< Exodus 10 >

1 And the LORD said unto Moses: 'Go in unto Pharaoh; for I have hardened his heart, and the heart of his servants, that I might show these My signs in the midst of them;
Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Nenda kwa Farao, kwa kuwa nimeufanya moyo wake kuwa mgumu na mioyo ya maafisa wake ili kwamba nipate kutenda ishara hizi zangu za ajabu miongoni mwao
2 and that thou mayest tell in the ears of thy son, and of thy son's son, what I have wrought upon Egypt, and My signs which I have done among them; that ye may know that I am the LORD.'
ili upate kuwaeleza watoto wako na wajukuu wako jinsi nilivyowatendea Wamisri kwa ukali na jinsi nilivyofanya ishara zangu miongoni mwao, nanyi mpate kujua kuwa Mimi ndimi Bwana.”
3 And Moses and Aaron went in unto Pharaoh, and said unto him: 'Thus saith the LORD, the God of the Hebrews: How long wilt thou refuse to humble thyself before Me? let My people go, that they may serve Me.
Kwa hiyo Mose na Aroni wakaenda kwa Farao na kumwambia, “Hili ndilo Bwana, Mungu wa Waebrania, asemalo: ‘Utaendelea hata lini kukataa kunyenyekea mbele yangu? Waachie watu wangu waende, ili wapate kuniabudu.
4 Else, if thou refuse to let My people go, behold, to-morrow will I bring locusts into thy border;
Kama ukikataa kuwaachia waende, kesho nitaleta nzige katika nchi yako.
5 and they shall cover the face of the earth, that one shall not be able to see the earth; and they shall eat the residue of that which is escaped, which remaineth unto you from the hail, and shall eat every tree which groweth for you out of the field;
Nao watafunika uso wa ardhi hata usionekane. Watatafuna mabaki machache yaliyobakizwa baada ya ile mvua ya mawe, yaani pamoja na kila mti unaoota katika mashamba yenu.
6 and thy houses shall be filled, and the houses of all thy servants, and the houses of all the Egyptians; as neither thy fathers nor thy fathers' fathers have seen, since the day that they were upon the earth unto this day.' And he turned, and went out from Pharaoh.
Nzige hao watajaza nyumba zako, za maafisa wako wote na za Wamisri wote. Jambo ambalo baba zenu wala babu zenu hawajapata kuona tangu siku ile walipoanza kuishi katika nchi hii mpaka leo hii.’” Ndipo Mose akageuka na kumwacha Farao.
7 And Pharaoh's servants said unto him: 'How long shall this man be a snare unto us? let the men go, that they may serve the LORD their God, knowest thou not yet that Egypt is destroyed?'
Maafisa wa Farao wakamwambia, “Mpaka lini huyu mtu atakuwa tanzi kwetu? Waachie hao watu waende zao, ili wapate kumwabudu Bwana Mungu wao. Je, bado hutambui kuwa Misri imeangamia?”
8 And Moses and Aaron were brought again unto Pharaoh; and he said unto them: 'Go, serve the LORD your God; but who are they that shall go?'
Ndipo Mose na Aroni wakaletwa kwa Farao. Farao akawaambia, “Nendeni, mkamwabudu Bwana Mungu wenu. Lakini ni nani hasa watakaokwenda?”
9 And Moses said: 'We will go with our young and with our old, with our sons and with our daughters, with our flocks and with our herds we will go; for we must hold a feast unto the LORD.'
Mose akajibu, “Tutakwenda na vijana wetu na wazee, pamoja na wana wetu na binti zetu, pia pamoja na kondoo zetu, ngʼombe, mbuzi, farasi na punda kwa sababu tutaadhimisha sikukuu kwa Bwana.”
10 And he said unto them: 'So be the LORD with you, as I will let you go, and your little ones; see ye that evil is before your face.
Farao akasema, “Bwana awe pamoja nanyi, kama nikiwaruhusu mwondoke pamoja na wanawake wenu na watoto wenu! Ni wazi kwamba mna makusudi mabaya.
11 Not so; go now ye that are men, and serve the LORD; for that is what ye desire.' And they were driven out from Pharaoh's presence.
La hasha! Wanaume peke yao na waende, wakamwabudu Bwana, kwa kuwa hilo ndilo mmekuwa mkiomba.” Kwa hiyo Mose na Aroni wakaondolewa mbele ya Farao.
12 And the LORD said unto Moses: 'Stretch out thy hand over the land of Egypt for the locusts, that they may come up upon the land of Egypt, and eat every herb of the land, even all that the hail hath left.'
Basi Bwana akamwambia Mose, “Nyoosha mkono wako juu ya Misri ili kundi la nzige liweze kuingia juu ya nchi na kutafuna kila kitu kiotacho katika mashamba na kila kitu kilichosazwa na ile mvua ya mawe.”
13 And Moses stretched forth his rod over the land of Egypt, and the LORD brought an east wind upon the land all that day, and all the night; and when it was morning, the east wind brought the locusts.
Kwa hiyo Mose akanyoosha fimbo yake juu ya Misri, Bwana akauleta upepo wa mashariki ukavuma katika nchi yote mchana wote na usiku kucha, kufikia asubuhi upepo ukawa umeleta nzige.
