< Genesis 9 >

1 And God blessed Noah and his sonnes, and said to them, Bring foorth fruite, and multiplie, and replenish the earth.
Kisha Mungu akambariki Nuhu na wanawe, na kuwaambia, “Zaeni, mkaongezeke, na muijaze nchi.
2 Also the feare of you, and the dread of you shalbe vpon euery beast of the earth, and vpon euery foule of the heauen, vpon all that moueth on the earth, and vpon all the fishes of the sea: into your hand are they deliuered.
Hofu na utisho wenu vitakuwa juu ya kila mnyama aliye hai juu ya nchi, juu ya kila ndege wa angani, juu ya kila kitu kiendacho chini juu ya ardhi, na juu ya samaki wote wa baharini. Vimetolewa katika mikono yenu.
3 Euery thing that moueth and liueth, shall be meate for you: as the greene herbe, haue I giuen you all things.
Kila kitu kiendacho kilicho hai kitakuwa chakula kwa ajili yenu. Kama nilivyo wapa mimea, sasa nawapa kila kitu.
4 But flesh with the life thereof, I meane, with the blood thereof, shall ye not eate.
Lakini msile nyama pamoja na uhai wake - yaani damu yake - ndani yake.
5 For surely I will require your blood, wherein your liues are: at the hand of euery beast will I require it: and at the hand of man, euen at the hand of a mans brother will I require the life of man.
Lakini kwa ajili ya damu yenu, uhai uliomo katika damu yenu nitataka malipo. Kutoka katika mkono wa kila mnyama nitaitaka. Kutoka katika mkono wa kila mtu, yaani, kutoka katika mkono wa yule ambaye amemuua ndugu yake, nitataka fidia kwa ajili ya uhai wa mtu huyo.
6 Who so sheadeth mans blood, by man shall his blood be shed: for in the image of God hath he made man.
Yeyote amwagaye damu ya mtu, kwa njia ya mtu damu yake itamwagwa, kwa sababu ilikuwa ni katika mfano wa Mungu kwamba Mungu alimuumba mtu.
7 But bring ye forth fruite and multiplie: grow plentifully in the earth, and increase therein.
Na hivyo nanyi zaeni na kuongezeka, sambaeni katika inchi yote na muongezeke juu yake.”
8 God spake also to Noah and to his sonnes with him, saying,
Kisha Mungu akazungumza na Nuhu na wanae pamoja naye, akisema,
9 Behold, I, euen I establish my couenant with you, and with your seede after you,
“Kwa ajili yangu, sikiliza! Ninakwenda kulithibitisha agano langu pamoja nawe na uzao wenu baada yenu,
10 And with euery liuing creature that is with you, with the foule, with the cattell, and with euery beast of the earth with you, from all that goe out of the Arke, vnto euery beast of the earth.
na kwa kila kiumbe hai kilicho pamoja nawe, pamoja na ndege, mnyama wa kufugwa, na kila kiumbe cha nchi pamoja nawe, kuanzia kwa wote waliotoka kwenye safina, mpaka kwa kila kiumbe hai juu ya nchi.
11 And my couenant will I establish with you, that from henceforth all flesh shall not be rooted out by ye waters of the flood, neither shall there be a flood to destroy the earth any more.
Kwa sababu hii ninalithibitisha agano langu pamoja nanyi, kwamba hapatatokea kuangamizwa kwa mwenye mwili kwa njia ya maji ya gharika. Tena hapatatokea gharika ya kuangamiza nchi.”
12 Then God saide, This is the token of the couenant which I make betweene me and you, and betweene euery liuing thing, that is with you vnto perpetuall generations.
Mungu akasema, “na hii ndiyo ishara ya agano ambalo ninafanya kati yangu na ninyi pamoja na kila kiumbe hai kilicho pamoja nanyi, kwa vizazi vyote vya baadaye:
13 I haue set my bowe in the cloude, and it shalbe for a signe of the couenant betweene me and the earth.
Nimeweka upinde wangu wa mvua katika wingu, na itakuwa ndiyo ishara ya agano kati yangu na nchi.
