< Joshua 2 >

1 Then Ioshua the sonne of Nun sent out of Shittim two men to spie secretly, saying, Go, view the land, and also Iericho: and they went, and came into an harlots house, named Rahab, and lodged there.
Kisha Yoshua mwana wa Nuni aliwatuma watu wawili kwa siri kama wapelelezi kutoka Shitimu. Akisema, “Nendeni mkaiangalie nchi, hasa Yeriko.” Walienda na wakafika katika nyumba ya kahaba ambaye jina lake ni Rahabu, na wakalala hapo.
2 Then report was made to the King of Iericho, saying, Beholde, there came men hither to night, of the children of Israel, to spie out the countrey.
Mfalme wa Yeriko aliambiwa, “Tazama watu wa Israeli wamekuja kuipeleleza nchi.”
3 And the King of Iericho sent vnto Rahab, saying, Bring foorth the men that are come to thee, and which are entred into thine house: for they be come to search out all the land.
Mfalme akatuma neno kwa Rahabu kusema, “Watoe watu waliokuja kwako ambao wameingia nyumbani mwako, kwa kuwa wamekuja kuipeleleza nchi yote.”
4 (But ye woman had taken the two men, and hid them) Therefore saide she thus, There came men vnto me, but I wist not whence they were.
Lakini mwanamke alikuwa amekwisha kuwachukua wale watu wawili na kuwaficha. Na akasema, “Ndiyo, watu walikuja kwangu, lakini sikujua walikotoka.
5 And when they shut the gate in the darke, the men went out, whither the men went I wote not: follow ye after them quickly, for ye shall ouertake them.
Ilipokuwa jioni wakati wa kufungwa kwa lango la mji, waliondoka. Sijui mahali walikoelekea. Mnaweza kuwakamata kama mtawafuata upesi.
6 (But she had brought them vp to the roofe of the house, and hidde them with the stalkes of flaxe, which she had spread abroad vpon the roofe)
Lakini yeye aliwapandisha juu darini na kuwaficha kwa mabua ya kitani ambayo alikuwa ameyalaza darini.
7 And certaine men pursued after them, the way to Iorden, vnto the foordes, and as soone as they which pursued after them, were gone out, they shut the gate.
Hivyo, watu waliwafuatilia njiani iliyoeleka katika vivuko vya Yordani. Na milango ilifungwa mara tu baada ya wale watu waliofuata kutoka nje.
8 And before they were a sleepe, she came vp vnto them vpon the roofe,
Wale wanaume walikuwa hajalala usiku, wakati alipowaendea kule darini.
9 And saide vnto the men, I knowe that the Lord hath giuen you the land, and that the feare of you is fallen vpon vs, and that all the inhabitants of the land faint because of you.
Akawaambia, “Ninajua kwamba Yahweh amewapa ninyi nchi na kwamba hofu juu yenu imetuingia. Watu wote wanaoishi katika nchi watayeyuka mbele yenu.
10 For we haue heard, howe the Lord dried vp the water of the redde Sea before you, when you came out of Egypt, and what you did vnto the two Kings of the Amorites, that were on the other side Iorden, vnto Sihon and to Og, whom ye vtterly destroyed:
Tumesikia jinsi ambavyo Yahweh alivyokausha maji ya Bahari ya Mianzi kwa ajili yenu wakati mkitoka Misri. Na tumesikia mlichokifanya kwa wafalme wawili wa Waamori walioko upande mwingine wa Yordani - Sihoni na Ogu - ambao mmewaangamiza kabisa.
11 And when wee heard it, our heartes did faint, and there remained no more courage in any because of you: for the Lord your God, he is the God in heauen aboue, and in earth beneath.
Mara tu tuliposikia, mioyo yetu iliyeyuka na hapakuwa na ujasiri wowote uliosalia kwa mtu yeyote - kwa kuwa Yahweh Mungu wenu, ni Mungu aliye juu mbinguni na chini duniani.