14 And the locusts went up over all the land of Egypt, and rested in all the borders of Egypt; very grievous were they; before them there were no such locusts as they, neither after them shall be such.
Wakaivamia Misri yote na kukaa kila eneo la nchi kwa wingi. Kamwe hapajapata kuwepo pigo la nzige kama hilo, wala halitakuwepo tena.
15 For they covered the face of the whole earth, so that the land was darkened; and they did eat every herb of the land, and all the fruit of the trees which the hail had left; and there remained not any green thing, either tree or herb of the field, through all the land of Egypt.
Wakafunika ardhi yote mpaka ardhi ikawa nyeusi. Wakatafuna kile chote kilichokuwa kimebakizwa na ile mvua ya mawe, kila kitu kiotacho mashambani pamoja na matunda kwenye miti. Hakuna kitu chochote cha kijani kilichosalia katika miti au mmea katika nchi yote ya Misri.
16 Then Pharaoh called for Moses and Aaron in haste; and he said: 'I have sinned against the LORD your God, and against you.
Farao akawaita Mose na Aroni kwa haraka na kuwaambia, “Nimetenda dhambi dhidi ya Bwana Mungu wenu na dhidi yenu pia.
17 Now therefore forgive, I pray thee, my sin only this once, and entreat the LORD your God, that He may take away from me this death only.'
Sasa unisamehe dhambi yangu mara moja tena na umwombe Bwana Mungu wako aondoe pigo hili baya kwangu.”
18 And he went out from Pharaoh, and entreated the LORD.
Kisha Mose akaondoka kwa Farao akamwomba Bwana.
19 And the LORD turned an exceeding strong west wind, which took up the locusts, and drove them into the Red Sea; there remained not one locust in all the border of Egypt.
Naye Bwana akaugeuza upepo ukavuma kutoka magharibi, wenye nguvu nyingi, ambao uliwaondoa wale nzige na kuwapeleka kwenye Bahari ya Shamu. Hakuna nzige hata mmoja aliyebaki popote katika nchi ya Misri.
20 But the LORD hardened Pharaoh's heart, and he did not let the children of Israel go.
Lakini Bwana akaufanya moyo wa Farao kuwa mgumu, wala hakuwaachia Waisraeli waondoke.
21 And the LORD said unto Moses: 'Stretch out thy hand toward heaven, that there may be darkness over the land of Egypt, even darkness which may be felt.'
Kisha Bwana akamwambia Mose, “Nyoosha mkono wako kuelekea angani ili giza litande katika nchi ya Misri, giza ambalo watu wanaweza kulipapasa na kulihisi.”
22 And Moses stretched forth his hand toward heaven; and there was a thick darkness in all the land of Egypt three days;
Kwa hiyo Mose akaunyoosha mkono wake kuelekea angani, na giza nene likafunika pote katika nchi ya Misri kwa muda wa siku tatu.
23 they saw not one another, neither rose any from his place for three days; but all the children of Israel had light in their dwellings.
Hakuna mtu yeyote aliyeweza kumwona mwenzake, wala kuondoka mahali alipokuwa kwa muda wa siku tatu. Lakini Waisraeli wote walikuwa na mwanga katika maeneo yao waliyokuwa wanaishi.
24 And Pharaoh called unto Moses, and said: 'Go ye, serve the LORD; only let your flocks and your herds be stayed; let your little ones also go with you.'
Ndipo Farao akamwita Mose na kusema, “Nendeni, mkamwabudu Bwana. Hata wanawake na watoto wenu mwaweza kwenda nao pia, lakini kondoo, mbuzi na ngʼombe wenu waacheni.”
25 And Moses said: 'Thou must also give into our hand sacrifices and burnt-offerings, that we may sacrifice unto the LORD our God.
Lakini Mose akasema, “Huna budi kuturuhusu tuwe na dhabihu na sadaka za kuteketezwa za kutoa mbele za Bwana Mungu wetu.
26 Our cattle also shall go with us; there shall not a hoof be left behind; for thereof must we take to serve the LORD our God; and we know not with what we must serve the LORD, until we come thither.'
Sisi ni lazima tuondoke na mifugo yetu pia, wala hakuna ukwato utakaoachwa nyuma. Inatupasa kutumia baadhi ya hiyo mifugo katika kumwabudu Bwana Mungu wetu, kwa kuwa mpaka tutakapofika huko hatutakuwa tumefahamu ni nini tutakachotumia katika kumwabudu Bwana.”
27 But the LORD hardened Pharaoh's heart, and he would not let them go.
Lakini Bwana akaufanya moyo wa Farao kuwa mgumu, hakuwa radhi kuwaachia waondoke.
28 And Pharaoh said unto him: 'Get thee from me, take heed to thyself, see my face no more; for in the day thou seest my face thou shalt die.'
Farao akamwambia Mose, “Ondoka mbele yangu! Hakikisha kuwa hutakuja mbele yangu tena! Siku ile utakapouona uso wangu utakufa.”
29 And Moses said: 'Thou hast spoken well; I will see thy face again no more.'
Mose akamjibu, “Iwe kama ulivyosema! Kamwe sitauona uso wako tena.”

< Exodus 10 >