14 And when I shall couer the earth with a cloud, and the bowe shall be seene in the cloude,
Hata itakuwa nitakapoleta wingu juu ya nchi na upinde wa mvua ukaonekana katika wingu,
15 Then will I remember my couenant, which is betweene me and you, and betweene euery liuing thing in all flesh, and there shalbe no more waters of a flood to destroy all flesh.
ndipo nitakumbuka agano langu, ambalo ni kati yangu na ninyi na kila kiumbe hai cha wote mwenye mwili. Maji hayatafanyika tena gharika kuharibu wote wenye mwili.
16 Therefore the bowe shalbe in the cloude, that I may see it, and remember the euerlasting couenant betweene God, and euery liuing thing in all flesh that is vpon the earth.
Upinde wa mvua utakuwa katika mawingu na nitauona, ili kukumbuka agano la milele kati ya Mungu na kila kiumbe hai cha wote wenye mwili ambacho kiko juu ya nchi.”
17 God said yet to Noah, This is the signe of the couenant, which I haue established betweene me and all flesh that is vpon the earth.
Kisha Mungu akamwambia Nuhu, “Hii ni ishara ya agano ambalo nimelithibitisha kati yangu na wenye mwili wote ambao wako juu ya nchi.”
18 Nowe the sonnes of Noah going foorth of the Arke, were Shem and Ham and Iapheth. And Ham is the father of Canaan.
Wana wa Nuhu ambao walitoka katika safina walikuwa ni Shemu, Hamu, na Yafethi. Na Hamu akamzaa kanaani.
19 These are the three sonnes of Noah, and of them was the whole earth ouerspred.
Watatu hawa walikuwa ndio wana wa Nuhu, na kutokea kwa hawa nchi yote ikajaa watu.
20 Noah also began to be an husband man and planted a vineyard.
Nuhu akaanza kuwa mkulima, na akapanda mizabibu.
21 And he drunke of ye wine and was drunken, and was vncouered in the middes of his tent.
Akanywa sehemu ya divai na akalewa. Akawa amelala hemeani uchi.
22 And when Ham the father of Canaan sawe the nakednesse of his father, he tolde his two brethren without.
Kisha Hamu, baba yake na Kanaani, akaona uchi wa baba yake na akawaambia ndugu zake wawili waliokuwa nje.
23 Then tooke Shem and Iapheth a garment, and put it vpon both their shoulders, and went backwarde, and couered the nakednesse of their father with their faces backwarde: so they sawe not their fathers nakednesse.
Kwa hiyo Shemu na Yafethi wakachukua kanzu wakaitanda juu ya mabega yao, na wakatembea kinyumenyume na wakaufunika uchi wa baba yao. Nyuso zao zikiwa zimegeuka nyuma upande mwingine, kwa hiyo hawakuona uchi wa baba yao.
24 Then Noah awoke from his wine, and knew what his yonger sonne had done vnto him,
Nuhu alipozinduka kutoka katika ulevi wake, alijua ni jambo gani mtoto wake mdogo amemfanyia.
25 And said, Cursed be Canaan: a seruant of seruants shall he be vnto his brethren.
Hivyo akasema, “Alaaniwe Kanaani. Na awe mtumishi kwa watumishi wa ndugu zake.”
26 He said moreouer, blessed be the Lord God of Shem, and let Canaan be his seruant.
Akasema pia, Yahwe, Mungu wa Shemu, abarikiwe, Kanaani na awe mtumwa wake.
27 God perswade Iapheth, that he may dwell in the tentes of Shem, and let Canaan be his seruant.
Mungu na apanuwe mipaka ya Yafethi, na afanye makazi yake katika hema za Shemu. Kanaani na awe mtumwa wake.”
28 And Noah liued after the flood three hundreth and fiftie yeeres.
Baada ya gharika, Nuhu aliishi miaka miatatu na hamsini.
29 So all the dayes of Noah were nine hundreth and fiftie yeeres: and he died.
Siku zote za Nuhu zilikuwa ni miaka mia tisa na hamsini, na kisha alikufa.

< Genesis 9 >