< 2 Kings 4 >

1 And one of the wiues of the sonnes of the Prophets cryed vnto Elisha, saying, Thy seruant mine husband is dead, and thou knowest, that thy seruant did feare the Lord: and the creditour is come to take my two sonnes to bee his bondmen.
Ndipo mke wa mmoja wa watoto wa manbii alipokuja kwa Elisha akilia, akisema, “Mtumishi wako mme wangu amukufa, na unajua kwamba mtumishi wako alikuwa anamcha Yahwe. Basi aliyemuwia amekuja kuwachukua watoto wangu wawili kwenda kuwa watumwa.”
2 Then Elisha saide vnto her, What shall I do for thee? tell mee, what hast thou at home? And she sayd, Thine handmayd hath nothing at home, saue a pitcher of oyle.
Hivyo Elisha akamwambia, “Nikusaidie nini? Niambie una nini kwenye nyumba yako?” Akamwambia “Mtumishi wako hana kitu kwenye nyumba, isipokuwa chupa ya mafuta.”
3 And he sayde, Goe, and borowe thee vessels abroad of all thy neighbours, emptie vessels, and spare not.
Kisha Elisha akasema, “Nenda kaazime vyombo kwa majirani zako, vyombo vitupu. Azima vyombo vingi uwezavyo.
4 And when thou art come in, thou shalt shut the doore vpon thee and vpon thy sonnes, and powre out into all those vessels, and set aside those that are full.
Kisha lazima uende ndani na kujifungia mlango wewe na watoto wako, na kumiminia mafuta vyombo vyote; vile vilivyojaa ukavitenge.”
5 So shee departed from him, and shut the doore vpon her, and vpon her sonnes. And they brought to her, and she powred out.
Basi akamuacha Elisha na kujifungia mlango yeye na watoto wake. Wakavileta vile vyombo kwake, na akivijaza kwa mafuta.
6 And when the vessels were full, shee sayde vnto her sonne, Bring mee yet a vessel. And hee said vnto her, There is no moe vessels. And the oyle ceased.
Ikawa vyombo vilipojaa, akamwambia mtoto wake, “Niletee chombo kingine.” Ila akamwambia, “Hakuna vyombo vingine.” Kisha mafuta yakakoma kutoka.
7 Then shee came and tolde the man of God. And he saide, Goe, and sell the oyle, and pay them that thou art in debt vnto, and liue thou and thy children of the rest.
Ndipo akaja na kumwambia mtu wa Mungu. Akasema, “Nenda kauze mafuta; lipa deni lako, na yatakayobaki waachie watoto wako.”
8 And on a time Elisha came to Shunem, and there a woman of great estimation constrained him to eate bread: and as he passed by, he turned in thither to eate bread.
Siku moja Elisha alitembea Shunemu ambapo mwanamke muhimu aliishi; alimsihi ale chakula pamoja naye. Ikawa alipopita mara nyingi, angeweza kusimama pale na kula.
9 And she sayde vnto her husband, Beholde, I know now, that this is an holy man of God that passeth by vs continually.
Huyo mwanamke akamwambia mme wake, “Ona, sasa nadhani kwamba huyu ni mtu mtakatifu wa Mungu ambaye hupita siku zote.
10 Let vs make him a litle chamber, I pray thee, with walles, and let vs set him there a bed, and a table, and a stoole, and a candlesticke, that hee may turne in thither when hee commeth to vs.
Ngoja tutengeneze chumba kidogo kwenye paa kwa ajili ya Elisha, na tuweke kitanda juu ya hicho chumba, meza, na taa. Kisha atakapokuwa anakuja kwetu, atakuwa anakaa hapo.”
11 And on a day, hee came thither and turned into the chamber, and lay therein,
Ikawa siku moja akaja tena kwamba Elisha akasimama pale, akakaa kwenye hicho chumba na kupumzika hapo.
