka wenu.
3 Speak ye unto all the congregation of Israel, saying: In the tenth day of this month they shall take to them every man a lamb, according to their fathers' houses, a lamb for a household;
Iambie jumuiya yote ya Israeli kwamba katika siku ya kumi ya mwezi huu, kila mtu atatwaa mwana-kondoo mmoja kwa ajili ya familia yake, mmoja kwa kila nyumba.
4 and if the household be too little for a lamb, then shall he and his neighbour next unto his house take one according to the number of the souls; according to every man's eating ye shall make your count for the lamb.
Ikiwa nyumba yoyote ina watu wachache wasioweza kumaliza huyo mwana-kondoo mzima, nyumba hiyo itabidi ishirikiane na nyumba ya jirani wa karibu, baada ya kuzingatia idadi ya watu waliomo. Mtaangalia ni kiasi gani cha nyama kitahitajika kulingana na mahitaji ya kila mtu.
5 Your lamb shall be without blemish, a male of the first year; ye shall take it from the sheep, or from the goats;
Wanyama mtakaowachagua, lazima wawe wa kiume wa umri wa mwaka mmoja wasiokuwa na dosari, mwaweza kuwachukua kati ya kondoo au mbuzi.
6 and ye shall keep it unto the fourteenth day of the same month; and the whole assembly of the congregation of Israel shall kill it at dusk.
Tunzeni wanyama hao mpaka siku ya kumi na nne ya mwezi, ambapo lazima watu wa jumuiya yote ya Israeli wachinje wanyama hao wakati wa jioni.
7 And they shall take of the blood, and put it on the two side-posts and on the lintel, upon the houses wherein they shall eat it.
Ndipo watakapochukua baadhi ya hiyo damu na kuipaka kwenye vizingiti vya juu na miimo ya milango ya nyumba ambamo watakula wana-kondoo hao.
8 And they shall eat the flesh in that night, roast with fire, and unleavened bread; with bitter herbs they shall eat it.
Usiku huo huo watakula nyama iliyookwa kwenye moto, pamoja na mboga chungu za majani na mikate isiyotiwa chachu.
9 Eat not of it raw, nor sodden at all with water, but roast with fire; its head with its legs and with the inwards thereof.
Msile nyama mbichi wala iliyochemshwa, lakini iwe imeokwa kwenye moto, kichwa, miguu na nyama zake za ndani.
10 And ye shall let nothing of it remain until the morning; but that which remaineth of it until the morning ye shall burn with fire.
Msibakize nyama yoyote mpaka asubuhi; nazo kama zitabakia mpaka asubuhi, lazima mziteketeze kwa moto.
11 And thus shall ye eat it: with your loins girded, your shoes on your feet, and your staff in your hand; and ye shall eat it in haste — it is the LORD'S passover.
Hivi ndivyo mtakavyokula: Mtajifunga mikanda viunoni, mtakuwa mmevaa viatu vyenu miguuni na kushika fimbo zenu mkononi mwenu. Mle kwa haraka; hii ni Pasaka ya Bwana.
12 For I will go through the land of Egypt in that night, and will smite all the first-born in the land of Egypt, both man and beast; and against all the gods of Egypt I will execute judgments: I am the LORD.
“Usiku huo huo nitapita katika nchi yote ya Misri na kumuua kila mzaliwa wa kwanza, wa wanadamu na wa wanyama, nami nitaihukumu miungu yote ya Misri. Mimi ndimi Bwana.
13 And the blood shall be to you for a token upon the houses where ye are; and when I see the blood, I will pass over you, and there shall no plague be upon you to destroy you, when I smite the land of Egypt.
Damu itakuwa ishara kwa ajili yenu ya kuonyesha nyumba ambazo mtakuwamo; nami nitakapoiona damu, nitapita juu yenu. Hakuna pigo la uharibifu litakalowagusa ninyi nitakapoipiga Misri.
14 And this day shall be unto you for a memorial, and ye shall keep it a feast to the LORD; throughout your generations ye shall keep it a feast by an ordinance for ever.
