< Numbers 3 >

1 These are the generations of Aaron and Moses, in the day when the Lord spoke to Moses on mount Sinai.
Hii ni hesabu ya jamaa ya Aroni na Mose kwa wakati ambao Bwana alizungumza na Mose katika Mlima Sinai.
2 And these are the names of the sons of Aaron: his firstborn Nadab, then Abihu, and Eleazar, and Ithamar.
Majina ya wana wa Aroni yalikuwa: Nadabu mzaliwa wa kwanza na Abihu, Eleazari na Ithamari.
3 These are the names of the sons of Aaron, the priests who were anointed and whose hands were filled and consecrated in order to exercise the priesthood.
Hayo yalikuwa majina ya wana wa Aroni, makuhani wapakwa mafuta, waliokuwa wamesimikwa kuhudumu kama makuhani.
4 For Nadab and Abihu died without children, when they offered, in the sight of the Lord, a strange fire, in the desert of Sinai. And so, Eleazar and Ithamar exercised the priesthood in the sight of Aaron, their father.
Hata hivyo Nadabu na Abihu walikufa mbele za Bwana walipotoa sadaka kwa moto usioruhusiwa mbele zake katika Jangwa la Sinai. Hawakuwa na wana; kwa hiyo Eleazari na Ithamari walihudumu peke yao kama makuhani wakati wote wa maisha ya Aroni baba yao.
5 And the Lord spoke to Moses, saying:
Bwana akamwambia Mose,
6 “Bring forward the tribe of Levi, and cause them to stand in the sight of Aaron the priest, in order to minister to him. And let them keep watch outside,
“Walete watu wa kabila la Lawi mbele ya Aroni kuhani ili wamsaidie.
7 and let them observe whatever pertains to the ritual for the multitude, in front of the tabernacle of the testimony,
Watafanya huduma kwa ajili yake na kwa jumuiya yote katika Hema la Kukutania kwa kufanya kazi za Maskani.
8 and let them take care of the vessels of the tabernacle, serving in its ministry.
Watatunza samani zote za Hema la Kukutania, wakitimiza wajibu wa kuhudumia Waisraeli kwa kufanya kazi ya Maskani.
9 And you shall give the Levites as a gift to Aaron and his sons; for they have been delivered to them by the sons of Israel.
Wakabidhi Walawi kwa Aroni na wanawe; hao ndio Waisraeli ambao wanakabidhiwa kwake kabisa.
10 But you shall appoint Aaron and his sons over the service of the priesthood. The outsider who approaches to minister shall be put to death.”
Waweke Aroni na wanawe kuhudumu kama makuhani; mtu mwingine yeyote atakayesogea mahali patakatifu ni lazima auawe.”
11 And the Lord spoke to Moses, saying:
Bwana akamwambia Mose,
12 “I have taken the Levites from the sons of Israel. For the Levites, and all the firstborn who open the womb among the sons of Israel, shall be mine.
“Nimewatwaa Walawi kutoka miongoni mwa Waisraeli badala ya mzaliwa wa kwanza wa kiume wa kila mwanamke wa Mwisraeli. Walawi ni wangu,
13 For every firstborn is mine. From the time that I struck the firstborn in the land of Egypt, I have sanctified for myself whatever is born first in Israel. From man, even to beast, they are mine. I am the Lord.”
kwa kuwa wazaliwa wote wa kwanza ni wangu. Nilipowaua wazaliwa wa kwanza huko Misri, nilimtenga kila mzaliwa wa kwanza katika Israeli awe wangu, akiwa mwanadamu au mnyama. Watakuwa wangu. Mimi ndimi Bwana.”
14 And the Lord spoke to Moses in the desert of Sinai, saying:
Bwana akamwambia Mose katika Jangwa la Sinai,
15 “Number the sons of Levi by the houses of their fathers and their families, every male from one month and above.”
“Wahesabu Walawi kwa jamaa zao na koo zao. Mhesabu kila mwanaume mwenye umri wa mwezi mmoja au zaidi.”
16 Moses numbered them, just as the Lord had instructed,
Kwa hiyo Mose akawahesabu, kama alivyoamriwa na neno la Bwana.
17 and there were found the sons of Levi by their names: Gershon and Kohath and Merari.
Haya yalikuwa majina ya wana wa Lawi: Gershoni, Kohathi na Merari.
18 The sons of Gershon: Libni and Shimei.
Haya ndiyo yaliyokuwa majina ya koo za Wagershoni: Libni na Shimei.