12 And sayd to Gehazi his seruant, Call this Shunammite: and when hee called her, she stood before him.
Elisha akamwambia Gehazi mtumishi wake, “Mwite huyu Mshunami.” Wakati alipomuita, alisimama mbele yake.
13 Then he sayd vnto him, Say vnto her now, Beholde, thou hast had all this great care for vs, what shall we doe for thee? Is there any thing to bee spoken for thee to the King or to the captaine of the hoste? And shee answered, I dwell among mine owne people.
Elisha akamwambia, “Mwambie, 'Umetusumbukia kwa kutujali. Nini kifanyike kwa ajili yako? Tunaweza kukuombea kwa mfalme au amri jeshi?”” Akajibu, “Ninaishi miongoni mwa watu wangu.”
14 Againe he sayde, What is then to be done for her? Then Gehazi answered, In deede she hath no sonne, and her husband is olde.
Kisha Elisha akajibu, “Tumfanyie nini kwa ajili yake, sasa?” Gehazi akajibu, “Kweli hana mtoto, na mume wake ni
15 Then said he, Cal her. And hee called her, and shee stoode in the doore.
mzee.” Hivyo Elisha akajibu, “Mwite.” Wakati alipomuita, akasimama kwenye mlango.
16 And he said, At this time appointed, according to the time of life, thou shalt embrace a sonne. And she sayd, Oh my Lord, thou man of God, doe not lye vnto thine handmayd.
Elisha akasema, “Katika kipindi kama hiki mwakani, katika kipindi cha mwaka mmoja, utakuwa ukimkumbatia mtoto.” Akasema “Hapana, bwana wangu na mtu wa Mungu, usidanganye kwa mtumishi wako.”
17 So the woman conceiued, and bare a sonne at that same season, according to the time of life, that Elisha had sayd vnto her.
Lakini yule mwanamke akabeba mimba na kujifungua mtoto wakume kipindi hicho hicho katika mwaka uliofuata, kama Elisha alivyokuwa amemwambia.
18 And when the childe was growen, it fell on a day, that he went out to his father, and to the reapers.
Wakati mtoto alipokuwa mkubwa, akaenda kwa baba yake siku moja, ambaye alikuwa na watu wanaovuna.
19 And he sayde to his father, Mine head, mine head. Who sayd to his seruant, Beare him to his mother.
Akamwambia baba yake, “Kichwa changu, kichwa changu.” Baba yake akamwambia mtumishi wake, “Mbebe mpeleke kwa mama yake.”
20 And hee tooke him and brought him to his mother, and hee sate on her knees till noone, and dyed.
Wakati mtumishi alipombeba kumrudisha kwa mama yake, yule mtoto alikaa kwenye magoti yake hadi mchana na baada ya hapo mtoto alikufa.
21 Then shee went vp, and layed him on the bed of the man of God, and shut the doore vpon him, and went out.
Hivyo yule mwanamke akambeba na kumlaza kwenye kile kitanda cha mtu wa Mungu, akafunga mlango, na kutoka nje.
22 Then she called to her husband, and sayd, Send with me, I pray thee, one of the yong men and one of the asses: for I will haste to the man of God, and come againe.
Akamwita mume wake, na kusema, “Tafadhali nitumie mmoja wa watumishi wako na moja ya punda wako ili niweze kuwahi kwa mtu wa Mungu ili niweze kurudi.”
23 And he sayd, Wherefore wilt thou goe to him to day? it is neither newe moone nor Sabbath day. And she answered, All shalbe well.
Mume wake akasema, “Kwa nini unataka kwenda kwake leo? Sio mwezi mpya wala Sabato.” alijibu, “Itakuwa sawa.”
24 Then she sadled an asse, and sayde to her seruant, Driue, and goe forward: staye not for me to get vp, except I bid thee.
Ndipo akatandika kwenye punda na kumwambia mtumishi wake, “Mwendeshe haraka; usinipunguzie mwendo hadi nitakapokwambia ufanye hivyo.”
