< Psalms 45 >

1 To him that excelleth on Shoshannim a song of love to give instruction, committed to the sonnes of Korah. Mine heart will vtter forth a good matter: I wil intreat in my workes of the King: my tongue is as the pen of a swift writer.
Moyo wangu unafurika kwa neno zuri; nitasoma kwa sauti maneno niliyo yaandika kuhusu mfalme; ulimi wangu ni kalamu ya mwandishi mwenye ustadi.
2 Thou art fayrer then the children of men: grace is powred in thy lips, because God hath blessed thee for euer.
Wewe u mzuri sana kuliko mwanadamu yeyote; neema imemiminwa midomoni mwako; Kwa hiyo tunajua ya kuwa Mungu amekubariki milele.
3 Gird thy sword vpon thy thigh, O most mightie, to wit, thy worship and thy glory,
Weka upanga wako upande wako, wewe uliye mwenye nguvu, katika utukufu wako na enzi yako.
4 And prosper with thy glory: ride vpon the worde of trueth and of meekenes and of righteousnes: so thy right hand shall teach thee terrible things.
Katika enzi yako enenda katika ushindi kwa sababu ya uaminifu, upole, na haki; mkono wako wa kuume utakufundisha mambo ya kutisha.
5 Thine arrowes are sharpe to pearce the heart of the Kings enemies: therefore the people shall fall vnder thee.
Mishale yako ni mkali; watu huanguka chini yako; mishale yako imo ndani ya mioyo ya adui za mfalme.
6 Thy throne, O God, is for euer and euer: the scepter of thy kingdome is a scepter of righteousnesse.
Kiti chako cha enzi, Mungu ni cha milele na milele; na fimbo ya haki ni fimbo ya utawala wako.
7 Thou louest righteousnes, and hatest wickednesse, because God, euen thy God hath anoynted thee with the oyle of gladnes aboue thy fellowes.
Umeipenda haki na kuchukia uovu; kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekupaka mafuta ya furaha kuliko wenzako.
8 All thy garments smelll of myrrhe and aloes, and cassia, when thou commest out of the yuorie palaces, where they haue made thee glad.
Mavazi yako yote hunukia manemane, udi, na mdalasini; kukoka katika majumba ya pembe vyombo vya muziki wa nyuzi vimekufurahisha.
9 Kings daugthers were among thine honorable wiues: vpon thy right hand did stand the Queene in a vesture of golde of Ophir.
Binti za wafalme ni kati ya wake zako waheshimiwa; na mkono wako wa kuume amesimama malikia aliye vaa mavazi ya dhahabu ya Ofiri.
10 Hearken, O daughter, and consider, and incline thine eare: forget also thine owne people and thy fathers house.
Sikiliza, mwanangu, tafakari na utege sikio lako; uwasahahu watu wako na watu wa nyumba ya baba yako.
11 So shall the King haue pleasure in thy beautie: for he is thy Lord, and reuerence thou him.
Hivyo mfalme atautamani uzuri wako; yeye ni Bwana wako; umstahi.
12 And the daughter of Tyrus with the rich of the people shall doe homage before thy face with presents.
Binti wa Tiro atakuwepo akiwa na zawadi; matajiri kati wa watu watajipendekeza kwako.
13 The Kings daughter is all glorious within: her clothing is of broydred golde.
Binti mfalme katika jumba la kifahari ana utukufu wote; mavazi yake yametengenezwa kwa dhahabu.
14 She shalbe brought vnto the King in raiment of needle worke: the virgins that follow after her, and her companions shall be brought vnto thee.
Naye ataongozwa kwa mfalme akiwa katika mavazi ya dhahabu; mabikra, wenzake wanoumfuata, wataletwa kwako mafalme.
15 With ioy and gladnes shall they be brought, and shall enter into the Kings palace.
Wao wataongozwa kwa furaha na shangwe; wataingia mahali pa mfalme.
16 In steade of thy fathers shall thy children be: thou shalt make them princes through all the earth.
Katika mahali pa baba zako watoto wako watakuwepo, ambao wewe utawafanya kuwa wakuu katika nchi yote.
17 I will make thy Name to be remembred through all generations: therefore shall the people giue thanks vnto thee world without ende.
Nami nitalifanya jina lako kukumbukwa katika uzao wote; kwa hiyo watu watakushukuru milele na milele.

< Psalms 45 >