< 1 Samuel 14 >

1 Now it fell upon a day, that Jonathan the son of Saul said unto the young man that bore his armour: 'Come and let us go over to the Philistines' garrison, that is on yonder side. But he told not his father.
Siku moja Yonathani mwana wa Sauli akamwambia kijana mbeba silaha wake, akasema, “Njoo, tuwavukie Wafilisti kwenye doria upande ule mwingine.” Lakini hakumwambia baba yake.
2 And Saul tarried in the uttermost part of Gibeah under the pomegranate-tree which is in Migron; and the people that were with him were about six hundred men,
Sauli alikuwa akikaa kwenye viunga vya Gibea chini ya mkomamanga huko Migroni. Alikuwa pamoja na watu kama 600,
3 and Ahijah, the son of Ahitub, Ichabod's brother, the son of Phinehas, the son of Eli, the priest of the LORD in Shiloh, wearing an ephod. And the people knew not that Jonathan was gone.
miongoni mwao alikuwepo Ahiya, ambaye alikuwa amevaa kisibau. Alikuwa mwana wa Ikabodi, nduguye Ahitubu mwana wa Finehasi, mwana wa Eli, kuhani wa Bwana huko Shilo. Hakuna yeyote aliyekuwa na habari kwamba Yonathani alikuwa ameondoka.
4 And between the passes, by which Jonathan sought to go over unto the Philistines' garrison, there was a rocky crag on the one side, and a rocky crag on the other side; and the name of the one was Bozez, and the name of the other Seneh.
Kila upande wa njia ambayo Yonathani alikusudia kupita ili kuvuka kufikia doria ya Wafilisti kulikuwepo na jabali; moja lilikuwa linaitwa Bosesi, na jingine Sene.
5 The one crag rose up on the north in front of Michmas, and the other on the south in front of Geba.
Jabali moja lilisimama kaskazini kuelekea Mikmashi na jingine upande wa kusini kuelekea Geba.
6 And Jonathan said to the young man that bore his armour: 'Come and let us go over unto the garrison of these uncircumcised; it may be that the LORD will work for us; for there is no restraint to the LORD to save by many or by few.'
Yonathani akamwambia kijana wake mbeba silaha, “Njoo, tuvukie doria ya wale jamaa wasiotahiriwa. Huenda Bwana atatenda kwa ajili yetu. Hakuna chochote kitakachoweza kumzuia Bwana kuokoa, kwamba ni kwa wingi au kwa uchache.”
7 And his armour-bearer said unto him: 'Do all that is in thy heart; turn thee, behold I am with thee according to thy heart.'
Mbeba silaha wake akamwambia, “Fanya yale yote uliyo nayo katika moyo wako. Songa mbele; moyo wangu na roho yangu viko pamoja nawe.”
8 Then said Jonathan: 'Behold, we will pass over unto the men, and we will disclose ourselves unto them.
Yonathani akasema, “Basi njoo; tutavuka kuwaelekea hao watu na kuacha watuone.
9 If they say thus unto us: Tarry until we come to you; then we will stand still in our place, and will not go up unto them.
Kama wakituambia, ‘Subirini hapo mpaka tuje kwenu,’ tutakaa pale tulipo na hatutakwea kwao.
10 But if they say thus: Come up unto us; then we will go up; for the LORD hath delivered them into our hand; and this shall be the sign unto us.'
Lakini kama watasema, ‘Pandeni mje kwetu,’ tutakwea, kwa sababu hiyo itakuwa ishara yetu kwamba Bwana amewatia mikononi mwetu.”
11 And both of them disclosed themselves unto the garrison of the Philistines; and the Philistines said: 'Behold Hebrews coming forth out of the holes where they hid themselves.'
Basi wote wawili wakajionyesha kwa doria ya Wafilisti. Wafilisti wakasema, “Tazama! Waebrania wanatambaa toka mashimoni walimokuwa wamejificha.”
12 And the men of the garrison spoke to Jonathan and his armour-bearer, and said: 'Come up to us, and we will show you a thing.' And Jonathan said unto his armour-bearer: 'Come up after me; for the LORD hath delivered them into the hand of Israel.'
Watu wa kwenye doria wakawapigia kelele Yonathani na mbeba silaha wake, wakisema, “Njooni, pandeni kwetu nasi tutawakomesha.” Basi Yonathani akamwambia mbeba silaha wake, “Panda nyuma yangu; Bwana amewatia mikononi mwa Israeli.”
13 And Jonathan climbed up upon his hands and upon his feet, and his armour-bearer after him; and they fell before Jonathan; and his armour-bearer slew them after him.