25 So she went, and came vnto the man of God to mount Carmel. And when the man of God sawe her ouer against him, he sayd to Gehazi his seruant, Beholde, the Shunammite.
Hivyo alienda na kuja na mtu wa Mungu katika mlima Karmeli. Basi wakati mtu wa Mungu alipomuona kwa mbali, akamwambia Gehazi mtumishi wake, “Tazama, mwanamke Mshunami anakuja.
26 Runne nowe, I say, to meete her, and say vnto her, Art thou in health? is thine husband in health? and is the child in health? And she answered, We are in health.
Tafadhali mkimbilie na umwambie, 'Hamjambo kwako pamoja na mume wako na mtoto wako?” Akajibu, “Hawajambo.”
27 And when shee came to the man of God vnto the moutaine, she caught him by his feete: and Gehazi went to her, to thrust her away: but the man of God said, Let her alone: for her soule is vexed within her, and the Lord hath hid it from me, and hath not told it mee.
Baada ya kufika kwa huyo mtu wa Mungu katika mlima, alimkumbatia miguu yake. Gehazi akaja karibu ili kumuondoa lakini mtu wa Mungu akasema, “Muache, kwa kuwa amefadhaika sana. na Yahwe amenificha tatizo kwangu, na hajanambia kitu.”
28 Then she said, Did I desire a sonne of my lord? did I not say, Deceiue me not?
Ndipo aksema, “Nilikuuliza mtoto wako, bwana wangu? Sikusema, 'Usinifiche'?
29 Then he sayd to Gehazi, Gird thy loynes, and take my staffe in thine hand, and goe thy way: if thou meete any, salute him not: and if any salute thee, answere him not: and laye my staffe vpon the face of the childe.
Ndipo Elisha akamwambia Geahazi, “Vaa kwa ajili ya safari na uchukue fimbo yangu mkononi mwako. Nenda kwake. Kama ukimkuta mtu yeyote, usimsalimie, na kama mtu yeyote akikusalimia, usimjibu. Laza fimbo yangu kwenye uso wa mtoto.
30 And the mother of the childe sayde, As the Lord liueth, and as thy soule liueth, I will not leaue thee. Therefore he arose, and followed her.
Lakini mama yake na huyo mtoto akasema, “Kama Yahwe aishivyo, na kama uishivyo, sintokuacha.” Hivyo Elisha akainuka na kumfuata.
31 But Gehazi was gone before them, and had layed the staffe vpon the face of the childe, but he neither spake nor heard: wherefore hee returned to meete him, and told him, saying, The childe is not waken.
Gehazi akawatangulia na kulaza ile fimbo kwneye uso wa yule mtoto, lakini yule mtoto hakuongea wala kusikia. Hivyo baada ya hapo Gehazi akarudi kuonana na Elisha na kumwambia akisema, “Mtoto hakuamka.”
32 Then came Elisha into the house, and beholde, the childe was dead, and layed vpon his bedde.
Ndipo Elisha alipofika kwenye ile nyumba, yule mtoto alikuwa amekufa na alikuwa bado yupo kwenye kitanda.
33 He went in therefore, and shut the doore vpon them twayne, and prayed vnto the Lord.
Hivyo Elisha aliingia ndani na kufunga malango yeye mwenyewe na yule mtoto na kuomba kwa Yahwe.
34 After he went vp, and lay vpon the child, and put his mouth on his mouth, and his eyes vpon his eies, and his hands vpon his handes, and stretched himselfe vpon him, and the flesh of the child waxed warme.
Alipanda juu na kulala juu ya yule mtoto; aliweka mdomo wake kwenye mdomo wake, macho yake kweneye macho yake, na mikono yake kwenye mikono yake. Akajinyoosha yeye mwenyewe kwa yule kijna, na mwili wa yule mtoto ukaanza kupata joto.
35 And hee went from him, and walked vp and downe in the house, and went vp and spred himselfe vpon him: then the childe neesed seuen times, and opened his eyes.