“Siku hii itakuwa kumbukumbu kwenu, mtaiadhimisha kuwa sikukuu kwa Bwana, katika vizazi vyenu vyote: mtaishika kuwa amri ya kudumu.
15 Seven days shall ye eat unleavened bread; howbeit the first day ye shall put away leaven out of your houses; for whosoever eateth leavened bread from the first day until the seventh day, that soul shall be cut off from Israel.
Kwa siku saba mtakula mikate isiyotiwa chachu. Katika siku ya kwanza mtaondoa chachu yote ndani ya nyumba zenu, kwa maana yeyote atakayekula chochote chenye chachu kuanzia siku ya kwanza hadi ya saba lazima akatiliwe mbali kutoka Israeli.
16 And in the first day there shall be to you a holy convocation, and in the seventh day a holy convocation; no manner of work shall be done in them, save that which every man must eat, that only may be done by you.
Katika siku ya kwanza mtakuwa na kusanyiko takatifu, na kusanyiko jingine katika siku ya saba. Katika siku hizo msifanye kazi kamwe isipokuwa kutayarisha chakula cha kila mmoja; hilo ndilo tu mtakalofanya.
17 And ye shall observe the feast of unleavened bread; for in this selfsame day have I brought your hosts out of the land of Egypt; therefore shall ye observe this day throughout your generations by an ordinance for ever.
“Mtaadhimisha Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, kwa sababu hiyo ndiyo siku ile niliyovitoa vikosi vyenu kutoka Misri. Mtaiadhimisha siku hii kwa vizazi vyenu vyote kuwa amri ya kudumu.
18 In the first month, on the fourteenth day of the month at even, ye shall eat unleavened bread, until the one and twentieth day of the month at even.
Katika mwezi wa kwanza mtakula mikate isiyotiwa chachu, kuanzia jioni ya siku ya kumi na nne hadi jioni ya siku ya ishirini na moja.
19 Seven days shall there be no leaven found in your houses; for whosoever eateth that which is leavened, that soul shall be cut off from the congregation of Israel, whether he be a sojourner, or one that is born in the land.
Kwa muda wa siku saba isionekane chachu yoyote katika nyumba zenu. Yeyote alaye chochote chenye chachu ndani yake, lazima akatiliwe mbali kutoka jumuiya ya Israeli, akiwa ni mgeni au mzawa.
20 Ye shall eat nothing leavened; in all your habitations shall ye eat unleavened bread.'
Msile chochote kilichotiwa chachu. Popote muishipo, ni lazima mle mikate isiyotiwa chachu.”
21 Then Moses called for all the elders of Israel, and said unto them: 'Draw out, and take you lambs according to your families, and kill the passover lamb.
Ndipo Mose akawaita wazee wote wa Israeli na kuwaambia, “Nendeni mara moja mkachague wanyama kwa ajili ya jamaa zenu, mkachinje mwana-kondoo wa Pasaka.
22 And ye shall take a bunch of hyssop, and dip it in the blood that is in the basin, and strike the lintel and the two side-posts with the blood that is in the basin; and none of you shall go out of the door of his house until the morning.
Chukueni kitawi cha hisopo, kichovyeni kwenye damu iliyopo kwenye sinia na kuipaka baadhi ya hiyo damu kwenye vizingiti na kwenye miimo yote miwili ya milango. Mtu yeyote asitoke nje ya mlango wa nyumba yake mpaka asubuhi.
23 For the LORD will pass through to smite the Egyptians; and when He seeth the blood upon the lintel, and on the two side-posts, the LORD will pass over the door, and will not suffer the destroyer to come in unto your houses to smite you.
Bwana apitapo katika nchi yote kuwapiga Wamisri, ataiona damu juu ya vizingiti na kwenye miimo ya milango, naye atapita juu, wala hatamruhusu mwangamizi kuingia katika nyumba zenu na kuwapiga ninyi.
24 And ye shall observe this thing for an ordinance to thee and to thy sons for ever.
“Shikeni maagizo haya yawe kanuni ya kudumu kwenu na kwa ajili ya wazao wenu.
