< Proverbs 7 >

1 My sonne, keepe my wordes, and hide my commandements with thee.
Mwanangu, yatunze maneno yangu na ndani yako udhihifadhi amri zangu.
2 Keepe my commandements, and thou shalt liue, and mine instruction as the apple of thine eyes.
Uzilinde amri zangu ili uishi na uyatunzetu mafundisho yangu kama mboni ya jicho.
3 Binde them vpon thy fingers, and write them vpon the table of thine heart.
Uyafunge katika vidole vyako; uyaandike katika kibao cha moyo wako.
4 Say vnto wisedome, Thou art my sister: and call vnderstanding thy kinswoman,
Mwambie hekima, “wewe ni dada yangu,” na ufahamu mwite jamaa yako,
5 That they may keepe thee from the strange woman, euen from the stranger that is smoothe in her wordes.
ili ujitunze mwenyewe dhidi ya mwanake haramu, dhidi ya mwanamke mgeni mwenye maneno laini.
6 As I was in the window of mine house, I looked through my windowe,
Nilikuwa naangalia kwenye wavu wa dirisha la nyumba yangu.
7 And I sawe among the fooles, and considered among the children a yong man destitute of vnderstanding,
Nikawatazama watu mwenye ukosefu wa uzoefu, na miongoni mwa watu vijana nikamwona kijana asiye na akili.
8 Who passed through the streete by her corner, and went toward her house,
Kijana huyo alishuka mtaani kwenye kona karibu na yule mwanamke, akaenda kwenye nyumba yake.
9 In the twilight in the euening, when the night began to be blacke and darke.
Ilikuwa katika utusiutusi wa siku muda wa jioni, wakati wa usiku na giza.
10 And beholde, there met him a woman with an harlots behauiour, and subtill in heart.
Akakutana na yule mwanake, amevaa kama kahaba, katika moyo wa udanyanyifu.
11 (She is babling and loud: whose feete can not abide in her house.
Alikuwa na kelele na upotovu; miguu yake haikutulia kwenye masikani.
12 Nowe she is without, nowe in the streetes, and lyeth in waite at euery corner)
Alielekea mitaani, kisha sehemu ya sokoni, na katika kila upande alisubiri kwa kuviza.
13 So she caught him and kissed him and with an impudent face said vnto him,
Basi akamshika na kumbusu, kwa uso wa nguvu akamwambia,
14 I haue peace offerings: this day haue I payed my vowes.
leo nimetoa sadaka yangu ya amani, nimelipa nadhili yangu,
15 Therefore came I forth to meete thee, that I might seeke thy face: and I haue found thee.
hivyo nilikuja kukutana nawe, kuutafuta uso wako kwa hamu, na sasa nimekupata.
16 I haue deckt my bed with ornaments, carpets and laces of Egypt.
Nimeweka matandiko juu ya kitanda changu, kitani za rangi kutoka Misri.
17 I haue perfumed my bedde with myrrhe, aloes, and cynamom.
Kitanda changu nimenyunyizia manemane, udi na mdalasini.
18 Come, let vs take our fill of loue vntill the morning: let vs take our pleasure in daliance.
Njoo, tunywe tujishibishe kwa upendo wetu hata asubuhi; tupate furaha kuu kwa matendo ya mahaba.
19 For mine husband is not at home: he is gone a iourney farre off.
Maana mume wangu hayupo nyumbani kwake; amekwenda safari ya mbali.
20 He hath taken with him a bagge of siluer, and will come home at the day appointed.
Alichukua mkoba wa fedha; atarudi siku ya mwezi mpevu.
21 Thus with her great craft she caused him to yeelde, and with her flattering lips she entised him.
katika maneno yake mengi akamshinda; na kwa midomo yake laini anampotosha.
22 And he followed her straight wayes, as an oxe that goeth to the slaughter, and as a foole to the stockes for correction,
Ghafula alimfuata kama maksai anayekwenda kwa mchinjaji, kama ayala aliyekamatwa kwa nguvu,
23 Till a dart strike through his liuer, as a bird hasteth to the snare, not knowing that he is in danger.
mpaka mshale upasue ini lake. Alikuwa kama ndege anayekimbili kwenye mtego. Hakujua kuwa itamgharimu maisha yake.
24 Heare me now therefore, O children, and hearken to the wordes of my mouth.
Na sasa, wanangu, nisikilizeni; zingatieni maneno ya kinywa changu.
25 Let not thine heart decline to her wayes: wander thou not in her paths.
Moyo wako usiyageukie mapito yake; usipotoshwe katika mapito yake.
26 For shee hath caused many to fall downe wounded, and the strong men are all slaine by her.
Amesababisha watu wengi kuanguka kwa kuwajeruhi; ameua watu wengi.
27 Her house is the way vnto ye graue, which goeth downe to the chambers of death. (Sheol h7585)
Nyumba yake ipo juu ya barabara ya kwenda kuzimu; huelekea chini kwenye vyumba vya mauti. (Sheol h7585)

< Proverbs 7 >