< 2 Kings 3 >

1 Nowe Iehoram the sonne of Ahab beganne to reigne ouer Israel in Samaria, the eighteenth yeere of Iehoshaphat King of Iudah, and reigned twelue yeeres.
Basi katika mwaka wa kumi na nane wa Yehoshefati mfalme wa Yuda, Yoramu mwana wa Ahabu alianza kutawala juu ta Israeli katika Samaria; alitawala miaka kumi na miwili.
2 And he wrought euill in the sight of the Lord, but not like his father nor like his mother: for he tooke away the image of Baal that his father had made.
Alifanya yaliyo maovo usoni kwa Yahwe, lakini si kama baba yake na mama yake; kwa kuwa aliiondoa ile nguzo ya mungu wa Baali ambayo baba yake aliitengeneza.
3 Neuerthelesse, he cleaued vnto the sinnes of Ieroboam, the sonne of Nebat, which made Israel to sinne, and departed not therefrom.
Hata hivyo alishikilia dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambaye alisababisha Israeli kufanya dhambi; wala hakuziacha mbali nao.
4 Then Mesha King of Moab had store of sheepe, and rendred vnto the King of Israel an hundreth thousande lambes, and an hundreth thousande rammes with the wooll.
Basi Mesha mfalme wa Moabu alifuga kondoo. Alikuwa akimpatia mfalme wa Israeli kondoo 100, 000 na manyoya ya kondoo dume 100, 000.
5 But when Ahab was dead, the king of Moab rebelled against the King of Israel.
Ila baada ya Ahabu kufa, yule mfalme wa Moabu aliasi dhidi ya mfalme wa Israeli.
6 Therefore King Iehoram went out of Samaria the same season, and nombred all Israel,
Hivyo Mfalme Joramu alikaondoka Samaria katika muda huo kuwahamasisha Waisraeli wote kwa ajili ya vita.
7 And went, and sent to Iehoshaphat King of Iudah, saying, The King of Moab hath rebelled against me: wilt thou goe with me to battell against Moab? And he answered, I will goe vp: for I am, as thou art, my people, as thy people, and mine horses as thine horses.
Akatuma mjumbe kwa Yehoshafati mfalme wa Yuda, akisema, “Mfalme wa Moabu ameasi dhidi yangu. Je mtakwenda pamoja nami kupigana dhidi ya Moabu?” Yehoshafati akajibu, “Nitaenda. Mimi ni kama wewe, watu wangu ni kama watu wako, farasi wangu ni kama farasi wako.”
8 Then said he, What way shall we goe vp? And he answered, The way of the wildernesse of Edom.
Ndipo akasema, “Tutawashambulia kwa njia gani?” Yehoshafati akajibu, “Kwa njia ya jangwa la Edemu.
9 So went the King of Israel and the king of Iudah, and the King of Edom, and when they had compassed the way seuen dayes, they had no water for the hoste, nor for the cattell that followed them.
Hivyo huyo mfalme wa Israeli, Yuda, na Edomu wakazunguka kwa mda wa siku saba. Hapakuwa na maji kwa ajili ya jeshi lao, wala kwa farasi au wanyama.
10 Therefore the King of Israel sayde, Alas, that the Lord hath called these three Kings, to giue them into the hand of Moab.
Basi mfalme wa Israeli akasema, “Hii ni nini? Yahwe amewaita wafalme watatu ili kutekwa mikononi mwa Moabu?”
11 But Iehoshaphat saide, Is there not here a Prophet of the Lord, that we may inquire of the Lord by him? And one of the King of Israels seruants answered, and said, Here is Elisha the sonne of Shaphat, which powred water on the handes of Eliiah.
Lakini Yehoshafati akasema, “je hakuna nabii wa Yahwe, ambaye tunaweza kufanya shauri kuhusu Yahwe kupitia yeye?” Mtumishi mmoja wa wafalme wa Israeli akajibu na kusema, “Elisha mwana wa Shafati yuko hapa, ambaye alikuwa akimimina maji kwenye mikono ya Eliya.”
12 Then Iehoshaphat saide, The worde of the Lord is with him. Therefore the King of Israel, and Iehoshaphat, and the King of Edom went downe to him.
Yehoshafati akasema, “Neno la Yahwe liko pamoja nami.” Hivyo mfalme wa Israeli, Yehoshaphati, na mfalme wa Edomu wakashuka chini kwenda kwake.
13 And Elisha sayde vnto the King of Israel, What haue I to doe with thee? get thee to the prophets of thy father and to the prophets of thy mother. And the King of Israel saide vnto him, Nay: for the Lord hath called these three Kings, to giue them into the hande of Moab.
Elisha akamwambia mfalme wa Israeli, “Nifanye nini kwa ajili yako? Nenda kwa manabii wa baba na mama yako.” Ndipo mfalme wa Israeli akamwambia, “Hapana, kwa sababu Yahwe amewaita hawa wafalme watatu pamoja ili kuruhusu jeshi la Moabu liwateke.”
14 Then Elisha said, As the Lord of hostes liueth, in whose sight I stande, if it were not, that I regarde the presence of Iehoshaphat the King of Iudah, I woulde not haue looked towarde thee, nor seene thee.
