< Proverbs 22 >

1 A good name is more desirable than great riches, and loving favor is better than silver and gold.
Jina jema huchaguliwa dhidi ya utajiri mwingi na fadhila ni bora kuliko fedha na dhahabu.
2 The rich and the poor have this in common: The LORD is the maker of them all.
Watu matajiri na masikini wanafanana katika hili - Yehova ni muumba wao wote.
3 A prudent man sees danger and hides himself; but the simple pass on, and suffer for it.
Mtu mwenye hekima huiona taabu na kujificha mwenyewe, bali mjinga huendelea mbele na huumia kwa ajili yake.
4 The result of humility and the fear of the LORD is wealth, honor, and life.
Thawabu ya unyenyekevu na kumcha Yehova ni utajiri, heshima na uzima.
5 Thorns and snares are in the path of the wicked; whoever guards his soul stays far from them.
Miiba na mitego hulala katika njia ya wakaidi; yeye anayelinda maisha yake atakuwa mbali navyo.
6 Train up a child in the way he should go, and when he is old he will not depart from it.
Mfundishe mtoto njia inayompasa na wakati akiwa mzee hatayaacha mafundisho hayo.
7 The rich rule over the poor. The borrower is servant to the lender.
Watu matajiri huwatawala watu masikini na mwenye kukopa ni mtumwa wa yule anayekopesha.
8 He who sows wickedness reaps trouble, and the rod of his fury will be destroyed.
Yule anayepanda udhalimu atavuna taabu na fimbo ya hasira yake itanyauka.
9 He who has a generous eye will be blessed, for he shares his food with the poor.
Mwenye jicho la ukarimu atabarikiwa, maana anashiriki mkate wake pamoja na masikini.
10 Drive out the mocker, and strife will go out; yes, quarrels and insults will stop.
Mfukuze mbali mwenye dhihaka, na ugomvi utaondoka, mashindano na matukano yatakoma.
11 He who loves purity of heart and speaks gracefully is the king’s friend.
Anayependa moyo safi na mwenye maneno ya neema, atakuwa rafiki yake mfalme.
12 The LORD’s eyes watch over knowledge, but he frustrates the words of the unfaithful.
Macho ya Yehova huyaangalia maarifa, bali huyapindua maneno ya wadanganyifu.
13 The sluggard says, “There is a lion outside! I will be killed in the streets!”
Mtu mvivu husema, “Kuna simba mtaani! Nitauwawa sehemu za njia.”
14 The mouth of an adulteress is a deep pit. He who is under the LORD’s wrath will fall into it.
Kinywa cha malaya ni shimo lenye kina kirefu; hasira ya Yehova huchochewa dhidi ya yule anayetumbukia ndani yake.
15 Folly is bound up in the heart of a child; the rod of discipline drives it far from him.
Upumbavu umefungwa katika moyo wa mtoto, lakini marudi ya fimbo huutoa.
16 Whoever oppresses the poor for his own increase and whoever gives to the rich, both come to poverty.
Anayewanyanyasa watu masikini ili kuongeza mali yake, au kuwapa matajiri, atakuwa masikini.
17 Turn your ear, and listen to the words of the wise. Apply your heart to my teaching.
Tega sikio lako na usikilize maneno ya wenye busara na utumia moyo wako katika maarifa yangu,
18 For it is a pleasant thing if you keep them within you, if all of them are ready on your lips.
maana itakuwa furaha kwako kama utayaweka ndani yako, kama yote yatakuwa katika midomo yako.
19 I teach you today, even you, so that your trust may be in the LORD.
Basi tumaini lako liwe kwa Yehova, ninayafundisha kwako leo- hata kwako.
20 Have not I written to you thirty excellent things of counsel and knowledge,
Sijakuandikia wewe misemo thelathini ya mafundisho na maarifa,
21 To teach you truth, reliable words, to give sound answers to the ones who sent you?
kwa kukufundisha kweli katika maneno haya yenye uaminifu, ili uwe na majibu yenye kutegemewa kwa waliokutuma?
22 Do not exploit the poor because he is poor; and do not crush the needy in court;
Usimwibie masikini kwa sababu ni masikini, au kumponda kwenye lango,
23 for the LORD will plead their case, and plunder the life of those who plunder them.
maana Yehova ataitetea kesi yao, na atawaibia uzima wale waliowaibia masikini.
24 Do not befriend a hot-tempered man. Do not associate with one who harbors anger,
Usifanye urafiki na mtu mwenye kutawaliwa na hasira na wala usiambatane pamoja na mwenye hasira kali,
25 lest you learn his ways and ensnare your soul.
au utajifunza njia zake na utakuwa chambo kwa nafsi yako.
26 Do not you be one of those who strike hands, of those who are collateral for debts.
Usiwe miongoni mwao wapigao mikono, mwenye kuahidi madeni.
27 If you do not have means to pay, why should he take away your bed from under you?
Kama umekosa njia za kulipa, nini kitaweza kuzuia mtu kuchukua kitanda chako chini yako?
28 Do not move the ancient boundary stone which your fathers have set up.
Usiondoe jiwe la mpaka la wahenga ambalo baba zako wameweka.
29 Do you see a man skilled in his work? He will serve kings. He will not serve obscure men.
Je umemwona mtu aliyeuwawa kwenye kazi yake? Atasimama mbele ya wafalme; hatasimama mbele ya watu wa kawaida.

< Proverbs 22 >