< Numbers 2 >

1 And the Lord spoke to Moses and Aaron, saying:
Bwana aliwaambia Mose na Aroni:
2 “Each one shall make camp, by their troops, as well as by their insignia and standards, and by the houses of their kinships, all around the tabernacle of the covenant.”
“Waisraeli watapiga kambi zao kuzunguka Hema la Kukutania kwa umbali fulani kutoka kwenye hema, kila mwanaume chini ya alama yake pamoja na bendera ya jamaa yake.”
3 To the east, Judah shall fix his tents, by the companies of his army. And the leader of his sons shall be Nahshon the son of Amminadab.
Kwa upande wa mashariki kuelekea mawio ya jua, kambi ya makundi ya Yuda watapiga kambi chini ya alama yao. Kiongozi wa watu wa Yuda ni Nashoni mwana wa Aminadabu.
4 And the entire total of the fighting men from his stock was seventy-four thousand six hundred.
Kundi lake lina watu 74,600.
5 Beside him, those of the tribe of Issachar were encamped, whose leader was Nathanael the son of Zuar.
Kabila la Isakari watapiga kambi karibu na Yuda. Kiongozi wa watu wa Isakari ni Nethaneli mwana wa Suari.
6 And the entire number of his fighting men was fifty-four thousand four hundred.
Kundi lake lina watu 54,400.
7 In the tribe of Zebulon, the leader was Eliab the son of Helon.
Kabila la Zabuloni litafuata. Kiongozi wa watu wa Zabuloni ni Eliabu mwana wa Heloni.
8 All the army of fighting men from his stock were fifty-seven thousand four hundred.
Kundi lake lina watu 57,400.
9 All who were numbered in the camp of Judah were one hundred eighty-six thousand four hundred. And these, by their companies, shall go forth first.
Wanaume wote walio katika kambi ya Yuda, kufuatana na makundi yao, ni 186,400. Wao watatangulia kuondoka.
10 In the camp of the sons of Ruben, toward the south side, the leader shall be Elizur the son of Shedeur.
Kwa upande wa kusini kutakuwa kambi ya makundi ya Reubeni chini ya alama yao. Kiongozi wa watu wa Reubeni ni Elisuri mwana wa Shedeuri.
11 And the entire army of his fighting men, who were numbered, were forty-six thousand five hundred.
Kundi lake lina watu 46,500.
12 Beside him, those of the tribe of Simeon were encamped, whose leader was Shelumiel the son of Zurishaddai.
Kabila la Simeoni watapiga kambi karibu na Reubeni. Kiongozi wa watu wa Simeoni ni Shelumieli mwana wa Surishadai.
13 And the entire army of his fighting men, who were numbered, were fifty-nine thousand three hundred.
Kundi lake lina watu 59,300.
14 In the tribe of Gad, the leader was Eliasaph the son of Reuel.
Kabila la Gadi litafuata. Kiongozi wa watu wa Gadi ni Eliasafu mwana wa Deueli.
15 And the entire army of his fighting men, who were numbered, were forty-five thousand six hundred fifty.
Kundi lake lina watu 45,650.
16 All who were counted in the camp of Ruben were one hundred fifty thousand and one thousand four hundred fifty, by their companies. These shall advance in the second place.
Wanaume wote walio katika kambi ya Reubeni, kufuatana na makundi yao, ni 151,450. Nao watakuwa nafasi ya pili kuondoka.
17 But the tabernacle of the testimony shall be lifted up by the officers of the Levites and their companies. In the manner in which it is set up, so also shall it be taken down. Each one shall advance according to their places and ranks.
Kisha Hema la Kukutania na kambi ya Walawi vitakuwa katikati ya kambi zote. Wao watasafiri kwa utaratibu ule ule kama walivyopiga kambi, kila mmoja mahali pake mwenyewe chini ya alama yake.
18 On the west side, there shall be the camp of the sons of Ephraim, whose leader was Elishama the son of Ammihud.
Upande wa magharibi kutakuwepo na kambi ya makundi ya Efraimu chini ya alama yao. Kiongozi wa watu wa Efraimu ni Elishama mwana wa Amihudi.
19 The entire army of his fighting men, who were numbered, were forty thousand five hundred.
Kundi lake lina watu 40,500.
20 And with them was the tribe of the sons of Manasseh, whose leader was Gamaliel the son of Pedahzur.
Kabila la Manase litafuata baada ya Efraimu. Kiongozi wa watu wa Manase ni Gamalieli mwana wa Pedasuri.
21 And the entire army of his fighting men, who were numbered, were thirty-two thousand two hundred.
Kundi lake lina watu 32,200.
22 In the tribe of the sons of Benjamin, the leader was Abidan the son of Gideoni.
Kabila la Benyamini litafuata baada ya Manase. Kiongozi wa watu wa Benyamini ni Abidani mwana wa Gideoni.
23 And the entire army of his fighting men, who were counted, were thirty-five thousand four hundred.
Kundi lake lina watu 35,400.
24 All who were numbered in the camp of Ephraim were one hundred eight thousand one hundred, by their companies. These shall advance third.
Wanaume wote walio katika kambi ya Efraimu kufuatana na makundi yao ni 108,100. Nao watakuwa nafasi ya tatu kuondoka.
25 Toward the north side, the sons of Dan were encamped, whose leader was Ahiezer the son of Ammishaddai.
Upande wa kaskazini kutakuwa na makundi ya kambi ya Dani, chini ya alama yao. Kiongozi wa watu wa Dani ni Ahiezeri mwana wa Amishadai.
26 The entire army of his fighting men, who were numbered, were sixty-two thousand seven hundred.
Kundi lake lina watu 62,700.
27 Beside him, those of the tribe of Asher fixed their tents, whose leader was Pagiel the son of Ochran.
Kabila la Asheri watapiga kambi karibu na Dani. Kiongozi wa watu wa Asheri ni Pagieli mwana wa Okrani.
28 The entire army of his fighting men, who were numbered, were forty thousand and one thousand five hundred.
Kundi lake lina watu 41,500.
29 From the tribe of the sons of Naphtali, the leader was Ahira the son of Enan.
Kabila la Naftali litafuata. Kiongozi wa watu wa Naftali ni Ahira mwana wa Enani.
30 The entire army of his fighting men were fifty-three thousand four hundred.
Kundi lake lina watu 53,400.
31 All who were numbered in the camp of Dan were one hundred fifty-seven thousand six hundred; and these shall advance at the very end.
Wanaume wote walio katika kambi ya Dani ni 157,600. Wao watakuwa wa mwisho kuondoka chini ya alama yao.
32 This is the number of the sons of Israel, of their army divided by the houses of their kinships and their companies: six hundred three thousand five hundred fifty.
Hawa ndio Waisraeli, wakiwa wamehesabiwa kufuatana na jamaa zao. Wote walio kambini kwa makundi yao ni watu 603,550.
33 But the Levites were not numbered among the sons of Israel. For so the Lord had instructed Moses.
Hata hivyo, Walawi hawakuhesabiwa pamoja na Waisraeli wengine, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
34 And the sons of Israel acted according to all the things that the Lord had commanded. They were encamped by their companies, and they advanced by the families and houses of their fathers.
Kwa hiyo Waisraeli wakafanya kila kitu Bwana alichomwamuru Mose. Hivyo ndivyo walivyopiga kambi chini ya alama zao, pia hivyo ndivyo walivyoondoka, kila mmoja akiwa na ukoo wake na jamaa yake.

< Numbers 2 >