12 Now therefore, I pray you, sweare vnto me by the Lord; that as I haue shewed you mercie, ye will also shewe mercie vnto my fathers house, and giue me a true token,
Sasa basi, tafadhali mniapie kwa Yahweh kwamba kama nilivyokuwa mwema kweu, nanyi pia mtaitendea mema nyumba ya baba yangu. Nipeni ishara ya uhakika
13 And that yee will saue aliue my father and my mother, and my brethren, and my sisters, and all that they haue: and that yee will deliuer our soules from death.
kwamba mtanihifadhi maisha ya baba, mama, kaka, dada zangu na famiie zao, na kwamba mtatuokoa kutoka katika kifo.
14 And the men answered her, Our life for you to die, if ye vtter not this our businesse: and when the Lord hath giuen vs the lande, we will deale mercifully and truely with thee.
Wanaume wakamjibu, “maisha yetu kwa ajili ya yenu, hata kifo! Kama hamtasema habari zetu, na Yahweh akisha kutupa nchi hii, tutakuwa wenye huruma na waaminifu kwenu.”
15 Then she let them downe by a corde thorowe the windowe: for her house was vpon the towne wall, and she dwelt vpon the wall.
hivyo aliwashusha chini kwa kupitia dirishani kwa kutumia kamba. Nyumba ambayo alikuwa anaishi ilijengwa katika ukuta wa mji.
16 And she said vnto them, Goe you into the mountaine, least the pursuers meete with you, and hide your selues there three dayes, vntill the pursuers be returned: then afterwarde may yee goe your way.
Akawaambia, “Nendeni milimani la sivyo watu waliowafuata watawaona. Jificheni huko kwa siku tatu mpaka watu waliowafuata watakaporudi. Kisha nendeni zenu.”
17 And the men said vnto her, We will be blamelesse of this thine othe, which thou hast made vs sweare.
Wanaume wakamwambia, “Hatutakuwa tumefungwa na ahadi ulizotufanya tuape mbele zako, kama hautalifanya hili.
18 Behold, when we come into the land, thou shalt bind this cord of red threde in the window, whereby thou lettest vs downe, and thou shalt bring thy father and thy mother, and thy brethren, and all thy fathers houshold home to thee.
Tutakapokuja katika nchi, ni lazima uifunge kamba hii nyekundu katika dirisha ulilotushushia chini, na utawakusanya katika nyumba baba yako, mama yako, kaka zako na wote wa nyumba ya baba yako.
19 And whosoeuer then doeth goe out at the doores of thine house into the streete, his blood shalbe vpon his head, and we will be giltlesse: but whosoeuer shall be with thee in the house, his blood shalbe on our head, if any hande touch him:
Na yeyote aendaye mtaani nje ya milango ya nyumba yako, damu yao itakuwa juu ya vichwa vyao na hatutakuwa na hatia yoyote. Lakini kama mkono utanyoshwa juu ya mtu yeyote aliye pamoja nawe katika nyumba, damu yake itakuwa juu ya vichwa vyetu.
20 And if thou vtter this our matter, we will be quite of thine othe, which thou hast made vs sweare.
Na ikiwa utaongea juu ya suala letu, tutakuwa huru dhidi ya kiapo ulichotuapisha.
21 And she answered, According vnto your wordes, so be it: then she sent them away, and they departed, and she bound the red cord in ye window.
Rahabu akawajibu, “Yote mliyosema nayatimie.” Akawatoa mbali na wakaondoka. Kisha akaifunga kamba nyekundu katika dirisha.
22 And they departed, and came into the mountaine, and there abode three dayes, vntil the pursuers were returned: and the pursuers sought them throughout all the way, but founde them not.
Wakaondoka na kwenda juu milimani na walikaa huko kwa siku tatu hadi pale wale waliowafuatilia waliporudi. Wale waliowafuata walitafuta njiani pote bila kuwaona.
23 So the two men returned, and descended from the mountaine, and passed ouer, and came to Ioshua the sonne of Nun, and tolde him all things that came vnto them.
Wale watu wawili walirudi na kuvuka mto na wakafika kwa Yoshua mwana wa Nuni, na walimwambia kila kitu kilichotokea kwao.
24 Also they saide vnto Ioshua, Surely the Lord hath deliuered into our handes all the lande: for euen all the inhabitants of the countrey faint because of vs.
Nao wakasema kwa Joshua, “kwa kweli Yahweh ametupa nchi hii. Wenyeji wote wa nchi wanayeyuka kwasababu yetu.

< Joshua 2 >