< Deuteronomy 8 >

1 You shall observe to do all the commands which I charge you today, that you may live and be multiplied, and enter in and inherit the land, which the Lord your God sware [to give] to your fathers.
Uwe mwangalifu kufuata kila agizo ninalokupa wewe leo, ili mweze kuishi, kuongezeka na mweze kuingia mkamiliki nchi ambayo Bwana aliahidi kwa kiapo kwa baba zenu.
2 And you shall remember all the way which the Lord your God led you in the wilderness, that he might afflict you, and try you, and that the things in your heart might be made manifest, whether you would keep his commandments or no.
Kumbuka jinsi Bwana Mungu wenu alivyowaongoza katika njia yote katika jangwa kwa miaka hii arobaini, kukunyenyekeza na kukujaribu ili ajue lililoko moyoni mwako, kwamba utayashika maagizo yake au la.
3 And he afflicted you and straitened you with hunger, and fed you with manna, which your fathers knew not; that he might teach you that man shall not live by bread alone, but by every word that proceeds out of the mouth of God shall man live.
Alikudhili na kukufanya uone njaa kisha akulishe kwa mana, ambayo wewe wala baba zako hamkuijua, awafundishe kuwa mwanadamu hataishi kwa mkate tu bali kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Bwana.
4 Your garments grew not old from off you, your shoes were not worn from off you, your feet were not [painfully] hardened, behold! these forty years.
Nguo zenu hazikuchakaa wala miguu yenu haikuvimba kwa miaka hii arobaini.
5 And you shall know in your heart, that as if any man should chasten his son, so the Lord your God will chasten you.
Mjue basi ndani ya mioyo yenu kama mtu anavyomwadibisha mwanawe, ndivyo Bwana Mungu wako atawaadibisha ninyi.
6 And you shall keep the commands of the Lord your God, to walk in his ways, and to fear him.
Shikeni maagizo ya Bwana Mungu wenu mtembee katika njia zake na kumheshimu.
7 For the Lord your God will bring you into a good and extensive land, where there are torrents of waters, and fountains of deep places issuing through the plains and through the mountains:
Kwa kuwa Bwana Mungu wenu anawaleta katika nchi nzuri, nchi yenye vijito na mabwawa ya maji, yenye chemchemi zinazotiririka mabondeni na katika vilima;
8 a land of wheat and barley, [wherein are] vines, figs, pomegranates; a land of olive oil and honey;
nchi yenye ngano na shayiri, mizabibu na mitini, mikomamanga, mafuta ya zeituni na asali;
9 a land on which you shall not eat your bread with poverty, and you shall not lack any thing upon it; a land whose stones are iron, and out of its mountains you shall dig brass.
nchi ambayo chakula hakitapungua na hamtakosa chochote; nchi ambayo miamba yake ni chuma na mnaweza kuchimba shaba kutoka kwenye vilima.
10 And you shall eat and be filled, and shall bless the Lord your God on the good land, which he has given you.
Wakati mtakapokwisha kula na kushiba, msifuni Bwana Mungu wenu kwa ajili ya nchi nzuri aliyowapa.
11 Take heed to yourself that you forget not the Lord your God, so as not to keep his commands, and his judgements, and ordinances, which I command you this day:
Jihadharini msimsahau Bwana Mungu wenu, mkashindwa kushika maagizo yake, sheria na amri zake ambazo ninawapa leo.
12 lest when you have eaten and are full, and have built goodly houses, and lived in them;
Angalia wakati mtakapokuwa mmekula na kushiba, mkajenga nyumba nzuri na kukaa humo,
13 and your oxen and your sheep are multiplied to you, and your silver and your gold are multiplied to you, and all your possessions are multiplied to you,
na wakati makundi yenu ya ngʼombe na mbuzi na kondoo yatakapoongezeka na fedha na dhahabu yenu itakapoongezeka na vyote mlivyo navyo vitakapozidishwa,
14 you should be exalted in heart, and forget the Lord your God, who brought you out of the land of Egypt, out of the house of bondage:
basi mioyo yenu isiwe na kiburi mkamsahau Bwana Mungu wenu aliyewatoa katika nchi ya Misri, kutoka nchi ya utumwa.
15 who brought you through that great and terrible wilderness, where [is] the biting serpent, and scorpion, and drought, where there was no water; who brought you a fountain of water out of the flinty rock:
Aliwaongoza kupitia jangwa lile kubwa na la kutisha, nchi ile ya kiu isiyo na maji, yenye nyoka wa sumu na nge. Aliwatolea maji kutoka kwenye mwamba mgumu.
16 who fed you with manna in the wilderness, which you knew not, and your fathers knew not; that he might afflict you, and thoroughly try you, and do you good in your latter days.
Aliwapa mana ya kula jangwani, kitu ambacho baba zenu hawakukijua, ili kuwanyenyekesha na kuwajaribu ninyi ili mwishoni apate kuwatendea mema.
17 Lest you should say in your heart, My strength, and the power of mine hand have wrought for me this great wealth.
Mnaweza kusema, “Uwezo wangu na nguvu za mikono yangu ndizo zilizonipatia utajiri huu.”
18 But you shall remember the Lord your God, that he gives you strength to get wealth; even that he may establish his covenant, which the Lord sware to your fathers, as at this day.
Lakini kumbukeni Bwana Mungu wenu, ndiye ambaye huwapa uwezo wa kupata utajiri, na hivyo kulithibitisha Agano lake, ambalo aliwaapia baba zenu, kama ilivyo leo.
19 And it shall come to pass if you do at all forget the Lord your God, and should go after other gods, and serve them, and worship them, I call heaven and earth to witness against you this day, that you shall surely perish.
Ikiwa mtamsahau Bwana Mungu wenu, mkaifuata miungu mingine, mkaiabudu na kuisujudia, ninashuhudia dhidi yenu leo kwamba hakika mtaangamizwa.
20 As also the other nations which the Lord God destroys before your face, so shall you perish, because you listened not to the voice of the Lord your God.
Kama mataifa Bwana aliyoyaangamiza mbele yenu, ndivyo ninyi mtakavyoangamizwa kwa kutokumtii Bwana Mungu wenu.

< Deuteronomy 8 >