Yonathani akapanda juu, akitumia mikono yake na miguu, pamoja na mbeba silaha wake papo hapo nyuma yake. Wafilisti wakaanguka mbele ya Yonathani, naye mbeba silaha wake akamfuata akiwaua nyuma yake.
14 And that first slaughter, which Jonathan and his armour-bearer made, was about twenty men, within as it were half a furrow's length in an acre of land.
Katika hilo shambulio la kwanza, Yonathani na mbeba silaha wake waliua kama watu ishirini kwenye eneo kama la nusu eka.
15 And there was a trembling in the camp in the field, and among all the people; the garrison, and the spoilers, they also trembled; and the earth quaked; so it grew into a terror from God.
Kisha fadhaa ikawapata jeshi lote, wale waliokuwa kambini na shambani, wale waliokuwa katika doria na makundi ya washambuliaji, nayo nchi ilitetemeka. Ilikuwa ni hofu ya ghafula iliyotumwa na Mungu.
16 And the watchmen of Saul in Gibeath-benjamin looked; and, behold, the multitude melted away, and they went hither and thither.
Wapelelezi wa Sauli huko Gibea ya Benyamini wakaona jeshi likitokomea pande zote.
17 Then said Saul unto the people that were with him: 'Number now, and see who is gone from us.' And when they had numbered, behold, Jonathan and his armour-bearer were not there.
Ndipo Sauli akawaambia watu wale waliokuwa pamoja naye, “Kagueni jeshi mkaone ni nani ameondoka katikati yetu.” Walipokagua, akawa ni Yonathani na mbeba silaha wake ambao hawakuwepo.
18 And Saul said unto Ahijah: 'Bring hither the ark of God.' For the ark of God was there at that time with the children of Israel.
Sauli akamwambia Ahiya, “Leta Sanduku la Mungu.” (Wakati huo lilikuwa kwa Waisraeli.)
19 And it came to pass, while Saul talked unto the priest, that the tumult that was in the camp of the Philistines went on and increased; and Saul said unto the priest: 'Withdraw thy hand.'
Wakati Sauli alipokuwa akisema na kuhani, makelele katika kambi ya Wafilisti yakaongezeka zaidi na zaidi. Hivyo Sauli akamwambia kuhani, “Rudisha mkono wako.”
20 And Saul and all the people that were with him were gathered together, and came to the battle; and, behold, every man's sword was against his fellow, and there was a very great discomfiture.
Kisha Sauli na watu wake wote wakakusanyika na kwenda vitani. Wakawakuta Wafilisti wakiwa wamechanganyikiwa kabisa, wakitiana panga kila mmoja na wenzake.
21 Now the Hebrews that were with the Philistines as beforetime, and that went up with them into the camp round about; even they also turned to be with the Israelites that were with Saul and Jonathan.
Wale Waebrania ambao walishakuwa pamoja na Wafilisti, na waliokuwa wamepanda pamoja nao katika kambi zao, wakaenda upande wa Waisraeli waliokuwa pamoja na Sauli na Yonathani.
22 Likewise all the men of Israel that had hid themselves in the hill-country of Ephraim, when they heard that the Philistines fled, even they also followed hard after them in the battle.
Waisraeli wote waliokuwa wamejificha katika nchi ya milima ya Efraimu waliposikia kuwa Wafilisti wamekimbia, wakajiunga vitani na kuwafuata kwa bidii.
23 So the LORD saved Israel that day; and the battle passed on as far as Beth-aven.
Hivyo Bwana akawaokoa Waisraeli siku ile, navyo vita vilienea hadi kupita Beth-Aveni.
24 And the men of Israel were distressed that day; but Saul adjured the people, saying: 'Cursed be the man that eateth any food until it be evening, and I be avenged on mine enemies.' So none of the people tasted food.
Basi watu wa Israeli walikuwa katika dhiki siku ile, kwa sababu Sauli alikuwa amewafunga watu kwa kiapo, akisema, “Alaaniwe mtu yeyote ambaye atakula chakula kabla ya jioni, kabla sijalipiza kisasi juu ya adui zangu!” Kwa hiyo hakuna mtu yeyote katika jeshi aliyeonja chakula.
25 And all the people came into the forest; and there was honey upon the ground.
Jeshi lote liliingia mwituni, na huko kulikuwepo na asali ardhini.
26 And when the people were come unto the forest, behold a flow of honey; but no man put his hand to his mouth; for the people feared the oath.
Walipoingia mwituni, wakaona asali ikitiririka, hata hivyo hakuna mtu yeyote aliyetia mkono wake kinywani, kwa sababu waliogopa kiapo.
27 But Jonathan heard not when his father charged the people with the oath; and he put forth the end of the rod that was in his hand, and dipped it in the honeycomb, and put his hand to his mouth; and his eyes brightened.
