< Nehemiah 6 >

1 And when Sanballat, and Tobiah, and Geshem the Arabian, and the rest of our enemies heard that I had built the wall, and that there were no more breaches therein, (though at that time I had not set vp the doores vpon the gates)
Wakati Sanbalati, Tobia, Geshemu Mwarabu na adui zetu wengine waliposikia kwamba nilijenga upya ukuta na kwamba hakuna sehemu yoyote iliyoachwa ya wazi, ingawa sijawaweka milango katika malango,
2 Then sent Sanballat and Geshem vnto me, saying, Come thou that we may meete together in the villages in the plaine of Ono: and they thought to doe me euill.
Sanbalati na Geshemu akatuma wajumbe akasema, “Njoni, tukutane pamoja mahali fulani katika tambarare ya Ono.” Lakini walitaka kunidhuru.
3 Therefore I sent messengers vnto them, saying, I haue a great worke to doe, and I can not come downe: why should the worke cease, whiles I leaue it, and come downe to you?
Niliwatuma wajumbe kwao, nikasema, “Ninafanya kazi kubwa na siwezi kushuka. Kwa nini kazi isimame wakati nitakapoondoka na kuja kwako?”
4 Yet they sent vnto me foure times after this sort. And I answered them after the same maner.
Walituma ujumbe huo huo mara nne, na mimi niliwajibu vile vile kila wakati.
5 Then sent Sanballat his seruant after this sorte vnto me the fift time, with an open letter in his hand,
Sanbalati alimtuma mtumishi wake kwangu kwa njia ile ile mara ya tano, na barua iliyo wazi mkononi mwake.
6 Wherein was written, It is reported among the heathen, and Gashmu hath sayd it, that thou and the Iewes thinke to rebel, for the which cause thou buildest the wall and thou wilt bee their King according to these wordes.
Imeandikwa, “Inaripotiwa kati ya mataifa, na Geshemu pia anasema, kwamba wewe na Wayahudi mna mpango wa kuasi, kwa sababu hiyo ndio mnajenga ukuta. Kutokana na taarifa hizi, unakaribia kuwa mfalme wao.
7 Thou hast also ordeyned the Prophets to preach of thee at Ierusalem, saying, There is a King in Iudah: and nowe according to these wordes it shall come to the Kings eares: come now therefore, and let vs take counsell together.
Nawe umewachagua manabii kutangaza habari zako juu ya Yerusalemu, wakisema, “Kuna mfalme huko Yuda!” Unaweza kuwa na hakika mfalme atasikia ripoti hizi. Basi, hebu njoo tuzungumze.
8 Then I sent vnto him, saying, It is not done according to these wordes that thou sayest: for thou feynest them of thine owne heart.
Kisha nikamtuma neno nikisema, “mambo kama hayo hayajafanyika kama unavyosema, kwa maana ndani ya moyo wako umeyabuni.”
9 For all they afrayed vs, saying, Their handes shalbe weakened from the worke, and it shall not be done: nowe therefore incourage thou me.
Kwa maana wote walitaka kututisha, wakifikiri, “Wataacha mikono yao kufanya kazi hiyo, na haitafanyika.” Lakini sasa, Mungu, tafadhali imarisha mikono yangu.
10 And I came to the house of Shemaiah the sonne of Delaiah the sonne of Mehetabeel, and he was shut vp, and he said, Let vs come together into the house of God in the middes of the Temple, and shut the doores of the Temple: for they will come to slay thee: yea, in the night will they come to kill thee.
Nikaenda nyumbani kwa Shemaya mwana wa Delaya, mwana wa Mehetabeli, aliyefungwa nyumbani mwake. Akasema, “Hebu tukutane pamoja katika nyumba ya Mungu, ndani ya hekalu, na tufunge milango ya hekalu, kwa maana wanakuja kukuua. Usiku wanakuja kukuua.”
11 Then I said, Should such a man as I, flee? Who is he, being as I am, that would go into the Temple to liue? I will not goe in.
Nikajibu, “Je! Mtu kama mimi ninaweza kukimbia? Na mtu kama mimi ninaweza kuingia hekaluni ili nipate kuishi? Sitaingia.”
12 And loe, I perceiued, that God had not sent him, but that he pronounced this prophecie against me: for Tobiah and Sanballat had hired him.
Niligundua kwamba sio Mungu aliyemtuma, lakini alikuwa amefanya unabii dhidi yangu. Tobia na Sanbalati walimwajiri.
13 Therefore was he hyred, that I might be afrayde, and doe thus, and sinne, and that they might haue an euill report that they might reproche me.
Walimpa kazi kunifanya niwe na hofu, ili nifanye kile alichosema na kutenda dhambi, hivyo wangeweza kunipa jina baya ili kuniaibisha.
14 My God, remember thou Tobiah, and Sanballat according vnto these their workes, and Noadiah the Prophetesse also, and the rest of the Prophets that would haue put me in feare.
Mungu wangu, wakumbuke Tobia na Sanbalati, na yote waliyofanya. Pia mkumbuke nabii Noadia na manabii wengine ambao walijaribu kunifanya niogope.
15 Notwithstanding the wall was finished on the fiue and twentieth day of Elul, in two and fiftie dayes.
Kwa hiyo ukuta ukamalizika siku ya ishirini na tano ya mwezi wa Eluli, baada ya siku hamsini na mbili.
16 And when all our enemies heard thereof, euen all the heathen that were about vs, they were afraid, and their courage failed them: for they knew, that this worke was wrought by our God.
Adui zetu wote waliposikia hayo, mataifa yote yaliyotuzunguka, waliogopa na wakakata tamaa sana machoni pao wenyewe. Kwa maana walijua kazi hiyo ilifanyika kwa msaada wa Mungu wetu.
17 And in these dayes were there many of the princes of Iudah, whose letters went vnto Tobiah, and those of Tobiah came vnto them.
Wakati huu wakuu wa Yuda walituma barua nyingi kwa Tobia, na barua za Tobia zikawajia.
18 For there were many in Iudah, that were sworne vnto him: for he was the sonne in lawe of Shechaniah, the sonne of Arah: and his sonne Iehonathan had the daughter of Meshullam, the sonne of Berechiah.
Kwa maana walikuwa wengi huko Yuda waliofungwa kwa kiapo chake, kwa sababu alikuwa mkwewe Shekania, mwana wa Ara. Mwanawe Yehohanani alikuwa amekuwa mkewe Meshulamu mwana wa Berekia.
19 Yea, they spake in his praise before me, and tolde him my wordes, and Tobiah sent letters to put me in feare.
Pia walizungumza nami kuhusu matendo yake mema na kumwambia maneno yangu. Barua zililetwa kwangu kutoka kwa Tobia kunitisha.

< Nehemiah 6 >