Elisha akajibu, “Kama Yawhe wa majeshi aishivo, ambaye nimesimama mbele zake, hakika kama nisingemheshimu uwepo wa Yehoshafati mfalme wa Yeda, Nisingevuta usikivu kwako, au hata kukutazama.
15 But nowe bring me a minstrel. And when the minstrel played, the hand of the Lord came vpon him.
Lakini sasa niletee mwanamuziki.” Ndipo alipokuja mpiga muziki alipocheza, mkono wa Yahwe ukaja juu ya Elisha.
16 And he saide, Thus saith the Lord, Make this valley full of ditches.
Akasema, “'Yahwe asema hivi, 'Fanya hili bonde la mto mkavu lijae mahandaki.'
17 For thus saith the Lord, Ye shall neither see winde nor see raine, yet the valley shalbe filled with water, that ye may drinke, both ye and your cattel, and your beastes.
Kwa kuwa Yahwe asema hivi, 'Hutaona upepo, wala hamtaona mvua, bali hili bonde la mto litajaa maji, na mtakunywa, ninyi na mifugo yenu na wanyama wenu wote.'
18 But this is a small thing in the sight of the Lord: for he will giue Moab into your hande.
Hiki ni kitu rahisi usoni mwa Yahwe. Pia atawapa ushindi juu ya hao Wamoabu.
19 And ye shall smite euery strong towne and euery chiefe citie, and shall fell euery faire tree, and shall stoppe all the fountaines of water, and marre euery good fielde with stones.
Mtaiteka kila ngome ya mji na kila mji mzuri, kukata kila mti mzuri, kusimamisha chemichemi zote za maji, na kuharibu kila sehemu nzuri ya nchi na miamba.”
20 And in the morning whe the meat offring was offred, beholde, there came water by the way of Edom: and the countrey was filled with water.
Hivyo asubuhi karibia na mda wa kutoa sadaka ya kuteketeza, yakaja maji kutoka uelekeo wa Edomu; nchi ikajaa maji.
21 And when al the Moabites heard that the Kings were come vp to fight against them, they gathered all that was able to put on harnesse, and vpwarde, and stood in their border.
Ndipo wakati Wamoabu wote waliposikia kwamba wafalme wamekuja kupigana dhidi yao, walikusanyika pamoja, wote waliotakiwa kubeba silaha, na wakasimama mpakani.
22 And they rose earely in the morning, when the sunne arose vpon the water, and the Moabites saw the water ouer against them, as red as blood.
Walitembea asubuhi na mapema na jua likang'aa kwenye maji. Wakati Wamoabu walipoyaona yale maji yaliyowaelekea, yanaonekana mekundu kama damu.
23 And they saide, This is blood the Kings are surely slaine, and one hath smitten another: now therefore, Moab, to the spoyle.
Wakatamka kwa hasira, “Hii ni damu! Yamkini hao wafalme wameharibiwa, na wameuna wao kwa wao! Sasa basi, Moabu, ngoja tuende tukawateke nyara!”
24 And when they came to the host of Israel, the Israelites arose vp, and smote the Moabites, so that they fled before them, but they inuaded them, and smote Moab.
Wakati walipokuja kwenye kambi ya Israeli, Waisraeli wakawashtukiza na kuwashambulia Wamoabi, ambao walikimbia mbele yao. Hilo jeshi la Israeli waliwakimbiza hao Wamoabu hadi kwao wakiwaua.
25 And they destroyed the cities: and on all the good field euery man cast his stone, and filled them and they stopt all the fountaines of water, and felled all the good trees: onely in Kirharaseth left they the stones thereof: howebeit they went about it with slings, and smote it.
Waliiharibu miji, na kila aina ya amani ya nchi kila mtu alirusha jiwe mpaka ulipojaa. Walizuia kila chemichemi ya maji na kukata chini miti mizuri yote. Kir-haresethi tu ndiyo ilichwa na mawe yake. Lakini hao maaskari wakawashambulia na makombeo wakiwazunguka na kuishambulia.
26 And when the King of Moab saw that the battel was too sore for him, he tooke with him seuen hudreth men that drew the sword, to break through vnto the King of Edom: but they could not.
Ndipo Mfalme Mesha wa Moabu alipoona kwamba ameshindwa, alichukua watu hodari wa upanga mia saba pamoja naye kwenda kwa mfalme wa Edomu, lakini walishindwa.
27 Then he tooke his eldest sonne, that should haue reigned in his stead, and offered him for a burnt offring vpon the wall: so that Israel was sore grieued, and they departed from him, and returned to their countrey.
Ndipo akamchukua mtoto wake wa kwanza, ambaye angetawala baada ya yeye, na akamuudhi kwa kumtoa kama sadaka ya kuteketezwa juu ya ukuta. Hivyo, kulikuwa na hasira kubwa dhidi ya Israeli, na hao Waisraeli, na Jeshi la Israeli likamuacha mfalme Mesha na kurudi kwenye nchi yao.

< 2 Kings 3 >