Lakini Yonathani alikuwa hajasikia kuwa baba yake alikuwa amewafunga watu kwa kiapo, hivyo akainyoosha ncha ya fimbo iliyokuwa mkononi mwake na kuichovya katika sega la asali. Akainua mkono wake na kuutia kinywani mwake, nayo macho yake yakawa maangavu.
28 Then answered one of the people, and said: 'Thy father straitly charged the people with an oath, saying: Cursed be the man that eateth food this day; and the people are faint.'
Kisha mmoja wa askari wake akamwambia, “Baba yako alilifunga jeshi kwa kiapo kikali, akisema, ‘Alaaniwe mtu yeyote alaye chakula leo!’ Ndiyo sababu watu wanalegea.”
29 Then said Jonathan: 'My father hath troubled the land; see, I pray you, how mine eyes are brightened, because I tasted a little of this honey.
Yonathani akasema, “Baba yangu ameitaabisha nchi. Ona jinsi nilivyopata nguvu mpya nilipoonja asali hii kidogo.
30 How much more, if haply the people had eaten freely to-day of the spoil of their enemies which they found? had there not been then a much greater slaughter among the Philistines?'
Ingekuwa bora zaidi mara ngapi kama watu wangalikula leo baadhi ya nyara walizoteka kutoka kwa adui zao. Je, mauaji ya Wafilisti yasingekuwa makubwa zaidi?”
31 And they smote of the Philistines that day from Michmas to Aijalon; and the people were very faint.
Siku ile baada ya Waisraeli kuwaua Wafilisti kutoka Mikmashi mpaka Aiyaloni, walikuwa wamechoka.
32 And the people flew upon the spoil, and took sheep, and oxen, and calves, and slew them on the ground; and the people did eat them with the blood.
Watu wakarukia zile nyara, wakichukua kondoo, ngʼombe na ndama, wakawachinja hapo juu ya nchi na kuwala, pamoja na damu.
33 Then they told Saul, saying: 'Behold, the people sin against the LORD, in that they eat with the blood.' And he said: 'Ye have dealt treacherously; roll a great stone unto me this day.'
Kisha mtu mmoja akamwambia Sauli, “Tazama, watu wanatenda dhambi dhidi ya Bwana kwa kula nyama yenye damu.” Akasema, “Mmevunja uaminifu. Livingirisheni jiwe kubwa hapa mara moja.”
34 And Saul said: 'Disperse yourselves among the people, and say unto them: Bring me hither every man his ox, and every man his sheep, and slay them here, and eat; and sin not against the LORD in eating with the blood.' And all the people brought every man his ox with him that night, and slew them there.
Kisha Sauli akasema, “Nendeni miongoni mwa watu, mwaambie, ‘Kila mmoja wenu aniletee ngʼombe wake na kondoo, mwachinjie hapa na mle. Msitende dhambi dhidi ya Bwana kwa kula nyama ikiwa na damu ndani yake.’” Hivyo kila mmoja akaleta ngʼombe wake jioni ile na kumchinja hapo.
35 And Saul built an altar unto the LORD; the same was the first altar that he built unto the LORD.
Ndipo Sauli akamjengea Bwana madhabahu, na ndiyo ilivyokuwa mara yake ya kwanza kujenga madhabahu.
36 And Saul said: 'Let us go down after the Philistines by night, and spoil them until the morning light, and let us not leave a man of them.' And they said: 'Do whatsoever seemeth good unto thee.' Then said the priest: 'Let us draw near hither unto God.'
Sauli akasema, “Tuteremke tufuatie Wafilisti usiku na kuwateka nyara mpaka mapambazuko, nasi tusiache hata mmoja wao hai.” Wakajibu, “Fanya lolote lile uonalo jema zaidi kwako.” Lakini kuhani akasema, “Tuulize kwa Mungu mahali hapa.”
37 And Saul asked counsel of God: 'Shall I go down after the Philistines? wilt Thou deliver them into the hand of Israel?' But He answered him not that day.
Basi Sauli akamuuliza Mungu, akisema, “Je, niteremke kuwafuatia Wafilisti? Je, utawatia mikononi mwa Israeli?” Lakini Mungu hakumjibu siku ile.
38 And Saul said: 'Draw nigh hither, all ye chiefs of the people; and know and see wherein this sin hath been this day.
Kwa hiyo Sauli akasema, “Njooni hapa, ninyi nyote ambao ni viongozi wa jeshi, na tutafute ni dhambi gani imefanywa leo.
39 For, as the LORD liveth, who saveth Israel, though it be in Jonathan my son, he shall surely die.' But there was not a man among all the people that answered him.
