< 1 Samuel 15 >

1 And Samuel said unto Saul: 'The LORD sent me to anoint thee to be king over His people, over Israel; now therefore hearken thou unto the voice of the words of the LORD.
Samweli akamwambia Sauli, “Mimi ndiye ambaye Bwana alinituma nikutie mafuta uwe mfalme juu ya watu wake Israeli, basi sasa sikiliza ujumbe kutoka kwa Bwana.
2 Thus saith the LORD of hosts: I remember that which Amalek did to Israel, how he set himself against him in the way, when he came up out of Egypt.
Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: ‘Nitawaadhibu Waamaleki kwa kile walichowatendea Israeli walipowavizia wakati walipanda kutoka Misri.
3 Now go and smite Amalek, and utterly destroy all that they have, and spare them not; but slay both man and woman, infant and suckling, ox and sheep, camel and ass.'
Basi sasa nenda ukawashambulie Waamaleki na kuwaangamiza kabisa pamoja na kila kitu kilicho mali yao. Usiwahurumie; waue wanaume na wanawake, watoto na wanyonyao, ngʼombe na kondoo, ngamia na punda.’”
4 And Saul summoned the people, and numbered them in Telaim, two hundred thousand footmen, and ten thousand men of Judah.
Ndipo Sauli akawaita watu na kuwapanga huko Telaimu, askari wa miguu 200,000 pamoja na watu 10,000 kutoka Yuda.
5 And Saul came to the city of Amalek, and lay in wait in the valley.
Sauli akaenda katika mji wa Amaleki na kuwavizia bondeni.
6 And Saul said unto the Kenites: 'Go, depart, get you down from among the Amalekites, lest I destroy you with them; for ye showed kindness to all the children of Israel, when they came up out of Egypt.' So the Kenites departed from among the Amalekites.
Kisha akawaambia Wakeni, “Ondokeni, waacheni Waamaleki ili nisije nikawaangamiza ninyi pamoja nao, kwa kuwa ninyi mliwatendea mema Waisraeli wote wakati walipanda kutoka Misri.” Basi Wakeni wakaondoka, wakawaacha Waamaleki.
7 And Saul smote the Amalekites, from Havilah as thou goest to Shur, that is in front of Egypt.
Ndipo Sauli akawashambulia Waamaleki toka Havila mpaka Shuri, hadi mashariki ya Misri.
8 And he took Agag the king of the Amalekites alive, and utterly destroyed all the people with the edge of the sword.
Akamchukua Agagi, mfalme wa Waamaleki akiwa hai, nao watu wake wote akawaangamiza kabisa kwa upanga.
9 But Saul and the people spared Agag, and the best of the sheep, and of the oxen, even the young of the second birth, and the lambs, and all that was good, and would not utterly destroy them; but every thing that was of no account and feeble, that they destroyed utterly.
Lakini Sauli na hilo jeshi wakamhifadhi hai Agagi na kondoo na ngʼombe walio wazuri, mafahali na wana-kondoo walionona kila kitu kilichokuwa kizuri. Hivi vitu hawakuwa radhi kuviangamiza kabisa, bali kila kitu kilichodharauliwa na kilicho dhaifu wakakiangamiza kabisa.
10 Then came the word of the LORD unto Samuel, saying:
Kisha neno la Bwana likamjia Samweli kusema:
11 'It repenteth Me that I have set up Saul to be king; for he is turned back from following Me, and hath not performed My commandments.' And it grieved Samuel; and he cried unto the LORD all night.
“Ninasikitika kwamba nimemfanya Sauli kuwa mfalme, kwa sababu ameacha kunifuata mimi na hakutimiza maagizo yangu.” Samweli akafadhaika, naye akamlilia Bwana usiku ule wote.
12 And Samuel rose early to meet Saul in the morning; and it was told Samuel, saying: 'Saul came to Carmel, and, behold, he is setting him up a monument, and is gone about, and passed on, and gone down to Gilgal.'
