< Numbers 1 >

1 And the Lord spoke to Moses in the wilderness of Sina, in the tabernacle of witness, on the first day of the second month, in the second year of their departure from the land of Egypt, saying,
Bwana alisema na Mose katika Jangwa la Sinai, katika Hema la Kukutania, siku ya kwanza ya mwezi wa pili, katika mwaka wa pili baada ya Waisraeli kutoka nchi ya Misri. Akamwambia,
2 Take the sum of all the congregation of Israel according to their kindred, according to the houses of their fathers' families, according to their number by their names, according to their heads: every male
“Hesabu watu wa jumuiya yote ya Waisraeli kwa kufuata koo zao na jamaa zao, ukiorodhesha kila mwanaume kwa jina lake, mmoja mmoja.
3 from twenty years old and upwards, every one that goes forth in the forces of Israel, take account of them with their strength; you and Aaron take account of them.
Wewe na Aroni mtawahesabu kwa migawanyo yao wanaume wote katika Israeli wenye miaka ishirini na kuendelea ambao wanaweza kutumika katika jeshi.
4 And with you there shall be each one of the rulers according to the tribe of each: they shall be according to the houses of their families.
Mwanaume mmoja kutoka kila kabila, kila aliye kiongozi wa jamaa yake, atawasaidia.
5 And these are the names of the men who shall be present with you; of the tribe of Ruben, Elisur the son of Sediur.
Haya ndiyo majina ya wanaume watakaowasaidia: “kutoka Reubeni, ni Elisuri mwana wa Shedeuri;
6 Of Symeon, Salamiel the son of Surisadai.
kutoka Simeoni, ni Shelumieli mwana wa Surishadai;
7 Of Juda, Naasson the son of Aminadab.
kutoka Yuda, ni Nashoni mwana wa Aminadabu;
8 Of Issachar, Nathanael the son of Sogar.
kutoka Isakari, ni Nethaneli mwana wa Suari;
9 Of Zabulon, Eliab the son of Chaelon.
kutoka Zabuloni, ni Eliabu mwana wa Heloni;
10 Of the sons of Joseph, of Ephraim, Elisama the son of Emiud: of Manasses, Gamaliel the son of Phadasur.
kutoka wana wa Yosefu: kutoka Efraimu, ni Elishama mwana wa Amihudi; kutoka Manase, ni Gamalieli mwana wa Pedasuri;
11 Of Benjamin, Abidan the son of Gadeoni.
kutoka Benyamini, ni Abidani mwana wa Gideoni;
12 Of Dan, Achiezer the son of Amisadai.
kutoka Dani, ni Ahiezeri mwana wa Amishadai;
13 Of Aser, Phagaiel the son of Echran.
kutoka Asheri, ni Pagieli mwana wa Okrani;
14 Of Gad, Elisaph the son of Raguel.
kutoka Gadi, ni Eliasafu mwana wa Deueli;
15 Of Nephthali, Achire the son of Aenan.
kutoka Naftali, ni Ahira mwana wa Enani.”
16 These were famous men of the congregation, heads of the tribes according to their families: these are heads of thousands in Israel.
Hawa walikuwa wanaume walioteuliwa kutoka jumuiya, viongozi wa makabila ya baba zao. Walikuwa wakuu wa koo za Israeli.
17 And Moses and Aaron took these men who were called by name.
Mose na Aroni wakawachukua wanaume hao waliokuwa wamepewa majina yao,
18 And they assembled all the congregation on the first day of the month in the second year; and they registered them after their lineage, after their families, after the number of their names, from twenty years old and upwards, every male according to their number:
wakaita jumuiya yote pamoja katika siku ya kwanza ya mwezi wa pili. Watu wakaonyesha nasaba zao kwa koo zao na jamaa zao, nao wanaume waliokuwa na miaka ishirini au zaidi waliorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja,
19 as the Lord commanded Moses, so they were numbered in the wilderness of Sina.
kama Bwana alivyomwagiza Mose. Hivyo aliwahesabu katika Jangwa la Sinai:
20 And the sons of Ruben the firstborn of Israel according to their kindred, according to their divisions, according to the houses of their families, according to the number of their names, according to their heads, were—all males from twenty years old and upward, every one that went out with the host—
Kutoka wazao wa Reubeni, mzaliwa wa kwanza wa kiume wa Israeli: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
21 the numbering of them of the tribe of Ruben, was forty-six thousand and four hundred.