Kwa hakika kama Bwana aiokoaye Israeli aishivyo, hata kama itakuwa juu ya mwana wangu Yonathani, ni lazima afe.” Lakini hakuna mtu yeyote aliyesema neno.
40 Then said he unto all Israel: 'Be ye on one side, and I and Jonathan my son will be on the other side.' And the people said unto Saul: 'Do what seemeth good unto thee.'
Kisha Sauli akawaambia Waisraeli wote, “Ninyi simameni huko; mimi na mwanangu Yonathani tutasimama hapa.” Watu wakajibu, “Fanya lile unaloona jema zaidi kwako.”
41 Therefore Saul said unto the LORD, the God of Israel: 'Declare the right.' And Jonathan and Saul were taken by lot; but the people escaped.
Kisha Sauli akamwomba Bwana, Mungu wa Israeli, akisema, “Nipe jibu lililo sawa.” Yonathani na Sauli wakatolewa kwa kura, nao watu wakawa salama.
42 And Saul said: 'Cast lots between me and Jonathan my son.' And Jonathan was taken.
Sauli akasema, “Pigeni kura kati yangu na mwanangu Yonathani.” Kura ikamwangukia Yonathani.
43 Then Saul said to Jonathan: 'Tell me what thou hast done.' And Jonathan told him, and said: 'I did certainly taste a little honey with the end of the rod that was in my hand; here am I: I will die.'
Basi Sauli akamwambia Yonathani, “Niambie ni nini ulichokifanya.” Hivyo Yonathani akamwambia, “Nilionja tu asali kidogo kwa ncha ya fimbo yangu. Je, sasa ni lazima nife?”
44 And Saul said: 'God do so and more also; thou shalt surely die, Jonathan.'
Sauli akasema, “Mungu na anishughulikie kwa ukali zaidi kama wewe Yonathani hutakufa.”
45 And the people said unto Saul: 'Shall Jonathan die, who hath wrought this great salvation in Israel? Far from it; as the LORD liveth, there shall not one hair of his head fall to the ground; for he hath wrought with God this day.' So the people rescued Jonathan, that he died not.
Lakini watu wakamwambia Sauli, “Je, Yonathani atakufa, yeye ambaye ameleta wokovu huu mkubwa Israeli? Hasha! Hakika kama Bwana aishivyo, hakuna hata unywele wa kichwa chake utakaoanguka juu ya ardhi, kwa kuwa alifanya jambo hili leo kwa msaada wa Mungu.” Basi watu wakamwokoa Yonathani, wala hakuuawa.
46 Then Saul went up from following the Philistines; and the Philistines went to their own place.
Kisha Sauli akaacha kuwafuata Wafilisti, nao wakajiondoa na kurudi katika nchi yao.
47 So Saul took the kingdom over Israel, and fought against all his enemies on every side, against Moab, and against the children of Ammon, and against Edom, and against the kings of Zobah, and against the Philistines; and whithersoever he turned himself, he put them to the worse.
Baada ya Sauli kujitwalia utawala katika Israeli, alipigana dhidi ya adui zake kila upande: Moabu, Waamoni, Edomu, wafalme wa Soba, na Wafilisti. Popote alipogeukia, aliwashinda.
48 And he did valiantly, and smote the Amalekites, and delivered Israel out of the hands of them that spoiled them.
Akapigana kishujaa na kuwashinda Waamaleki, akiikomboa Israeli kutoka mikono ya wale waliokuwa wamewateka nyara.
49 Now the sons of Saul were Jonathan, and Ishvi, and Malchi-shua; and the names of his two daughters were these: the name of the first-born Merab, and the name of the younger Michal;
Wana wa Sauli walikuwa Yonathani, Ishvi na Malki-Shua. Jina la binti yake mkubwa lilikuwa Merabu, naye mdogo aliitwa Mikali.
50 and the name of Saul's wife was Ahinoam the daughter of Ahimaaz; and the name of the captain of his host was Abner, the son of Ner, Saul's uncle.
Jina la mkewe Sauli aliitwa Ahinoamu binti wa Ahimaasi. Jina la jemadari wa jeshi la Sauli aliitwa Abneri mwana wa Neri, naye Neri alikuwa babaye mdogo Sauli.
51 And Kish was the father of Saul, and Ner the father of Abner was the son of Abiel.
Babaye Sauli yaani, Kishi na Neri baba yake Abneri walikuwa wana wa Abieli.
52 And there was sore war against the Philistines all the days of Saul; and when Saul saw any mighty man, or any valiant man, he took him unto him.
Siku zote za utawala wa Sauli zilikuwa za vita vikali dhidi ya Wafilisti, na wakati wowote Sauli alimwona mtu mwenye nguvu au shujaa, alimchukua kwa utumishi wake.

< 1 Samuel 14 >