< Daniel 10 >

1 In the third yeere of Cyrus King of Persia, a thing was reueiled vnto Daniel (whose name was called Belteshazzar) and the worde was true, but the time appointed was long, and he vnderstood the thing, and had vnderstanding of the vision.
Katika mwaka wa tatu wa Koreshi mfalme wa Uajemi, ujumbe ulifunuliwa kwa Danieli, aliyeitwa pia Belteshaza. Ujumbe huu ulikuwa ni wa kwelil. Ulihusu vita kuu. Danieli aliufahamu ujumbe alipopata ufumbuzi kutoka katika maono.
2 At the same time I Daniel was in heauines for three weekes of dayes.
Katika siku hizo, mimi Danieli, nilikuwa katika maombolezo kwa wiki tatu.
3 I ate no pleasant bread, neither came flesh nor wine in my mouth, neither did I anoint my selfe at all, till three weekes of dayes were fulfilled.
Sikula chakula kizuri, sikula nyama, sikunywa divai, na sikujipaka mafuta mwenyewe mpaka ukamilifu wa wiki tatu nzima.
4 And in the foure and twentieth day of the first moneth, as I was by the side of that great riuer, euen Hiddekel,
Katika siku ya ishirini na nne ya mwezi wa kwanza, nilipokuwa niko karibu na mto mkubwa (ambao ni Tigrisi),
5 And I lift vp mine eyes, and looked, and beholde, there was a man clothed in linnen, whose loynes were girded with fine golde of Vphaz.
Nilitazama juu na nikamwona mtu aliyevaa kitani, akiwa na mkanda kiunoni mwake uliotengenezwa kwa dhahabu safi kutoka Ufazi.
6 His body also was like the Chrysolite, and his face (to looke vpon) like the lightning, and his eyes as lamps of fire, and his armes and his feete were like in colour to polished brasse, and the voyce of his wordes was like the voyce of a multitude.
Mwili wake ulikuwa kama kito, na sura yake ilikuwa kama radi. Macho yake yalikuwa kama miali ya tochi, na mikono yake na miguu yake ilikuwa kama shaba iliyosafishwa. Sauti ya maneno yake ilikuwa kama sauti ya umati mkubwa wa watu.
7 And I Daniel alone sawe the vision: for the men that were with me, sawe not the vision: but a great feare fell vpon them, so that they fled away and hid themselues.
Mimi, Danieli peke yangu niliyaona maono, na watu niliokuwa na pamoja hawakuyaona maono. Lakini, jambo kuu la kuogofya liliwaijia juu yao, na walikimbia na kujificha wao wenyewe.
8 Therefore I was left alone, and sawe this great vision, and there remained no strength in me: for my strength was turned in me into corruption, and I reteined no power.
Hivyo niliachwa peke yangu na niliyaona maono haya ajabu. Hakuna nguvu iliyobakia ndani yangu; mwonekano wangu wa kung'aa ulibadilika na kuwa mwonekano wa uharibifu, na hazikubakia nguvu ndani yangu.
9 Yet heard I the voyce of his wordes: and when I heard the voyce of his wordes, I slept on my face: and my face was toward the ground.
Kisha nikasikia maneno yake, na nilipoyasikia, nilianguka kifudifudi na kupata usingizi mzito.
10 And behold, an hand touched me, which set me vp vpon my knees and vpon the palmes of mine hands.
Mkono ulinigusa, na ilinifanya nitetemeke katika magoti yangu na viganja vya mikono yangu.
11 And he sayde vnto me, O Daniel, a man greatly beloued, vnderstand the wordes that I speake vnto thee, and stand in thy place: for vnto thee am I nowe sent. And when hee had sayde this worde vnto me, I stood trembling.
Malaika aliniambia, “Danieli, mtu aliyetunzwa sana, yafahamu maneno ninayokwambia wewe. Simama wima, kwa kuwa nimeshakutuma.” Na alipomaliza kuniambia ujumbe huu, nilisimama nikiwa natetemeka.