19 The sons of Kohath: Amram, and Izhar, Hebron and Uzziel.
Koo za Wakohathi zilikuwa ni: Amramu, Ishari, Hebroni na Uzieli.
20 The sons of Merari: Mahli and Mushi.
Koo za Wamerari zilikuwa ni: Mahli na Mushi. Hizi ndizo zilizokuwa koo za Walawi, kufuatana na jamaa zao.
21 From Gershon were two families: the Libnites, and the Shimeites.
Kulikuwa na koo za Walibni na Washimei kwa Gershoni; hizi ndizo zilizokuwa koo za Wagershoni.
22 The people of these were numbered, of the male sex, from one month and above: seven thousand five hundred.
Idadi ya waume wote waliokuwa na mwezi mmoja au zaidi waliohesabiwa walikuwa 7,500.
23 These shall encamp behind the tabernacle, toward the west,
Ukoo wa Wagershoni walitakiwa kuweka kambi zao upande wa magharibi, nyuma ya Maskani.
24 under the leader Eliasaph the son of Lael.
Kiongozi wa jamaa za Wagershoni alikuwa Eliasafu mwana wa Laeli.
25 And they shall keep watch over the tabernacle of the covenant:
Katika Hema la Kukutania, Wagershoni walikuwa na wajibu wa kutunza Maskani na hema, vifuniko vyake, pazia katika mlango wa kuingilia ndani ya Hema la Kukutania,
26 the tabernacle itself, and its covering; the tent that is drawn before the doors of the covering of the covenant; and the curtains of the atrium; likewise, the tent that is suspended at the entrance of the atrium of the tabernacle; and whatever pertains to the ritual of the altar; the cords of the tabernacle and all its implements.
mapazia ya ua, pazia katika ingilio la ua unaozunguka Maskani na madhabahu, pamoja na kamba, na kila kinachohusika kwa matumizi yake.
27 The kinship of Kohath includes the peoples of the Amramites and Izharites and Hebronites and Uzzielites. These are the families of the Kohathites, having been counted by their names,
Kwa Kohathi kulikuwepo koo za Waamramu, Waishari, Wahebroni na Wauzieli; hizi ndizo zilizokuwa koo za Wakohathi.
28 all those of the male gender, from one month and above: eight thousand six hundred. They shall keep watch over the Sanctuary,
Hesabu ya waume wote wenye mwezi mmoja au zaidi ilikuwa watu 8,600. Wakohathi waliwajibika kutunza mahali patakatifu.
29 and they shall encamp toward the south side.
Koo za Wakohathi zilitakiwa kuweka kambi zao upande wa kusini wa Maskani.
30 And their leader shall be Elisaphan the son of Uzziel.
Kiongozi wa jamaa za koo za Wakohathi alikuwa Elisafani mwana wa Uzieli.
31 And they shall take care of the ark, and the table and the lampstand, the altars and the vessels of the Sanctuary, by which they minister, and the veil, and all the articles of this kind.
Waliwajibika kutunza Sanduku la Agano, meza, kinara cha taa, madhabahu, na vile vyombo vya mahali patakatifu vinavyotumika kuhudumu, pazia, na kila kitu kinachohusika na matumizi yake.
32 But the leader of the leaders of the Levites, Eleazar the son of Aaron the priest, shall be over those who watch over the care of the Sanctuary.
Kiongozi mkuu wa Walawi alikuwa Eleazari mwana wa kuhani, Aroni. Aliwekwa juu ya wale waliowajibika kutunza mahali patakatifu.
33 And truly, from Merari are the peoples of the Mahlites and Mushites, having been counted by their names,
Kwa Merari kulikuwa na koo za Wamahli na Wamushi; hizi zilikuwa koo za Merari.
34 all those of the male gender, from one month and above: six thousand two hundred.
Hesabu ya waume wote wenye umri wa mwaka mmoja au zaidi waliohesabiwa walikuwa 6,200.
35 Their leader is Suriel the son of Abihaiel. They shall make camp on the north side.
Kiongozi wa jamaa za koo za Wamerari alikuwa Surieli mwana wa Abihaili; hawa walitakiwa kuweka kambi zao upande wa kaskazini mwa Maskani.
