< Daniel 9 >

1 In the first yeere of Darius the sonne of Ahashuerosh, of the seede of the Medes, which was made King ouer the realme of the Caldeans,
Dario mwana wa Ahasuero, wa uzao wa Wamedi. Alikuwa na Ahasuero ambaye alifanywa mfalme juu ya ufalme wa watu wa Babeli.
2 Euen in the first yeere of his reigne, I Daniel vnderstood by bookes the nomber of the yeeres, whereof the Lord had spoken vnto Ieremiah the Prophet, that he would accomplish seuentie yeeres in the desolation of Ierusalem.
Sasa katika mwaka wa kwanza wa utawala wa Dario, mimi Danieli, nilikuwa najisomea vitabu vilivyo na neno la Yahweh, neno ambalo lilikuwa limemjia Yeremia nabii. Niligundua kwamba kungekuwa na miaka sabini hadi mwisho wa kuachwa kwa Yerusalemu ungefika.
3 And I turned my face vnto the Lord God, and sought by prayer and supplications with fasting and sackcloth and ashes.
Niliugeuza uso wangu kumwelekea Bwana Mungu, ili kumtafuta yeye kwa sala na maombi, kwa kufunga, na kuvaa nguo za magunia na kukaa katika majivu.
4 And I prayed vnto the Lord my God, and made my confession, saying, Oh Lord God, which art great and fearefull, and keepest couenant and mercy toward them which loue thee, and toward them that keepe thy commandements,
Nilimwomba Yahweh Mungu wangu, na niliungama dhambi zetu. Nilisema, “Tafadhali, Bwana, wewe ni Mungu mkuu na mwenye kuheshimiwa, wewe hutunza maagano na uliye mwaminifu katika kuwapenda wale wanaokupenda wewe na kuzishika amri zako.
5 We haue sinned, and haue committed iniquitie and haue done wickedly, yea, we haue rebelled, and haue departed from thy precepts, and from thy iudgements.
Tumetenda dhambi na tumefanya yaliyo mabaya. Tumeenenda kwa uovu na tumeasi, tumegeuka upande kinyume na amri na maagizo yako.
6 For we would not obey thy seruants the Prophets, which spake in thy Name to our Kings, to our princes, and to our fathers, and to all the people of the land.
Hatujawasikiliza watumishi wako manabii walizungumza na wafalme wetu, viongozi wetu, baba zetu, na kwa watu wote wa nchi kwa jina lako.
7 O Lord, righteousnes belongeth vnto thee, and vnto vs open shame, as appeareth this day vnto euery man of Iudah, and to the inhabitants of Ierusalem: yea, vnto all Israel, both neere and farre off, through all the countreys, whither thou hast driuen them, because of their offences, that they haue committed against thee.
Kwako Bwana, kuna uadilifu. Hata hivyo, kwetu kuna aibu katika nyuso zetu, kwa watu wa Yuda na wale wanaoishi Yerusalem, na kwa Israeli yote. Hii ni pamoja na wale walio karibu na wale walio mbali katika nchi zote ambazo kwazo uliwatawanya. Hii ni kwasababu ya udanganyifu mkubwa tulioufanya kinyume chako.
8 O Lord, vnto vs apperteineth open shame, to our Kings, to our princes, and to our fathers, because we haue sinned against thee.
Kwetu sisi, Yahweh, kuna fedheha katika nyuso, na kwa wafalme wetu, na kwa viongozi wetu, na kwa baba zetu, kwasababu tumekutenda dhambi wewe.
9 Yet compassion and forgiuenesse is in the Lord our God, albeit we haue rebelled against him.
Kwa Bwana Mungu wetu kuna huruma na msamaha, kwa kuwa tumemwasi yeye.
10 For we haue not obeyed the voyce of the Lord our God, to walke in his lawes, which he had laide before vs by the ministerie of his seruants the Prophets.
Hatujaitii sauti ya Yahweh Mungu wetu kwa kutembea katika sheria zake alizotupatia kupitia watumishi wake manabii.