12 Then sayd he vnto me, Feare not, Daniel: for from the first day that thou diddest set thine heart to vnderstand, and to humble thy selfe before thy God, thy wordes were heard, and I am come for thy wordes.
Kisha aliniambia, “Usiogope, Danieli. Tangu siku ya kwanza ulipoiweka akili yako kutaka kufahamu na kujinyenyekeza mwenyewe mbele ya Mungu, maneno yako yalisikiwa, na nimekuja kwasababu ya maneno yako.
13 But the prince of the kingdome of Persia withstoode me one and twentie dayes: but loe, Michael one of the chiefe princes, came to helpe me, and I remained there by the Kings of Persia.
Mwana wa mfalme wa ufalme wa Uajemi alinizuia, na niliwekwa huko na mfalme wa Uajemi kwa siku ishirini na moja. Lakini Mikaeli, mmoja kati ya wakuu alikuja kunisaidia.
14 Nowe I am come to shewe thee what shall come to thy people in the latter dayes: for yet the vision is for many dayes.
Sasa nimekuja kukusaidia ili ufahamu kile kitakachotokea kwa watu wako katika siku za mwisho. Kwa kuwa maono ni kwa ajili siku ambazo hazijatokea bado.
15 And when he spake these wordes vnto me, I set my face towarde the grounde, and helde my tongue.
Na alipokuwa akali akiniambia maneno haya, niligeuza uso wangu na kuuelekeza chini na sikuwa na uwezo wa kuzungumza.
16 And beholde, one like the similitude of the sonnes of man touched my lippes: then I opened my mouth, and spake, and said vnto him that stoode before me, O my Lord, by the vision my sorowes are returned vpon me, and I haue reteined no strength.
Yeye aliyekuwa kama wana wa mtu alinigusa mdomo wangu na nifumbua kinywa changu na nilimwambia huyo aliyekuwa amesimam mbele yangu: “Bwana wangu, niko katika masumbuko makali kwasababu ya maono; sina nguvu ndani yangu iliyosalia.
17 For howe can the seruant of this my Lord talke with my Lord being such one? for as for me, straight way there remained no strength in me, neither is there breath left in me.
Mimi ni mtumishi wako. Je ninawezaje kuongea na Bwana wangu? Kwa kuwa sasa sina nguvu, na hakuna pumzi iliyosalia ndani yangu.”
18 Then there came againe, and touched me one like the appearance of a man, and he strengthened me,
Tena yule mwenye mwonekano wa mtu alinigusa na kunitia nguvu.
19 And said, O man, greatly beloued, feare not: peace be vnto thee: be strong and of good courage. And when he had spoken vnto me, I was strengthened, and saide, Let my Lord speake: for thou hast strengthened me.
Alisema, “Usiogope, mtu ulithaminiwa sana. Amani na iwe kwako! Uwe mwenye nguvu, uwe na nguvu!” Na alipokuwa anaongea na mimi, nilipata nguvu. Nilimwambia, “Bwana wangu na aseme, kwa kuwa umenitia nguvu.”
20 Then saide he, Knowest thou wherefore I am come vnto thee? but nowe will I returne to fight with the prince of Persia: and when I am gone forth, loe, the prince of Grecia shall come.
Aliniambia, “Je unajua ni kwanini nimekuja kwako? Nitarudi hivi karibuni kupigana na mkuu wa Uajemi. Na nitakapoenda, mkuu wa Ugiriki atakuja.
21 But I will shew thee that which is decreeed in the Scripture of trueth: and there is none that holdeth with me in these things, but Michael your prince.
Lakini nitakwambia kile kilichoandikwa katika Kitabu cha Ukweli. Hakuna yeyote anayejionesha kuwa na nguvu pamoja nami dhidi yao, isipokuwa Mikaeli mkuu wenu.”

< Daniel 10 >