< Numbers 33 >

1 These are the mansions of the children of Israel, who went out of Egypt by their troops under the conduct of Moses and Aaron,
Hivi ndivyo vituo katika safari ya Waisraeli walipotoka Misri kwa vikosi chini ya uongozi wa Mose na Aroni.
2 Which Moses wrote down according to the places of their encamping, which they changed by the commandment of the Lord.
Kwa agizo la Bwana, Mose aliweka kumbukumbu ya vituo katika safari yao. Hivi ndivyo vituo katika safari yao:
3 Now the children of Israel departed from Ramesses the first month, on the fifteenth day of the first month, the day after the phase, with a mighty hand, in the eight of all the Egyptians,
Waisraeli walisafiri kutoka Ramesesi katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa kwanza, siku iliyofuata Pasaka. Walitembea kwa ujasiri wazi mbele ya Wamisri wote,
4 Who were burying their firstborn, whom the Lord had slain (upon their gods also he had executed vengeance, )
waliokuwa wakizika wazaliwa wao wa kwanza wote, ambao Bwana alikuwa amewaua katikati yao, kwa kuwa Bwana alikuwa ameleta hukumu juu ya miungu yao.
5 And they camped in Soccoth.
Waisraeli waliondoka Ramesesi na kupiga kambi huko Sukothi.
6 And from Soccoth they came into Etham, which is in the uttermost borders of the wilderness.
Wakaondoka Sukothi na kupiga kambi huko Ethamu, pembeni mwa jangwa.
7 Departing from thence they came over against Phihahiroth, which looketh towards Beelsephon, and they camped before Magdalum.
Wakaondoka Ethamu, wakageuka wakarudi Pi-Hahirothi, hadi mashariki ya Baal-Sefoni, wakapiga kambi yao karibu na Migdoli.
8 And departing from Phihahiroth, they passed through the midst of the sea into the wilderness: and having marched three days through the desert of Etham, they camped in Mara.
Wakaondoka Pi-Hahirothi wakapita katikati ya bahari mpaka jangwani, na baada ya kusafiri kwa siku tatu katika Jangwa la Ethamu, walipiga kambi huko Mara.
9 And departing from Mara, they came into Elim, where there were twelve fountains of waters, and seventy palm trees: and there they camped.
Wakaondoka Mara wakaenda Elimu, mahali ambapo palikuwa na chemchemi kumi na mbili na mitende sabini, huko wakapiga kambi.
10 But departing from thence also, they pitched their tents by the Red Sea. And departing from the Red Sea,
Wakaondoka Elimu na kupiga kambi kando ya Bahari ya Shamu.
11 They camped in the desert of Sin.
Wakaondoka kando ya Bahari ya Shamu na kupiga kambi katika Jangwa la Sini.
12 And they removed from thence, and came to Daphca.
Wakaondoka katika Jangwa la Sini, wakapiga kambi huko Dofka.
13 And departing from Daphca, they camped in Alus.
Wakaondoka Dofka, wakapiga kambi huko Alushi.
14 And departing from Alus, they pitched their tents in Raphidim, where the people wanted water to drink.
Wakaondoka Alushi, wakapiga kambi Refidimu, mahali ambapo hapakuwa na maji kwa ajili ya watu kunywa.
15 And departing from Raphidim, they camped in the desert of Sinai.
Wakaondoka Refidimu na kupiga kambi katika Jangwa la Sinai.
16 But departing also from the desert of Sinai, they came to the graves of lust.
Wakaondoka katika Jangwa la Sinai na kupiga kambi huko Kibroth-Hataava.
17 And departing from the graves of lust, they camped in Haseroth.
Wakaondoka Kibroth-Hataava na kupiga kambi huko Haserothi.
18 And from Haseroth they came to Rethma.
Wakaondoka Haserothi na kupiga kambi huko Rithma.
19 And departing from Rethma, they camped in Remmomphares.
Wakaondoka Rithma na kupiga kambi huko Rimon-Peresi.
20 And they departed from thence and came to Lebna.
Wakaondoka Rimon-Peresi na kupiga kambi huko Libna.
21 Removing from Lebna they camped in Ressa.
Wakaondoka Libna na kupiga kambi huko Risa.
22 And departing from Ressa, they came to Ceelatha.
Wakaondoka Risa na kupiga kambi huko Kehelatha.
23 And they removed from thence and camped in the mountain Sepher.
Wakaondoka Kehelatha na kupiga kambi kwenye mlima Sheferi.
24 Departing from the mountain Sepher, they came to Arada.
Wakaondoka kwenye mlima Sheferi na kupiga kambi huko Harada.
25 From thence they went and camped in Maceloth.
Wakaondoka Harada na kupiga kambi huko Makelothi.
26 And departing from Maceloth, they came to Thahath.
Wakaondoka Makelothi na kupiga kambi huko Tahathi.
27 Removing from Thahath they camped in Thare.
Wakaondoka Tahathi na kupiga kambi huko Tera.
28 And they departed from thence, and pitched their tents in Methca.
Wakaondoka Tera na kupiga kambi huko Mithka.
29 And removing from Methca, they camped in Hesmona.
Wakaondoka Mithka na kupiga kambi huko Hashmona.
30 And departing from Hesmona, they came to Moseroth.
Wakaondoka Hashmona na kupiga kambi Moserothi.
31 And removing from Moseroth, they camped in Benejaacan.
Wakaondoka Moserothi na kupiga kambi huko Bene-Yakani.