Idadi kutoka kabila la Reubeni ilikuwa watu 46,500.
22 For the children of Symeon according to their kindred, according to their divisions, according to the houses of their families, according to the number of their names, according to their polls, all males from twenty years old and upward, every one that goes out with the host,
Kutoka wazao wa Simeoni: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi walihesabiwa na kuorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
23 the numbering of them of the tribe of Symeon, was fifty-nine thousand and three hundred.
Idadi kutoka kabila la Simeoni walikuwa watu 59,300.
24 For the sons of Juda according to their kindred, according to their divisions, according to the houses of their families, according to the number of their names, according to their polls, all males from twenty years old and upward, every one that goes forth with the host,
Kutoka wazao wa Gadi: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
25 the numbering of them of the tribe of Juda, was seventy-four thousand and six hundred.
Idadi kutoka kabila la Gadi walikuwa watu 45,650.
26 For the sons of Issachar according to their kindred, according to their divisions, according to the houses of their families, according to the number of their names, according to their polls, all males from twenty years old and upward, every one that goes forth with the host,
Kutoka wazao wa Yuda: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
27 the numbering of them of the tribe of Issachar, was fifty-four thousand and four hundred.
Idadi kutoka kabila la Yuda walikuwa watu 74,600.
28 For the sons of Zabulon according to their kindred, according to their divisions, according to the houses of their families, according to the number of their names, according to their polls, all males from twenty years old and upward, every one that goes out with the host,
Kutoka wazao wa Isakari: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
29 the numbering of them of the tribe of Zabulon, was fifty-seven thousand and four hundred.
Idadi kutoka kabila la Isakari walikuwa watu 54,400.
30 For the sons of Joseph, the sons of Ephraim, according to their kindred, according to their divisions, according to the houses of their families, according to the number of their names, according to their polls, all males from twenty years old and upward, every one that goes out with the host,
Kutoka wazao wa Zabuloni: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
31 the numbering of them of the tribe of Ephraim, was forty thousand and five hundred.
Idadi kutoka kabila la Zabuloni walikuwa watu 57,400.
32 For the sons of Manasse according to their kindred, according to their divisions, according to the houses of their families, according to the number of their names, according to their polls, all males from twenty years old and upward, every one that goes out with the host,
Kutoka wana wa Yosefu: Kutoka wazao wa Efraimu: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
33 the numbering of them of the tribe of Manasse, was thirty-two thousand and two hundred.
Idadi kutoka kabila la Efraimu walikuwa watu 40,500.
34 For the sons of Benjamin according to their kindred, according to their divisions, according to the houses of their families, according to the number of their names, according to their polls, every male from twenty years old and upward, every one that goes forth with the host,
Kutoka wazao wa Manase: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
35 the numbering of them of the tribe of Benjamin, was thirty-five thousand and four hundred.
Idadi kutoka kabila la Manase walikuwa watu 32,200.
36 For the sons of Gad according to their kindred, according to their divisions, according to the houses of their families, according to the number of their names, according to their polls, all males from twenty years old and upward, every one that goes forth with the host,
Kutoka wazao wa Benyamini: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
37 the numbering of them of the tribe of Gad, was forty and five thousand and six hundred and fifty.
Idadi kutoka kabila la Benyamini walikuwa watu 35,400.
