< 1 Khokhuen 17 >

1 David te amah im ah a om van nen tah David loh tonghma Nathan taengah, “Kai he lamphai im ah ka om dae BOEIPA kah paipi thingkawng tah himbaiyan hmuiah sut om ke,” a ti nah.
Baada ya Daudi kuingia rasmi katika jumba lake la kifalme, akamwambia nabii Nathani, “Hebu tazama, mimi ninakaa kwenye nyumba nzuri iliyojengwa kwa mierezi, wakati Sanduku la Agano la Bwana liko ndani ya hema.”
2 Te vaengah Nathan loh David te, “Pathen he nang taengah om coeng tih na thinko khuikah bangla a cungkuem he saii ngawn,” a ti nah.
Nathani akamjibu Daudi, “Lolote ulilo nalo moyoni mwako litende, kwa maana Mungu yu pamoja nawe.”
3 Te khoyin ah tah Pathen kah ol te Nathan taengla pawk tih,
Usiku ule neno la Mungu likamjia Nathani, kusema:
4 “Cet lamtah ka sal David te thui pah. BOEIPA loh he ni a thui. Kai hamla om nah im na sak moenih.
“Nenda ukamwambie mtumishi wangu Daudi, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Wewe hutanijengea mimi nyumba ili nikae humo.
5 Israel ka khuen khohnin lamloh tahae khohnin hil he im khuiah ka om hlan. Tedae dap khat lamloh dap khat neh dungtlungim ah ni ka om.
Mimi sijakaa ndani ya nyumba tangu siku ile niliyowatoa Israeli kutoka Misri mpaka leo. Nimehama kutoka hema moja hadi jingine na kutoka mahali pamoja hadi pengine.
6 Israel boeih te a cungkuem dongah ka caeh puei. Israel kah laitloek pakhat taengah ol ka thui coeng te ta? Te te ka pilnam luem puei ham ka uen tih, “Balae tih kai hamla lamphai im na sak uh pawh?” ka ti nah.
Je, popote nilipokwenda pamoja na Waisraeli wote, wakati wowote nilimwambia kiongozi yeyote niliyemwagiza kuwachunga watu wangu, kwa nini hujanijengea nyumba ya mierezi?’
7 Te dongah ka sal David taengah he he thui pah laeh. Caempuei BOEIPA loh he ni a thui. Kai loh nang te tolkhoeng lamloh, boiva hnuk lamloh ka pilnam Israel soah rhaengsang la om ham kan loh coeng.
“Sasa basi, mwambie mtumishi wangu Daudi, ‘Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: Nilikuchukua machungani na kutoka kuandama kondoo ili uwatawale watu wangu Israeli.
8 Na caeh nah takuem ah nang te kan om puei. Na thunkha boeih te na mikhmuh lamloh ka khoe. Na ming te diklai kah hlanglen ming la ka khueh ni.
Nimekuwa pamoja nawe popote ulipokwenda, nami nimekuondolea mbali adui zako wote mbele yako. Basi nitalifanya jina lako kuwa kuu kama majina ya watu walio wakuu sana duniani.
9 Ka pilnam Israel ham hmuen ka khueh vetih anih te ka phung ni. Te vaengah a hmuiah kho a sak vetih tlai voel mahpawh. Lamhma kah bangla anih hmawn sak ham khaw dumlai ca rhoek loh koei uh voel mahpawh.
Nami nitawapatia watu wangu Israeli mahali na nitawapa ili wawe na mahali pao wenyewe pa kuishi na wasisumbuliwe tena. Watu waovu hawatawaonea tena, kama walivyofanya mwanzoni,
10 Ka pilnam Israel soah lai aka tloek la kang uen khohnin lamloh, “Na thunkha boeih te ka kunyun sak bitni. Te phoeiah namah taengkah ka thui bangla BOEIPA loh nang hamla im han sak bitni.
na ambavyo wamefanya siku zote tangu nilipowachagua viongozi kwa ajili ya watu wangu Israeli. Pia nitawatiisha adui zenu wote. “‘Pamoja na hayo ninakuambia kwamba Bwana atakujengea nyumba:
11 Na khohnin loh cum tih na pa rhoek taengla na cet cakhaw na tiingan te namah hnukah ka thoh ni. Na ca rhoek taeng lamloh aka om te khaw a ram ka cikngae sak ni.