36 Under their care shall be the panels of the tabernacle, and the bars, and the columns with their bases, and all the things which pertain to service of this kind,
Wamerari waliwekwa kutunza miimo ya Maskani, mataruma yake, nguzo, vitako na vifaa vyake vyote na kila kitu kilichohusika na matumizi yake,
37 and the columns of the surrounding atrium with their bases, and the tent pegs with their cords.
na pia nguzo za ua unaozunguka pamoja na vitako vyake, vigingi vya hema na kamba zake.
38 Moses and Aaron, with their sons, shall make camp before the tabernacle of the covenant, that is, on the east side, holding the custody of the Sanctuary in the midst of the sons of Israel. Whatever foreigner approaches it shall die.
Mose, na Aroni na wanawe walitakiwa kuweka kambi zao mashariki mwa Maskani, kuelekea mawio ya jua, mbele ya Hema la Kukutania. Wao walihusika na utunzaji wa mahali patakatifu kwa niaba ya Waisraeli. Mtu mwingine yeyote aliyepasogelea mahali patakatifu angeuawa.
39 All the Levites, whom Moses and Aaron numbered by their families according to the precept of the Lord, of the male gender, from one month and above, were twenty-two thousand.
Jumla ya hesabu ya Walawi waliohesabiwa na Mose na Aroni kwa amri ya Bwana, kufuatana na koo, pamoja na kila mume mwenye umri wa mwezi mmoja au zaidi, walikuwa 22,000.
40 And the Lord said to Moses: “Number the firstborn of the male sex from the sons of Israel, from one month and above, and you shall take their total.
Bwana akamwambia Mose, “Wahesabu wazaliwa wa kwanza wa kiume wote wa Waisraeli wenye umri wa mwezi mmoja au zaidi na uorodheshe majina yao.
41 And you shall bring the Levites to me, in place of all the firstborn of the sons of Israel, and you shall bring their cattle to me, in place of all the firstborn of the cattle of the sons of Israel. I am the Lord.”
Nitwalie Walawi badala ya wazaliwa wa kwanza wa Waisraeli, nayo mifugo ya Walawi badala ya wazaliwa wa mifugo ya Waisraeli. Mimi ndimi Bwana.”
42 Moses took a census, just as the Lord had instructed, of the firstborn of the sons of Israel.
Hivyo Mose akawahesabu wazaliwa wa kwanza wote wa Waisraeli, kama Bwana alivyomwamuru.
43 And the males by their names, from one month and above, were twenty-two thousand two hundred seventy-three.
Jumla ya hesabu ya wazaliwa wa kwanza waume wenye umri wa mwezi mmoja au zaidi, walioorodheshwa kwa majina, walikuwa 22,273.
44 And the Lord spoke to Moses, saying:
Bwana akamwambia Mose,
45 “Take the Levites, in place of the firstborn of the sons of Israel, and the cattle of the Levites, in place of their cattle, and so the Levites shall be mine. I am the Lord.
“Watwae Walawi badala ya wazaliwa wa kwanza wote wa Israeli, nayo mifugo ya Walawi badala ya mifugo yao. Walawi watakuwa wangu. Mimi ndimi Bwana.
46 But for the price of the two hundred and seventy-three, which exceed the number of the Levites compared to the number of firstborn of the sons of Israel,
Ili kukomboa wazao wa kwanza 273 wa Waisraeli ambao wamezidi hesabu ya Walawi,
47 you shall take five shekels for each head, by the measure of the Sanctuary. A shekel has twenty obols.
kusanya shekeli tano kwa kila mmoja, kufuatana na shekeli ya mahali patakatifu, ambayo ina uzito wa gera ishirini.
48 And you shall give the money to Aaron and his sons as the price of those that are in excess.”
Mpe Aroni na wanawe hizo fedha kwa ajili ya ukombozi wa idadi ya Waisraeli waliozidi.”
49 Therefore, Moses took the money for those that were in excess, and whom they had redeemed from the Levites
Kwa hiyo Mose akakusanya fedha za ukombozi kutoka kwa wale ambao hesabu yao ilizidi wale waliokombolewa na Walawi.
50 in place of the firstborn of the sons of Israel: one thousand three hundred sixty-five shekels, according to the weight of the Sanctuary.
Kutokana na wazaliwa wa kwanza wa Waisraeli alikusanya fedha yenye uzito wa shekeli 1,365 kufuatana na shekeli ya mahali patakatifu.
51 And he gave it to Aaron and his sons, according to the word by which the Lord had instructed him.
Mose akampa Aroni na wanawe ile fedha ya ukombozi, kama alivyoamriwa na neno la Bwana.

< Numbers 3 >