11 Yea, all Israel haue transgressed thy Lawe, and are turned backe, and haue not heard thy voyce: therefore the curse is powred vpon vs, and the othe that is written in the Lawe of Moses the seruant of God, because we haue sinned against him.
Israeli wote wameiasi sheria yako na kugeukia upande, kwa kukataa kuitii sauti yako. Laana na viapo vilivyoandikwa katika sheria ya Musa, mtumishi wa Mungu, zimemwagwa juu yetu kwa kuwa tummetenda dhambi.
12 And he hath confirmed his wordes, which he spake against vs, and against our iudges that iudged vs, by bringing vpon vs a great plague: for vnder the whole heauen hath not bene the like, as hath bene brought vpon Ierusalem.
Yahweh ameyathibitisha maneno ambayo aliyasema kinyume na sisi na kinyume na viongozi wetu juu yetu, kwa kuleta juu yetu janga kubwa. Kwa kuwa chini ya mbingu yote haijawahi kufanyika kitu chochote ambacho kinaweza kulinganishwa na kile kilichofanyika huko Yerusalemu.
13 All this plague is come vpon vs, as it is written in the Lawe of Moses: yet made we not our prayer before the Lord our God, that we might turne from our iniquities and vnderstand thy trueth.
Kama ilivyoandikwa kwenye sheria ya Musa, baa hili lote limetupata, ingawa bado hatujaomba rehema kutoka kwa Yahweh Mungu wetu kwa kugeuka na kuacha maovu yetu na kuufuata ukweli wako.
14 Therefore hath the Lord made ready the plague, and brought it vpon vs: for the Lord our God is righteous in all his works which he doeth: for we would not heare his voyce.
Hivyo basi, Yahweh ameyaweka tayari maafa na ameyaleta juu yetu, kwa kuwa Yahweh Mungu wetu ni mwenye haki katika matendo yote anayoyafanya, ingawa bado hatujaitii sauti yake.
15 And nowe, O Lord our God, that hast brought thy people out of the land of Egypt with a mightie hand, and hast gotten thee renoume, as appeareth this day, we haue sinned, we haue done wickedly.
Basi sasa, Bwana Mungu wetu, uliwatoa watu wako katika nchi ya Misri kwa mkono wenye nguvu, na umejifanyia jina maarufu kwa ajli yako mwenyewe, hata siku hii ya leo. Lakini bado tumekutenda dhambi; tumefanya mambo ya hila. Kwasababu ya matendo yako yote ya haki,
16 O Lord, according to all thy righteousnes, I beseech thee, let thine anger and thy wrath be turned away from thy citie Ierusalem thine holy Mountaine: for because of our sinnes, and for the iniquities of our fathers, Ierusalem and thy people are a reproche to all that are about vs.
Bwana, iache hasira na ghadhabu yako iwe mbali na mji wako Yerusalemu, mlima wako mtakatifu. Hii ni kwasababu ya dhambi zetu, na kwasababu ya uovu wa baba zetu, Yerusalemu na watu wako wamekuwa kitu cha kudharauliwa na wote wanaotuzunguka.
17 Nowe therefore, O our God, heare the prayer of thy serunant, and his supplications, and cause thy face to shine vpon thy Sanctuarie, that lyeth waste for the Lords sake.
Basi sasa, Mungu wetu, sikiliza sala za mtumishi wako na maombi yake kwa ajili ya rehema; kwa ajili yako, Bwana ufanye uso wako ung'ae katika sehemu yako takatifu iliyoachwa ukiwa.
18 O my God, encline thine eare and heare: open thine eyes, and beholde our desolations, and the citie whereupon thy Name is called: for we doe not present our supplications before thee for our owne righteousnes, but for thy great tender mercies.
Mungu wangu, fungua masikio yako na usikie; fumbua macho yako na uone. Tumeharibiwa; utazame mji unaoitwa kwa jina lako. Hatukuombi msaada wako kwasababu ya haki yetu, ila kwasababu ya rehema zako kuu.
19 O Lord, heare, O Lord forgiue, O Lord consider, and doe it: deferre not, for thine owne sake, O my God: for thy Name is called vpon thy citie, and vpon thy people.