32 And departing from Benejaacan, they came to mount Gadgad.
Wakaondoka Bene-Yakani na kupiga kambi huko Hor-Hagidgadi.
33 From thence they went and camped in Jetebatha.
Wakaondoka Hor-Hagidgadi na kupiga kambi huko Yotbatha.
34 And from Jetebatha they came to Hebrona.
Wakaondoka Yotbatha na kupiga kambi huko Abrona.
35 And departing from Hebrona, they camped in Asiongaber.
Wakaondoka Abrona na kupiga kambi huko Esion-Geberi.
36 They removed from thence and came into the desert of Sin, which is Cades.
Wakaondoka Esion-Geberi na kupiga kambi huko Kadeshi katika Jangwa la Sini.
37 And departing from Cades, they camped in mount Her, in the uttermost borders of the land of Edom.
Wakaondoka Kadeshi na kupiga kambi kwenye Mlima Hori, mpakani mwa Edomu.
38 And Aaron the priest went up into mount Hor at the commandment of the Lord: and there he died in the fortieth year of the coming forth of the children of Israel out of Egypt, the fifth month, the first day of the month,
Kwa amri ya Bwana, kuhani Aroni alipanda Mlima Hori, mahali alipofia katika siku ya kwanza ya mwezi wa tano, mwaka wa arobaini baada ya Waisraeli kutoka Misri.
39 When he was a hundred and twenty-three years old.
Aroni alikufa juu ya Mlima Hori akiwa na umri wa miaka 123.
40 And king Arad the Chanaanite, who dwelt towards the south, heard that the children of Israel were come to the land of Chanaan.
Mfalme Mkanaani wa Aradi, ambaye aliishi huko Negebu ya Kanaani, akasikia kwamba Waisraeli wanakuja.
41 And they departed from mount Her, and camped in Salmona.
Wakaondoka kwenye mlima Hori na kupiga kambi huko Salmona.
42 From whence they removed and came to Phunon.
Wakaondoka Salmona, wakapiga kambi huko Punoni.
43 And departing from Phunon, they camped in Oboth.
Wakaondoka Punoni, wakapiga kambi huko Obothi.
44 And from Oboth they came to Ijeabarim, which is in the borders of the Moabites.
Wakaondoka Obothi, wakapiga kambi huko Iye-Abarimu, mipakani mwa Moabu.
45 And departing from Ijeabarim they pitched their tents in Dibongab.
Wakaondoka Iye-Abarimu, wakapiga kambi huko Dibon-Gadi.
46 From thence they went and camped in Helmondeblathaim.
Wakaondoka Dibon-Gadi na kupiga kambi huko Almon-Diblathaimu.
47 And departing from Helmondeblathaim, they came to the mountains of Abarim over against Nabo.
Wakaondoka Almon-Diblathaimu na kupiga kambi katika milima ya Abarimu, karibu na Nebo.
48 And departing from the mountains of Abarim, they passed to the plains of Moab, by the Jordan, over against Jericho.
Wakaondoka kwenye milima ya Abarimu na kupiga kambi kwenye tambarare ya Moabu, kando ya Yordani ngʼambo ya Yeriko.
49 And there they camped from Bethsi moth even to Ablesatim in the plains of the Moabites,
Huko kwenye tambarare za Moabu walipiga kambi kandokando ya Mto Yordani, kuanzia Beth-Yeshimothi mpaka Abel-Shitimu.
50 Where the Lord said to Moses:
Katika tambarare za Moabu kando ya Yordani kuvukia Yeriko, Bwana akamwambia Mose,
51 Command the children of Israel, and say to them: When you shall have passed over the Jordan, entering into the land of Chanaan,
“Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Mtakapovuka Mto Yordani kuingia Kanaani,
52 Destroy all the inhabitants of that land: beat down their pillars, and break in pieces their statues, and waste all their high places,
wafukuzeni wakazi wote wa nchi iliyo mbele yenu. Haribuni sanamu zao zote za kuchongwa, na sanamu zilizotengenezwa kwa kuyeyusha chuma, na kupabomoa mahali pao pa ibada.
53 Cleansing the land, and dwelling in it. For I have given it you for a possession.
Mtaimiliki nchi hiyo na kukaa huko, kwa kuwa nimewapeni ninyi kuimiliki.
54 And you shall divide it among you by lot. To the more you shall give a larger part, and to the fewer a lesser. To every one as the lot shall fall, so shall the inheritance be given. The possession shall be divided by the tribes and the families.
Mtaigawanya nchi hiyo kwa kupiga kura, kufuatana na koo zenu. Kwa kundi kubwa zaidi toa urithi mkubwa zaidi, na kwa kundi dogo zaidi urithi mdogo zaidi. Chochote kinachowaangukia kwa kura kitakuwa chao. Mtaigawanya nchi kufuatana na makabila ya babu zenu.
55 But if you will not kill the inhabitants of the land: they that remain, shall be unto you as nails in your eyes, and spears in your sides, and they shall be your adversaries in the land of your habitation.
“‘Lakini kama hamkuwafukuza wenyeji wakaao katika nchi hiyo, wale mtakaowaruhusu wabaki watakuwa kama sindano kwenye macho yenu na miiba kwenu kila upande. Watawasumbua katika nchi mtakayoishi.
56 And whatsoever I had thought to do to them, I will do to you.
Kisha nitawatenda ninyi kile ambacho nimepanga kuwatenda wao.’”

< Numbers 33 >