< Job 29 >

1 So Iob proceeded and continued his parable, saying,
Ayubu akaendelea na kusema,
2 Oh that I were as in times past, when God preserued me!
Ee, ningekuwa kama nilivyokuwa miezi iliyopita wakati Mungu aliponiagalia,
3 When his light shined vpon mine head: and when by his light I walked thorowe the darkenesse,
taa yake ilipowaka kichwani pangu, na pale nilipotembea gizani kwa nuru yake.
4 As I was in the dayes of my youth: when Gods prouidence was vpon my tabernacle:
Ee, kwamba ningekuwa kama nilivyokuwa katika siku za ujana wangu uhusiano wangu na Mungu ulivyokuwa mzuri,
5 When the almightie was yet with me, and my children round about me.
wakati Mwenyezi alipokuwa pamoja nami, na wanangu walipokuwa karibu nami,
6 When I washed my pathes with butter, and when the rocke powred me out riuers of oyle:
wakati maisha yangu yalipokuwa yamejawa na utele, na mwamba uliponichuruzishia chemichemi za mafuta.
7 When I went out to the gate, euen to the iudgement seat, and when I caused them to prepare my seate in the streete.
Nilipokwenda langoni mwa mji, nilipokaa katika eneo la mji,
8 The yong men saw me, and hid themselues, and the aged arose, and stood vp.
vijana waliniona na walikaa mbali kwa kuniheshimu, na wazee waliinuka na kusimama kwa ajili yangu.
9 The princes stayed talke, and layde their hand on their mouth.
Wana wa mfalme waliacha kuongea nilipofika; wangeweka mkono wao katika vinywa vyao.
10 The voyce of princes was hidde, and their tongue cleaued to the roofe of their mouth.
Sauti za waheshimiwa zililazimishwa, na ndimi zao hazikuweza kuongea vinywani mwao.
11 And when the eare heard me, it blessed me: and when the eye sawe me, it gaue witnesse to me.
Kwani baada ya kunisikia, wangenibariki; waliponiona, wangeniona na kuniheshimu
12 For I deliuered the poore that cryed, and the fatherlesse, and him that had none to helpe him.
kwa maana nilikuwa nikiwasaidia masikini waliokuwa wakiteseka, na yatima, asiye na msaada.
13 The blessing of him that was ready to perish, came vpon me, and I caused the widowes heart to reioyce.
Baraka zao waliokuwa karibu kuangamia zilinipata; niliufanya moyo wa mjane kuimba kwa furaha.
14 I put on iustice, and it couered me: my iudgement was as a robe, and a crowne.
Nilijivika utakatifu, nao ulinifunika; haki yangu ilikuwa kama kanzu na kilemba.
15 I was the eyes to the blinde, and I was the feete to the lame.
Niliwasaidia vipofu; niliwasaidia walemavu.
16 I was a father vnto the poore, and when I knewe not the cause, I sought it out diligently.
Niliwasaidia wahitaji; niliwasaidia hata wasionijua.
17 I brake also the chawes of the vnrighteous man, and pluckt the praye out of his teeth.
Nilimnyamazisha mwovu; nilimpokonya manusura kutoka katika meno yake.
18 Then I sayde, I shall die in my nest, and I shall multiplie my dayes as the sand.
Kisha nilisema nitakufa mahali salama; nitazizidisha siku zangu kama mchanga.
19 For my roote is spread out by the water, and the dewe shall lye vpon my branche.
Mizizi yangu imeenea majini, na umande kukaa usiku wote katika matawi yangu.
20 My glory shall renue towarde me, and my bowe shall be restored in mine hand.
Heshima yangu ni mpya daima, na nguvu za upinde wangu zipo katika mkono wangu kila wakati.
21 Vnto me men gaue eare, and wayted, and helde their tongue at my counsell.
Watu walinisikiliza; walinisubiri; walisikiliza ushauri wangu.
22 After my wordes they replied not, and my talke dropped vpon them.
Nilipo maliza kuongea hawakunena tena, maneno yangu yaliwatia nguvu kama mvua.
23 And they wayted for me, as for the raine, and they opened their mouth as for the latter rayne.
Waliningoja kama kungoja mvua; waliyathamini maneno yangu, kama walivyotamani mvua iliyokawia.
24 If I laughed on them, they beleeued it not: neither did they cause the light of my countenance to fall.
Niliwafurahia bila wao kutarajia; hawakukataa uzuri wa uso wangu.
25 I appoynted out their way, and did sit as chiefe, and dwelt as a King in the army, and like him that comforteth the mourners.
Nilikuwa kama mfalme wao na kuwachagulia cha kufanya; nilikuwa kama mfalme katika jeshi lake, kama awafarijiye waombolezaji mazishini.

< Job 29 >