< Psalms 83 >

1 A song, or Psalme committed to Asaph. Keep not thou silence, O God: bee not still, and cease not, O God.
Ee Mungu, usikae kimya! usitupuuze na kustarehe, Ee Mungu.
2 For lo, thine enemies make a tumult: and they that hate thee, haue lifted vp the head.
Tazama, adui zako wanafanya vurugu, na wale wakuchukiao wameinua vichwa vyao.
3 They haue taken craftie counsell against thy people, and haue consulted against thy secret ones.
Wanafanya hila juu ya watu wako na kwa pamoja kupanga njama dhidi ya wale uwalindao. Wamesema,
4 They haue said, Come and let vs cut them off from being a nation: and let the name of Israel be no more in remembrance.
“Njoni na tuwaangamize wao kama taifa. Kisha jina la Israeli halitakumbukwa.”
5 For they haue consulted together in heart, and haue made a league against thee:
Wamepanga njama pamoja wakiwa na mkakati mmoja; wamefanya muungano dhidi yako.
6 The tabernacles of Edom, and the Ishmaelites, Moab and the Agarims:
Hii inajumuisha hema za Edomu na Waishmaeli, na watu wa Moabu na Wahagari, ambao wamepanga njama pamoja nao
7 Gebal and Ammon, and Amalech, the Philistims with the inhabitants of Tyrus:
Gebal, Amoni, Amaleki; pia inajumuisha Filisti na wenyeji wa Tiro.
8 Asshur also is ioyned with them: they haue bene an arme to the children of Lot. (Selah)
Ashuri pia ameshirikina nao; wanawasaidia wana wa Lutu. Serah
9 Doe thou to them as vnto the Midianites: as to Sisera and as to Iabin at the riuer of Kishon.
Ufanye kwao kama ulivyofanya kwa Midiani, kama ulivyofanya kwa Sisera na kwa Yabini kwenye Mto Kishoni.
10 They perished at En-dor, and were dung for the earth.
Waliangamizwa kule Endori na wakawa kama mbolea juu ya chi.
11 Make them, euen their princes like Oreb and like Zeeb: yea, all their princes like Zebah and like Zalmuna.
Uvifanye vyeo vyao kama Oreb na Zeeb, na wakuu wao wote kama Zeba na Zalmuna.
12 Which haue said, Let vs take for our possession the habitations of God.
Wao walisema, natujimilikishe malisho ya Mungu.”
13 O my God, make them like vnto a wheele, and as the stubble before the winde.
Ee Mungu wangu, uwafanye kama mavumbi ya kisulisuli, kama makapi mbele ya upepo,
14 As the fire burneth the forest, and as the flame setteth the mountaines on fire:
Kama moto uteketezao msitu, na kama miali ya moto iwakayo milimani.
15 So persecute them with thy tempest, and make them afraide with thy storme.
Uwafuatie kwa tufani yako, na kuwafadhaisha kwa dhoruba yako.
16 Fill their faces with shame, that they may seeke thy Name, O Lord.
Uwajaze nyuso zao kwa aibu ili kwamba waweze kulitafuta jina lako, Yahwe.
17 Let them be confounded and troubled for euer: yea, let them be put to shame and perish,
Nao waaibishwe na kufadhaishwa milele; waangamizwe katika aibu.
18 That they may knowe that thou, which art called Iehouah, art alone, euen the most High ouer all the earth.
Kisha watajua kwamba ni wewe pekee, Yahwe, Uliye Juu ya nchi yote.

< Psalms 83 >