25 And it shall come to pass, when ye be come to the land which the LORD will give you, according as He hath promised, that ye shall keep this service.
Mtakapoingia katika nchi Bwana atakayowapa kama alivyoahidi, shikeni desturi hii.
26 And it shall come to pass, when your children shall say unto you: What mean ye by this service?
Watoto wenu watakapowauliza, ‘Sikukuu hii ina maana gani kwenu?’
27 that ye shall say: It is the sacrifice of the LORD'S passover, for that He passed over the houses of the children of Israel in Egypt, when He smote the Egyptians, and delivered our houses.' And the people bowed the head and worshipped.
Basi waambieni, ‘Hii ni dhabihu ya Pasaka kwa Bwana, ambaye alipita juu ya nyumba za Waisraeli katika nchi ya Misri na hakudhuru nyumba zetu alipowapiga Wamisri.’” Ndipo watu wa Israeli waliposujudu na kuabudu.
28 And the children of Israel went and did so; as the LORD had commanded Moses and Aaron, so did they.
Waisraeli wakafanya kama vile Bwana alivyomwagiza Mose na Aroni.
29 And it came to pass at midnight, that the LORD smote all the firstborn in the land of Egypt, from the first-born of Pharaoh that sat on his throne unto the first-born of the captive that was in the dungeon; and all the first-born of cattle.
Ilipofika usiku wa manane, Bwana akawapiga wazaliwa wa kwanza wote katika Misri, kuanzia mzaliwa wa kwanza wa Farao, mrithi wa kiti cha ufalme, hadi mzaliwa wa kwanza wa mfungwa, aliyekuwa gerezani, na wazaliwa wa kwanza wa mifugo yote pia.
30 And Pharaoh rose up in the night, he, and all his servants, and all the Egyptians; and there was a great cry in Egypt; for there was not a house where there was not one dead.
Farao, na maafisa wake wote, na Wamisri wote wakaamka usiku, na kulikuwa na kilio kikubwa katika nchi ya Misri, kwa kuwa haikuwepo nyumba ambayo hakufa mtu.
31 And he called for Moses and Aaron by night and said: 'Rise up, get you forth from among my people, both ye and the children of Israel; and go, serve the LORD, as ye have said.
Wakati huo Farao akawaita Mose na Aroni na kuwaambia, “Ondokeni! Tokeni kwa watu wangu, ninyi pamoja na Waisraeli! Nendeni mkamwabudu Bwana kama mlivyoomba.
32 Take both your flocks and your herds, as ye have said, and be gone; and bless me also.'
Chukueni makundi yenu ya kondoo na mbuzi pamoja na ngʼombe, kama mlivyosema, nanyi mwende zenu. Nanyi pia mnibariki.”
33 And the Egyptians were urgent upon the people, to send them out of the land in haste; for they said: 'We are all dead men.'
Wamisri wakawahimiza Waisraeli waondoke kwa haraka na kuacha nchi yao. Kwa kuwa walisema, “La sivyo, tutakufa wote!”
34 And the people took their dough before it was leavened, their kneading-troughs being bound up in their clothes upon their shoulders.
Hivyo watu wakachukua donge lao la unga kabla ya kutiwa chachu, wakaweka ndani ya mabakuli ya kukandia, wakayaviringisha katika vitambaa na kuyabeba mabegani mwao.
35 And the children of Israel did according to the word of Moses; and they asked of the Egyptians jewels of silver, and jewels of gold, and raiment.
Waisraeli wakafanya kama Mose alivyowaelekeza, nao wakawaomba Wamisri wawapatie vitu vya fedha, dhahabu na nguo.
36 And the LORD gave the people favour in the sight of the Egyptians, so that they let them have what they asked. And they despoiled the Egyptians.
Basi Bwana alikuwa amewafanya Wamisri kuwa wakarimu kwa hawa watu, wakawapatia Waisraeli vile walivyotaka kwao; kwa hiyo wakawateka nyara Wamisri.
37 And the children of Israel journeyed from Rameses to Succoth, about six hundred thousand men on foot, beside children.