Asubuhi na mapema Samweli akaamka kwenda kukutana na Sauli, lakini akaambiwa, “Sauli amekwenda Karmeli. Huko amesimamisha mnara kwa heshima yake mwenyewe naye ameendelea na kuteremkia Gilgali.”
13 And Samuel came to Saul; and Saul said unto him: 'Blessed be thou of the LORD; I have performed the commandment of the LORD.'
Samweli alipomfikia, Sauli akamwambia, “Bwana akubariki! Nimetimiza yale Bwana aliniagiza.”
14 And Samuel said: 'What meaneth then this bleating of the sheep in mine ears, and the lowing of the oxen which I hear?'
Lakini Samweli akasema, “Nini basi huu mlio wa kondoo masikioni mwangu? Huu mlio wa ngʼombe ninaousikia ni kitu gani?”
15 And Saul said: 'They have brought them from the Amalekites; for the people spared the best of the sheep and of the oxen, to sacrifice unto the LORD thy God; and the rest we have utterly destroyed.'
Sauli akajibu, “Askari wamewaleta kutoka kwa Waamaleki, waliwaacha wale kondoo na ngʼombe wazuri ili kuwatoa dhabihu kwa Bwana, Mungu wako, lakini tuliwaangamiza kabisa wengine wote.”
16 Then Samuel said unto Saul: 'Stay, and I will tell thee what the LORD hath said to me this night.' And he said unto him: 'Say on.'
Samweli akamwambia Sauli, “Ngoja! Nami nitakuambia lile Bwana aliloniambia usiku huu.” Sauli akajibu, “Niambie.”
17 And Samuel said: 'Though thou be little in thine own sight, art thou not head of the tribes of Israel? And the LORD anointed thee king over Israel;
Samweli akamwambia, “Ingawa zamani ulijiona mdogo machoni pako mwenyewe, Je, hukuwa kiongozi wa kabila za Israeli? Bwana alikutia mafuta kuwa mfalme juu ya Israeli.
18 and the LORD sent thee on a journey, and said: Go and utterly destroy the sinners the Amalekites, and fight against them until they be consumed.
Naye akakutuma kwa kazi maalum, akisema, ‘Nenda ukaangamize kabisa wale watu waovu, wale Waamaleki, upigane nao vita mpaka utakapowaangamiza kabisa.’
19 Wherefore then didst thou not hearken to the voice of the LORD, but didst fly upon the spoil, and didst that which was evil in the sight of the LORD?'
Kwa nini hukumtii Bwana? Kwa nini ulivamia nyara na kufanya uovu machoni pa Bwana?”
20 And Saul said unto Samuel: 'Yea, I have hearkened to the voice of the LORD, and have gone the way which the LORD sent me, and have brought Agag the king of Amalek, and have utterly destroyed the Amalekites.
Sauli akasema, “Lakini nilimtii Bwana. Nilikamilisha ile kazi ambayo Bwana alinituma. Niliwaangamiza Waamaleki kabisa na kumleta Agagi mfalme wao.
21 But the people took of the spoil, sheep and oxen, the chief of the devoted things, to sacrifice unto the LORD thy God in Gilgal.'
Askari walichukua kondoo na ngʼombe kutoka kwenye nyara, zile ambazo ni nzuri sana zimewekwa wakfu kwa Mungu, ili zitolewe dhabihu kwa Bwana Mungu wako huko Gilgali.”
22 And Samuel said: 'Hath the LORD as great delight in burnt-offerings and sacrifices, as in hearkening to the voice of the LORD? Behold, to obey is better than sacrifice, and to hearken than the fat of rams.
Lakini Samweli akajibu: “Je, Bwana anafurahia sadaka za kuteketezwa na dhabihu kama vile kuitii sauti ya Bwana? Kutii ni bora zaidi kuliko dhabihu, nako kusikia ni bora kuliko mafuta ya kondoo dume.
23 For rebellion is as the sin of witchcraft, and stubbornness is as idolatry and teraphim. Because thou hast rejected the word of the LORD, He hath also rejected thee from being king.'