38 For the sons of Dan according to their kindred, according to their divisions, according to the houses of their families, according to the number of their names, according to their polls, all males from twenty years old and upward, every one that goes forth with the host,
Kutoka wazao wa Dani: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
39 the numbering of them of the tribe of Dan, was sixty and two thousand and seven hundred.
Idadi kutoka kabila la Dani walikuwa watu 62,700.
40 For the sons of Aser according to their kindred, according to their divisions, according to the houses of their families, according to the number of their names, according to their polls, every male from twenty years old and upward, every one that goes forth with the host,
Kutoka wazao wa Asheri: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
41 the numbering of them of the tribe of Aser, was forty and one thousand and five hundred.
Idadi kutoka kabila la Asheri walikuwa watu 41,500.
42 For the sons of Nephthali according to their kindred, according to their divisions, according to the houses of their families, according to the number of their names, according to their polls, every male from twenty years old and upward, every one who goes forth with the host,
Kutoka wazao wa Naftali: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
43 the numbering of them of the tribe of Nephthali, was fifty-three thousand and four hundred.
Idadi kutoka kabila la Naftali walikuwa watu 53,400.
44 This is the numbering which Moses and Aaron and the rulers of Israel, being twelve men, conducted: there was a man for each tribe, they were according to the tribe of the houses of their family.
Hawa walikuwa wanaume waliohesabiwa na Mose, Aroni na viongozi kumi na wawili wa Israeli, kila mmoja akiwakilisha jamaa yake.
45 And the whole numbering of the children of Israel with their host from twenty years old and upward, every one that goes out to set himself in battle array in Israel, came to
Wanaume wote Waisraeli waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi la Israeli walihesabiwa kufuatana na jamaa zao.
46 six hundred thousand and three thousand and five hundred and fifty.
Jumla ya hesabu yao ilikuwa watu 603,550.
47 But the Levites of the tribe of their family were not counted amongst the children of Israel.
Hata hivyo, jamaa ya kabila la Lawi hawakuhesabiwa pamoja na wengine.
48 And the Lord spoke to Moses, saying,
Bwana alikuwa amemwambia Mose:
49 See, you shall not muster the tribe of Levi, and you shall not take their numbers, in the midst of the children of Israel.
“Kamwe usihesabu kabila la Lawi wala kuwaweka pamoja katika hesabu ya Waisraeli wengine.
50 And do you set the Levites over the tabernacle of witness, and over all its furniture, and over all things that are in it; and they shall do service in it, and they shall encamp round about the tabernacle.
Badala yake, waweke Walawi kuwa viongozi wa Maskani ya Ushuhuda, juu ya samani zake na kila kitu kilichomo ndani yake. Wao watabeba Maskani na samani zake zote; wataitunza na kupiga kambi kuizunguka.
51 And in removing the tabernacle, the Levites shall take it down, and in pitching the tabernacle they shall set it up: and let the stranger that advances [to touch it] die.
Wakati wowote Maskani inapohamishwa, Walawi wataifungua, na wakati wowote maskani inapotakiwa kusimamishwa, Walawi watafanya kazi hiyo. Mtu yeyote mwingine ambaye atasogea karibu nayo atauawa.
52 And the children of Israel shall encamp, every man in his own order, and every man according to his company, with their host.
Waisraeli watapiga mahema yao kwa makundi makundi, kila mwanaume katika kambi yake mwenyewe chini ya bendera yake.
53 But let the Levites encamp round about the tabernacle of witness fronting it, and [so] there shall be no sin amongst the children of Israel; and the Levites themselves shall keep the guard of the tabernacle of witness.
Hata hivyo, Walawi watapiga mahema yao kuzunguka Maskani ya Ushuhuda ili ghadhabu isiipate jumuiya ya Waisraeli. Walawi watawajibika kwa utunzaji wa Maskani ya Ushuhuda.”
54 And the children of Israel did according to all that the Lord commanded Moses and Aaron, so did they.
Waisraeli walifanya yote haya sawasawa kama Bwana alivyomwamuru Mose.

< Numbers 1 >