Baada ya hapo Elisha aliinuka na kuanza kutembea kuzunguka kile chumba na kurudi tena juu na kujinyoosha mwenyewe kwa yule kijana. Yule kijana alipiga chafya mara saba na kisha akafungua macho yake!
36 Then he called Gehazi, and sayd, Call this Shunammite. So he called her, which came in vnto him. And he said vnto her, Take thy sonne.
Hivyo Elisha akamwita Gehazi na kumwambia, “Mwite yule Mshunami!” Hivyo akamwita, na wakati alipofika kwenye kile chumba, Elisha akasema, “Mchukue mtoto wako.”
37 And she came, and fell at his feete, and bowed her selfe to the ground, and tooke vp her sonne, and went out.
Kisha akainamisha uso wake chini kwenye miguu yake na kusujudu, na kisha kumchukua mtoto wake na kuondoka.
38 Afterward Elisha returned to Gilgal, and a famine was in the land, and the children of the Prophets dwelt with him. And hee sayd vnto his seruant, Set on the great pot, and seethe pottage for the children of the Prophets.
Kisha Elisha akarudi tena Gilgali. Kulikuwa na njaa katika nchi, na wana wa manabii walikuwa wamekaa mbele yake. Akamwambia mtumishi wake, “Weka sufuria kubwa kwenye moto na pika kwa ajili ya watoto wa manabii.”
39 And one went out into the fielde, to gather herbes, and founde, as it were, a wilde vine, and gathered thereof wilde gourdes his garment ful, and came and shred them into the pot of pottage: for they knew it not.
Mmoja wao akaenda kwenye shamba kukusanya mboga mboga. Alikuta matango ya porini na kukusanya ya kutosha hadi alipojaza kwenye nguo yake. Walizikata na kuziweka kwenye sufuria, lakini hakujua zilikuwa za aina gani.
40 So they powred out for the men to eate: and when they did eate of the pottage, they cryed out, and sayde, O thou man of God, death is in the pot: and they could not eate thereof.
Basi, wakawapakulia na kusambaziwa kwa watu kwa ajili ya kula. Baadae, kadiri walivyokuwa wakiendelea kula, walipiga kelele na kusema, “Mtu wa Mungu, kuna kifo kwenye sufuria!” Hivyo wasingeweza kula tena.
41 Then he said, Bring meale. And hee cast it into the potte, and sayd, Powre out for the people, that they may eate: and there was none euill in the pot.
Lakini Elisha akasema, “Late unga.” Alitupia kwenye sufuria na kusema, “Pakua kwa watu kwa ajili ya kula, kwa hiyo wanaweza kula.” Kisha hapakuwa kitu chochote kibaya kwenye ile sufuria.
42 Then came a man from Baal-shalisha, and brought the man of God bread of the first fruits, euen twenty loaues of barley, and full eares of corne in the huske. And hee saide, Giue vnto the people, that they may eate.
Akaja mtu kutoka Baal Shalisha kwa mtu wa Mungu na kumletea chakula cha kwanza cha mavuno yake mikate shirirni ya shayiri, na masuke mabichi kwenye gunia. Akasema, “Wape haya watu ili waweze kula.”
43 And his seruant answered, How shoulde I set this before an hundreth men? He sayd againe, Giue it vnto the people, that they may eate: for thus sayth the Lord, They shall eate, and there shall remaine.
Mtumishi wake akasema, “Je, niandae hii mbele ya watu mia moja?” Lakini Elisha akasema, “Wapeni hawa watu, ili waweze kula, kwa sabau Yahwe anasema, 'Watakula na kingine kitabaki.”'
44 So he set it before them, and they did eate, and left ouer, according to the word of the Lord.
Basi mtumishi wake akawaandalia mbele yao; wakala, na kuacha kingine kimebaki, kama neno la Yahwe lilivyokuwa limesema.

< 2 Kings 4 >