Kwa maana kuasi ni kama dhambi ya uaguzi, nao ukaidi ni kama uovu wa kuabudu sanamu. Kwa sababu umelikataa neno la Bwana, naye amekukataa wewe kuendelea kuwa mfalme.”
24 And Saul said unto Samuel: 'I have sinned; for I have transgressed the commandment of the LORD, and thy words; because I feared the people, and hearkened to their voice.
Ndipo Sauli akamwambia Samweli, “Nimetenda dhambi. Nimevunja amri ya Bwana na maagizo yako. Niliwaogopa watu na kwa hiyo nikafanya walivyotaka.
25 Now therefore, I pray thee, pardon my sin, and return with me, that I may worship the LORD.'
Sasa ninakusihi usamehe dhambi yangu, nawe urudi pamoja nami, ili nipate kumwabudu Bwana.”
26 And Samuel said unto Saul: 'I will not return with thee; for thou hast rejected the word of the LORD, and the LORD hath rejected thee from being king over Israel.'
Lakini Samweli akamwambia, “Sitarudi pamoja nawe. Umelikataa neno la Bwana, naye Bwana amekukataa wewe, usiendelee kuwa mfalme juu ya Israeli!”
27 And as Samuel turned about to go away, he laid hold upon the skirt of his robe, and it rent.
Samweli alipogeuka ili aondoke, Sauli akangʼangʼania pindo la joho lake, nalo likararuka.
28 And Samuel said unto him: 'The LORD hath rent the kingdom of Israel from thee this day, and hath given it to a neighbour of thine, that is better than thou.
Samweli akamwambia, “Bwana ameurarua ufalme wa Israeli kutoka kwako leo, naye ameutia kwa mmoja wa majirani zako, aliye bora kuliko wewe.
29 And also the Glory of Israel will not lie nor repent; for He is not a man, that He should repent.'
Yeye aliye Utukufu wa Israeli hasemi uongo wala hana kigeugeu; kwa kuwa yeye si mwanadamu, hata abadili nia yake.”
30 Then he said: 'I have sinned; yet honour me now, I pray thee, before the elders of my people, and before Israel, and return with me, that I may worship the LORD thy God.'
Sauli akajibu, “Nimetenda dhambi. Lakini tafadhali niheshimu mbele ya wazee wa watu wangu na mbele ya Israeli; rudi pamoja nami, ili nipate kumwabudu Bwana Mungu wako.”
31 So Samuel returned after Saul; and Saul worshipped the LORD.
Hivyo Samweli akarudi pamoja na Sauli, naye Sauli akamwabudu Bwana.
32 Then said Samuel: 'Bring ye hither to me Agag the king of the Amalekites.' And Agag came unto him in chains. And Agag said: 'Surely the bitterness of death is at hand.'
Ndipo Samweli akasema, “Niletee Agagi mfalme wa Waamaleki.” Agagi akaja kwake kwa ujasiri, akifikiri, “Hakika uchungu wa mauti umepita.”
33 And Samuel said: As thy sword hath made women childless, so shall thy mother be childless among women. And Samuel hewed Agag in pieces before the LORD in Gilgal.
Lakini Samweli akasema, “Kama upanga wako ulivyofanya wanawake kufiwa na watoto wao, ndivyo mama yako atakavyokuwa hana mtoto miongoni mwa wanawake.” Naye Samweli akamuua Agagi mbele za Bwana huko Gilgali.
34 Then Samuel went to Ramah; and Saul went up to his house to Gibeath-shaul.
Kisha Samweli akaenda Rama, lakini Sauli akapanda nyumbani kwake huko Gibea ya Sauli.
35 And Samuel never beheld Saul again until the day of his death; for Samuel mourned for Saul; and the LORD repented that He had made Saul king over Israel.
Hadi siku Samweli alipofariki hakwenda kumwona Sauli tena, ingawa Samweli alimwombolezea. Naye Bwana alihuzunika kwamba alimfanya Sauli kuwa mfalme juu ya Israeli.

< 1 Samuel 15 >