Bwana, sikiliza! Bwana, samehe! Bwana, tuangalie na ufanye jambo! Kwa ajili yako mwenyewe, usichelewe, Mungu wangu, kwa kuwa mji wako na watu wako wanaitwa kwa jina lako.”
20 And whiles I was speaking and praying, and confessing my sinne, and the sinne of my people Israel, and did present my supplication before the Lord my God, for the holy Mountaine of my God,
Nilipokuwa ninaongea kwa kuomba na kuungama dhambi yangu na dhambi ya watu wangu Israeli, na kuwasilisha maombi yangu mbele ya Yahweh Mungu wangu kwa niaba ya mlima mtakatifu wa Mungu.
21 Yea, while I was speaking in prayer, euen the man Gabriel, whome I had seene before in the vision, came flying, and touched mee about the time of the euening oblation.
Nilipokuwa ninaomba, mtu Gabrieli, ambaye nilikuwa nimemwona katika ndoto hapo awali, alipaa kwa kasi kushuka kuja nilipo, ilikuwa ni wakati wa sadaka ya jioni.
22 And he informed me, and talked with me, and sayd, O Daniel, I am now come forth to giue thee knowledge and vnderstanding.
Alinipa ufahamu na aliniambia, “Danieli, nimekuja sasa ili nikupe utambuzi na ufahamu.
23 At the beginning of thy supplications the commandement came foorth, and I am come to shewe thee, for thou art greatly beloued: therefore vnderstande the matter and consider the vision.
Ulipoanza kuomba rehema, amri ilitolewa na nimekuja kukueleza jibu, kwa kuwa unapendwa sana. Hivyo basi, tafakari neno hili na uufahamu ufunuo.
24 Seuentie weekes are determined vpon thy people and vpon thine holy citie, to finish the wickednes, and to seale vp the sinnes, and to reconcile the inquitie, and to bring in euerlasting righteousnesse, and to seale vp the vision and prophecie, and to anoynt the most Holy.
Miaka sabini na saba zimeamriwa kwa ajili ya watu wako na mji wako mtakatifu kukomesha hatia na kumaliza dhambi, na kuleta haki ya milele, na kutimiza maono na unabii, na kupaweka wakfu mahali patakatifu sana.
25 Knowe therefore and vnderstande, that from the going foorth of the commandement to bring againe the people, and to builde Ierusalem, vnto Messiah the prince, shall be seuen weekes and threescore and two weekes, and the streete shalbe built againe, and the wall euen in a troublous time.
Ujue na kufahamu kuwa tangu kupitishwa kwa amri ya kurudi na kuijenga upya Yerusalemu mpaka ujio wa mpakwa mafuta (atakayekuwa kiongozi), kutakuwa na majuma saba na majuma sitini na mbili. Yerusalemu itajengwa pamoja na mitaa yake na handaki, licha ya kuwepo kwa nyakati za shida
26 And after threescore and two weekes, shall Messiah be slaine, and shall haue nothing, and the people of the prince that shall come, shall destroy the citie and the Sanctuarie, and the end thereof shalbe with a flood: and vnto the end of the battell it shalbe destroyed by desolations.
Baada ya miaka ya majuma sitini na mbili, mtiwa mafuta ataharibiwa na atakuwa hana kitu chochote. Jeshi la kiongozi ajaye litauangamiza mji na mahali patakatifu. Mwisho wake utatatokea kwa gharika, na kutakuwa na vita hata mwisho. Uharibifu umekwisha amriwa.
27 And he shall confirme the couenant with many for one weeke: and in the middes of the weeke he shall cause the sacrifice and the oblation to cease, and for the ouerspreading of the abominations, he shall make it desolate, euen vntill the consummation determined shalbe powred vpon the desolate.
Atalithibitisha agano pamoja na watu wengi kwa miaka saba. Katikati ya miaka saba atakomesha dhabihu na sadaka. Baada ya chukizo la uharibifu atatokea mtu atakayeleta ukiwa. Mwisho kamili na uharibifu umeamriwa kutokea kwa yeye aliyesababisha ukiwa.”

< Daniel 9 >