< Joshua 3 >

1 Then Ioshua rose very earely, and they remoued from Shittim, and came to Iorden, he, and all the children of Israel, and lodged there, before they went ouer.
Yoshua aliamka asubuhi na mapema, nao walisafiri kutoka Shitimu. Walifika Yordani, yeye na watu wote wa Israeli, na wakapiga kambi hapo kabla hawajavuka ng'ambo.
2 And after three dayes the officers went throughout the hoste,
Baada ya siku tatu, maafisa walienda katika kambi, wakawaagiza watu,
3 And commanded the people, saying, When ye see the Arke of the couenat of the Lord your God, and the Priestes of the Leuites bearing it, ye shall depart from your place, and goe after it.
“Mtakapoona sanduku la agano la Yahweh Mungu wenu, na makuhani kutoka miongoni mwa Walawi wamelibeba, ni lazima muondoke sehemu hii na kulifuata.
4 Yet there shalbe a space betweene you and it, about two thousande cubites by measure: ye shall not come neere vnto it, that ye may knowe the way, by the which ye shall goe: for ye haue not gone this way in times past.
Lazima kuwe na umbali wa dhiraa elfu moja kati yenu na sanduku. Msilisogelee karibu, ili muweze kuiona njia ya kupitia, kwakuwa hamjawahi kupita njia hii kabla.
5 (Nowe Ioshua had saide vnto the people, Sanctifie your selues: for to morowe the Lord will doe wonders among you)
Yoshua akawaambia watu, “Jitakaseni ninyi wenyewe keso, kwa kuwa Yahweh atafanya maajabu miongoni mwenu.”
6 Also Ioshua spake vnto the Priestes, saying, Take vp the Arke of the couenant, and goe ouer before the people: so they tooke vp the Arke of the couenant, and went before the people.
Kisha Yoshua akawaambia makuhani, “Chukueni sanduku la agano, na kulipitisha mbele za watu.” Hivyo, wakalichukua sanduku la agano na wakaenda mbele za watu.
7 Then the Lord saide vnto Ioshua, This day will I begin to magnifie thee in the sight of all Israel, which shall knowe, that as I was with Moses, so will I be with thee.
Yahweh akamwambia Yoshua, “Siku hii nitakufanya kuwa mtu mkubwa katika macho ya Waisraeli wote. Watajua kuwa kama nilivyokuwa na Musa ndivyo nitakavyokuwa pamoja na wewe.
8 Thou shalt therefore command the Priests that beare the Arke of the Couenant, saying, When ye are come to the brinke of the waters of Iorden, ye shall stande still in Iorden.
Utawaamuru makuhani ambao hulibeba sanduku la agano, 'Mtakapofika katika ukingo wa maji ya Yordani, ni lazima msimame katika Mto Yordani.'”
9 Then Ioshua said vnto the children of Israel, Come hither, and heare the wordes of the Lord your God.
Kisha Yoshu akawaambia watu wa Israeli, “Njooni hapa na msikilize maneno ya Yahweh Mungu wenu.
10 And Ioshua said, Hereby ye shall know that the liuing God is among you, and that he will certainely cast out before you the Canaanites, and the Hittites, and the Hiuites, and the Perizzites, and the Girgashites, and the Amorites, and the Iebusites.
Kwa hili mtajua kwamba Mungu aliye hai yuko miongoni mwenu na kwamba atawaondosha mbele yenu Wakanaani, Wahiti, Wahivi, Waperizi, Wagrigashi, Waamori na Wayebusi.
11 Beholde, the Arke of the couenant of the Lord of all the worlde passeth before you into Iorden.
Tazama! Sanduku la agano la Bwana wa nchi yote litavuka mbele yenu katika Yordani.
12 Nowe therefore take from among you twelue men out of the tribes of Israel, out of euery tribe a man.
Sasa chagueni wanaume kumi na wawili kutoka katika makabila ya Israeli, mmoja katika kila kabila.
13 And assoone as the soles of the feete of the Priestes (that beare the Arke of the Lord God the Lord of all the worlde) shall stay in the waters of Iorden, the waters of Iorden shall be cut off: for the waters that come from aboue, shall stande still vpon an heape.
Wakati nyayo za miguu ya makuhani walichukualo sanduku la Yahweh, Bwana wa nchi yote, zitakapogusa maji ya Yordani, maji ya Yordani yatatindika, na hata maji yatiririkayo kutoka juu yatakoma kutiririka nayo yatasimama kama chuguu.
14 Then when the people were departed from their tentes to goe ouer Iorden, the Priestes bearing the Arke of the Couenant, went before people.
Hivyo wakati watu walipotoka ili kuvuka Yordani, makuhani waliobeba sanduku la agano waende mbele ya watu.
15 And as they that bare the Arke came vnto Iorden, and the feete of the Priestes that bare the Arke were dipped in the brinke of the water, (for Iorden vseth to fill all his bankes all the time of haruest)
Mara tu wale walichukuao sanduku wakiisha kufika Yordani, na miguu ya watu wale waliobeba sanduku itakapotiwa katika ukingo wa maji (maana sasa Yordani hujaa hadi katika kingo zake zote katika kipindi chote cha mavuno),
16 Then the waters that came downe from aboue, stayed and rose vpon an heape and departed farre from the citie of Adam, that was beside Zaretan: but the waters that came downe towarde the Sea of the wildernes, euen the salt Sea, failed, and were cut off: so the people went right ouer against Iericho.
maji yote yaliyotiririka kutoka juu yalisimama katika chuguu kimoja. Maji yakakoma kutiririka kutoka katika umbali mrefu. Maji yaliacha kutiririka kutoka Adam, mji ulio karibu na Zarethani, hadi bahari ya Negevu, Bahari ya Chumvi. Na watu walivuka ng'ambo karibu na Yeriko.
17 But the Priestes that bare the Arke of the couenant of the Lord, stoode drie within Iorden readie prepared, and all the Israelites went ouer dry, vntill all the people were gone cleane ouer through Iorden.
Makuhani waliolibeba sanduku la agano la Yahweh walisimama katika nchi kavu katikati ya Yordani mpaka watu wote wa Israeli walipokwisha kuvuka katika nchi kavu.

< Joshua 3 >