Waisraeli wakasafiri kutoka Ramesesi mpaka Sukothi. Walikuwepo wanaume wapatao 600,000 waendao kwa miguu bila kuhesabu wanawake na watoto.
38 And a mixed multitude went up also with them; and flocks, and herds, even very much cattle.
Watu wengine wengi wakafuatana nao, pamoja na makundi makubwa ya mifugo wakiwemo kondoo, mbuzi na ngʼombe.
39 And they baked unleavened cakes of the dough which they brought forth out of Egypt, for it was not leavened; because they were thrust out of Egypt, and could not tarry, neither had they prepared for themselves any victual.
Wakatengeneza maandazi yasiyotiwa chachu kwa ule unga uliokandwa waliokuwa wameutoa Misri, donge hilo la unga halikuwa limetiwa chachu, kwa kuwa walikuwa wameondolewa Misri kwa haraka nao hawakuwa na muda wa kuandaa chakula chao.
40 Now the time that the children of Israel dwelt in Egypt was four hundred and thirty years.
Waisraeli walikuwa wameishi Misri kwa muda wa miaka 430.
41 And it came to pass at the end of four hundred and thirty years, even the selfsame day it came to pass, that all the host of the LORD went out from the land of Egypt.
Ilikuwa ni siku ya mwisho ya hiyo miaka 430, vikosi vyote vya Bwana vilipokuwa vimeondoka Misri.
42 It was a night of watching unto the LORD for bringing them out from the land of Egypt; this same night is a night of watching unto the LORD for all the children of Israel throughout their generations.
Kwa sababu Bwana aliutenga usiku ule ili kuwatoa Waisraeli katika nchi ya Misri, katika usiku huu Waisraeli wote wanapaswa kuadhimisha kwa kukesha ili kumheshimu Bwana katika vizazi vijavyo.
43 And the LORD said unto Moses and Aaron: 'This is the ordinance of the passover: there shall no alien eat thereof;
Bwana akamwambia Mose na Aroni, “Haya ndiyo masharti kwa ajili ya Pasaka: “Mgeni hataruhusiwa kula Pasaka.
44 but every man's servant that is bought for money, when thou hast circumcised him, then shall he eat thereof.
Mtumwa yeyote ambaye mmemnunua aweza kuila kama mmemtahiri,
45 A sojourner and a hired servant shall not eat thereof.
lakini kibarua yeyote au msafiri haruhusiwi kula.
46 In one house shall it be eaten; thou shalt not carry forth aught of the flesh abroad out of the house; neither shall ye break a bone thereof.
“Sharti iliwe ndani ya nyumba; msichukue nyama yoyote nje ya nyumba hiyo. Msiuvunje mfupa wowote.
47 All the congregation of Israel shall keep it.
Jumuiya yote ya Israeli ni lazima waiadhimishe Pasaka hiyo.
48 And when a stranger shall sojourn with thee, and will keep the passover to the LORD, let all his males be circumcised, and then let him come near and keep it; and he shall be as one that is born in the land; but no uncircumcised person shall eat thereof.
“Mgeni aishiye miongoni mwenu ambaye anataka kuadhimisha Pasaka ya Bwana ni lazima wanaume wote waliomo nyumbani mwake wawe wametahiriwa, ndipo aweze kushiriki kama mzawa. Mwanaume yeyote asiyetahiriwa haruhusiwi kuila.
49 One law shall be to him that is homeborn, and unto the stranger that sojourneth among you.'
Sheria iyo hiyo itamuhusu mzawa na mgeni anayeishi miongoni mwenu.”
50 Thus did all the children of Israel; as the LORD commanded Moses and Aaron, so did they.
Waisraeli wote walifanya kama vile Bwana alivyomwagiza Mose na Aroni.
51 And it came to pass the selfsame day that the LORD did bring the children of Israel out of the land of Egypt by their hosts.
Siku ile ile Bwana akawatoa Waisraeli katika nchi ya Misri kwa vikosi vyao.

< Exodus 12 >