< Proverbs 21 >

1 The king’s heart is in the LORD’s hand like the watercourses. He turns it wherever he desires.
Moyo wa mfalme ni mfereji wa maji katika mkono wa Yehova; anaugeuza popote anakopenda.
2 Every way of a man is right in his own eyes, but the LORD weighs the hearts.
Kila njia ya mtu ni sawa katika macho yake mwenyewe, lakini ni Yehova anayeipima mioyo.
3 To do righteousness and justice is more acceptable to the LORD than sacrifice.
Kutenda haki na adili hukubaliwa zaidi na Yehova kuliko sadaka.
4 A high look and a proud heart, the lamp of the wicked, is sin.
Macho ya kiburi na moyo wa majivuno- taa ya waovu- ni dhambi.
5 The plans of the diligent surely lead to profit; and everyone who is hasty surely rushes to poverty.
Mipango ya mwenye juhudi huelekea kwenye mafanikio tu, bali kila mtu anayetenda kwa haraka huelekea umasikini.
6 Getting treasures by a lying tongue is a fleeting vapor for those who seek death.
Kujipatia utajiri kwa ulimi wa uongo ni mvuke unaopita upesi na mtego ambao unafisha.
7 The violence of the wicked will drive them away, because they refuse to do what is right.
Vurugu ya waovu itawaburuta mbali, maana wanakataa kutenda haki.
8 The way of the guilty is devious, but the conduct of the innocent is upright.
Njia ya mwenye hatia ni ukatiri, bali mwenye usafi hutenda yaliyo ya haki.
9 It is better to dwell in the corner of the housetop than to share a house with a contentious woman.
Bora kuishi kwenye kona ya juu darini kuliko katika nyumba pamoja na mke mgonvi.
10 The soul of the wicked desires evil; his neighbor finds no mercy in his eyes.
Hamu ya mwovu ni uchu wa mabaya; jirani yake haoni ukarimu katika macho yake.
11 When the mocker is punished, the simple gains wisdom. When the wise is instructed, he receives knowledge.
Mwenye dhihaka anapoadhibiwa mjinga hupata busara, na mtu mwenye busara anapofundishwa, anaongeza maarifa.
12 The Righteous One considers the house of the wicked, and brings the wicked to ruin.
Atendaye haki huilinda nyumba ya mwovu; huwashusha waovu kwenye uharibifu.
13 Whoever stops his ears at the cry of the poor, he will also cry out, but shall not be heard.
Anayeziba masikio yake kwenye kilio cha masikini, pia atalia, lakini hatajibiwa.
14 A gift in secret pacifies anger, and a bribe in the cloak, strong wrath.
Zawadi ya siri hutuliza hasira na zawadi ya kificho hutuliza ghadhabu kuu.
15 It is joy to the righteous to do justice; but it is a destruction to the workers of iniquity.
Haki ikitendeka, huleta furaha kwa mwenye kutenda wema, lakini huleta hofu kubwa kwa watenda mabaya.
16 The man who wanders out of the way of understanding shall rest in the assembly of the departed spirits.
Yule anayezurura kutoka kwenye njia ya ufahamu, atapumzika kwenye kusanyiko la wafu.
17 He who loves pleasure will be a poor man. He who loves wine and oil will not be rich.
Anayependa raha atakuwa masikini; anayependa divai na mafuta hawezi kuwa tajiri.
18 The wicked is a ransom for the righteous, the treacherous for the upright.
Mtu mbaya ni fidia kwa yule atendaye haki, na mdanganyifu ni fidia kwa waaminifu.
19 It is better to dwell in a desert land, than with a contentious and fretful woman.
Bora kuishi jangwani kuliko kuishi pamoja na mwanamke ambaye huchochea sana ugomvi na malalamiko.
20 There is precious treasure and oil in the dwelling of the wise, but a foolish man swallows it up.
Hazina yenye thamani na mafuta vipo nyumbani kwa mwenye busara, bali mtu mpumbavu huviharibu.
21 He who follows after righteousness and kindness finds life, righteousness, and honor.
Mtu atendaye haki na mwema -huyu mtu hupata uzima, haki na heshima.
22 A wise man scales the city of the mighty, and brings down the strength of its confidence.
Mtu mwenye busara huupima mji wa mashujaa, na huiangusha ngome wanayoitumaini.
23 Whoever guards his mouth and his tongue keeps his soul from troubles.
Anayelinda kinywa chake na ulimi wake hujilinda mwenyewe na taabu.
24 The proud and arrogant man—“Scoffer” is his name— he works in the arrogance of pride.
Mtu mwenye kiburi na maringo- “Dhihaka” ndilo jina lake - hutenda kwa majivuno na kujidai.
25 The desire of the sluggard kills him, for his hands refuse to labor.
Shauku ya mtu mvivu itamuua, maana mikono yake hukataa kufanya kazi.
26 There are those who covet greedily all day long; but the righteous give and do not withhold.
Kwa siku nzima hupatwa na uchu na uchu zaidi, lakini atendaye haki hutoa na wala hazuii.
27 The sacrifice of the wicked is an abomination— how much more, when he brings it with a wicked mind!
Sadaka ya mwovu ni chukizo; huwa ni chukizo zaidi anapoileta kwa nia mbaya.
28 A false witness will perish. A man who listens speaks to eternity.
Shahidi wa uongo ataangamia, bali anayesikiliza ataongea kwa muda wote.
29 A wicked man hardens his face; but as for the upright, he establishes his ways.
Mtu mwovu huufanya uso wake kuwa mgumu, bali mtu mwadilifu ni thabiti juu ya njia zake.
30 There is no wisdom nor understanding nor counsel against the LORD.
Hakuna hekima, hakuna ufahamu, na hakuna shauri linaloweza kusimama kinyume na Yehova.
31 The horse is prepared for the day of battle; but victory is with the LORD.
Farasi hutayarishwa kwa siku ya mapigano, lakini ushindi hupatikana kwa Yehova.

< Proverbs 21 >