< Job 37 >

1 At this also mine heart is astonied, and is mooued out of his place.
Hakika, moyo wangu hutetemeka kwa hili; umeondolewa kutoka katika sehemu yake.
2 Heare the sound of his voyce, and the noyse that goeth out of his mouth.
Sikia, Ee, Sikia kelele za sauti yake, sauti inayotoka katika mdomo wake.
3 He directeth it vnder the whole heauen, and his light vnto the endes of the world.
Huiagiza sauti chini ya mbingu yote, na huutuma mwanga wake katika mipaka ya dunia.
4 After it a noyse soundeth: hee thundereth with the voyce of his maiestie, and hee will not stay them when his voyce is heard.
Sauti huunguruma baada yake; yeye huunguruma kwa sauti ya ukuu wake; hauzuii mshindo wa mwanga wakati sauti yake inaposikika.
5 God thundereth marueilously with his voyce: he worketh great things, which we know not.
Mungu huunguruma kwa sauti yake kwa namna ya ajabu; yeye hufanya mambo makubwa ambayo sisi hatuwezi kuyafahamu.
6 For he sayth to the snowe, Be thou vpon the earth: likewise to the small rayne and to the great rayne of his power.
Kwa kuwa huiambia theluji, 'Angukeni juu ya dunia'; hali kadhalika kwa manyunyu ya mvua, 'Iweni manyunyu makubwa ya mvua.'
7 With the force thereof he shutteth vp euery man, that all men may knowe his worke.
Huuzuia mkono wa kila mtu usifanye kazi, ili kwamba watu wote aliowaumba wataona matendo yake.
8 Then the beastes go into the denne, and remaine in their places.
Kisha hayawani huenda na kujificha na kukaa katika mapango yake.
9 The whirlewind commeth out of the South, and the colde from the North winde.
Dhoruba hutoka katika chumba chake upande wa kusini na baridi kutoka katika pepo zilizotawanyika katika upande wa Kaskazini.
10 At the breath of God the frost is giuen, and the breadth of the waters is made narrowe.
Barafu imetolewa kwa pumzi ya Mungu; upana wa maji umeganda kama chuma.
11 He maketh also the cloudes to labour, to water the earth, and scattereth the cloude of his light.
Hakika, huyapima mawingu manene yenye unyevu; yeye huusambaza mwanga wake katika mawingu.
12 And it is turned about by his gouernment, that they may doe whatsoeuer he commandeth them vpon the whole worlde:
Yeye huyazungusha mawingu kwa uongozi wake, ili yafanye chochote anayoyaagiza juu ya uso wote wa ulimwengu.
13 Whether it be for punishment, or for his lande, or of mercie, he causeth it to come.
Huyafanya haya yote yatokee; wakati mwingine hutokea kwa ajili ya kusahihisha, wakati mwingine kwa ajili ya nchi yake, na wakati mwingine ni kwa matendo ya agano la uaminifu.
14 Hearken vnto this, O Iob: stand and consider the wonderous workes of God.
Yasikilize haya, Ayubu; acha na ufikiri juu matendo ya ajabu ya Mungu.
15 Diddest thou knowe when God disposed them? and caused the light of his cloud to shine?
Je unajua ni kwa namna gani Mungu hushurutisha mawingu na kuufanya mwanga wa radi ung'ae ndani yake?
16 Hast thou knowen the varietie of the cloude, and the wonderous workes of him, that is perfite in knowledge?
Je unafahamu kuelea kwa mawingu, matendo ya ajabu ya Mungu, Je ni nani aliyemkamilifu katika maarifa?
17 Or howe thy clothes are warme, when he maketh the earth quiet through the South winde?
Je unafahamu ni kwa jinsi gani mavazi yako huwa ya moto wakati nchi ikiwa imetulia kwasababu ya upepo unaotoka upande wa kusini?
18 Hast thou stretched out the heaues, which are strong, and as a molten glasse?
Je unaweza kulitandaza anga kama anavyofanya - anga ambalo lina nguvu kama kioo cha chuma kigumu?
19 Tell vs what we shall say vnto him: for we can not dispose our matter because of darknes.
Tufundishe sisi kile tunachopaswa kumwambia yeye, kwa kuwa hatuwezi kutoa hoja zetu katika mpangilio kwasababu ya kiza katika akili zetu.
20 Shall it be told him when I speake? or shall man speake when he shalbe destroyed?
Je anapaswa kuambiwa kwamba ninapenda kuongea naye? Je mtu angependa kumezwa?
21 And nowe men see not the light, which shineth in the cloudes, but the winde passeth and clenseth them.
Sasa, watu hawawezi kulitazama jua wakati linang'aa katika anga baada ya upepo kupita katikati yake na umelisafisha kwa mawingu yake.
22 The brightnesse commeth out of the North: the praise thereof is to God, which is terrible.
Kutoka upande wa kaskazini hutokea fahari ya dhahabu - juu ya Mungu kuna ukuu wa kutisha.
23 It is the Almightie: we can not finde him out: he is excellent in power and iudgement, and aboundant in iustice: he afflicteth not.
Na kuhusu Mwenye nguvu, hatuwezi kumpata; yeye ni mkuu katika nguvu na haki. Yeye hatesi watu.
24 Let men therefore feare him: for he will not regarde any that are wise in their owne conceit.
Hivyo basi, watu humwogopa. Yeye huwa hawajali wale ambao ni wenye hekima katika akili zao wenyewe.”

< Job 37 >