Wakati wako utakapokuwa umekwisha, nawe ukawa umekwenda kukaa na baba zako, nitamwinua mzao wako aingie mahali pako kuwa mfalme, mmoja wa wana wako mwenyewe, nami nitaufanya imara ufalme wake.
12 Anih loh kai hamla im a sak vetih a ngolkhoel te kumhal duela ka cikngae sak ni.
Yeye ndiye atakayejenga nyumba kwa ajili yangu, nami nitakifanya imara kiti cha ufalme wake milele.
13 Kai he anih taengah pa la ka om vetih anih khaw kamah taengah capa la om ni. Na hmai ah aka om taeng lamloh ka lat bangla ka sitlohnah he anih taeng lamloh ka lat mahpawh.
Mimi nitakuwa baba yake, naye atakuwa mwanangu. Kamwe sitaondoa upendo wangu kwake, kama nilivyouondoa kwa yeye aliyekutangulia.
14 Anih te kamah im neh ka ram ah kumhal duela ka pai sak ni. A ngolkhoel khaw kumhal duela a cikngae la om ni,” a ti nah.
Nitamweka juu ya nyumba yangu na ufalme wangu milele; kiti chake cha enzi nitakifanya imara milele.’”
15 He ol cungkuem neh hekah mangthui cungkuem bangla Nathan loh David taengah a thui pah tangloeng.
Nathani akamwarifu Daudi maneno yote ya maono haya.
16 Te phoeiah manghai David te cet tih BOEIPA mikhmuh ah ngol. Te vaengah Pathen BOEIPA aw kai he unim?, He la kai nan khuen ham akhaw ka imkhui he mebang nim?
Ndipo Mfalme Daudi akaingia ndani, akaketi mbele za Bwana, akasema: “Mimi ni nani, Ee Bwana Mungu, na jamaa yangu ni nini, hata umenileta mpaka hapa nilipo?
17 He tah Pathen namah mikhmuh ah rhaidaeng. Tedae a hlahoei lamkah khaw na sal imkhui ham na thui. Tangtlaeng Pathen BOEIPA loh boeimang hlang la kai nan hmuh.
Kana kwamba hili halitoshi machoni pako, Ee Mungu, umenena pia kuhusu siku zijazo za nyumba ya mtumishi wako. Umeniangalia kama mtu aliyetukuka kuliko watu wote, Ee Bwana Mungu.
18 Na sal thangpomnah ham te namah taengah David loh metlam koep a thap eh? Namah loh na sal he na ming coeng.
“Daudi aweza kukuambia nini zaidi kuhusu kumheshimu mtumishi wako? Kwa maana wewe unamjua mtumishi wako,
19 BOEIPA aw na sal ham kong ah lennah cungkuem te ming sak ham na lungbuei kah bangla lennah cungkuem he na saii.
Ee Bwana Mungu. Kwa ajili ya mtumishi wako, tena sawasawa na mapenzi yako, umefanya jambo hili kubwa sana na kujulisha ahadi hizi zote zilizo kubwa sana.
20 BOEIPA namah bang he om pawt tih Pathen a tloe a om moenih. Tedae namah tah a cungkuem dongah kaimih hna neh kan yaak uh coeng.
“Hakuna aliye kama wewe, Ee Bwana Mungu, wala hakuna Mungu ila wewe, kama vile tulivyosikia kwa masikio yetu wenyewe.
21 Diklai ah namtu pakhat khaw na pilnam Israel bangla om nim? Namah ham lennah ming la khueh ham, a pilnam te lat pah ham Pathen loh a paan coeng. Egypt lamkah na lat na pilnam mikhmuh lamloh na haek ham tah namtom loh a rhih.
Naye ni nani aliye kama watu wako Israeli: taifa pekee duniani ambalo Mungu wake alitoka kwenda kulikomboa kwa ajili yake mwenyewe na kujifanyia jina kwa ajili yake mwenyewe, kwa kufanya maajabu makubwa na ya kutisha kwa kuwafukuza mataifa mbele ya watu wako, ambao uliwakomboa kutoka Misri?
22 Na pilnam Israel te namah ham kumhal kah pilnam la na khueh. BOEIPA namah tah amih kah Pathen la na om pai.
Uliwafanya watu wako Israeli kuwa watu wako wewe mwenyewe milele, nawe, Ee Bwana Mungu, umekuwa Mungu wao.
23 BOEIPA aw, na sal ham neh a imkhui ham na thui ol te kumhal duela cak pawn saeh. Na thui bangla saii pai laeh.
“Sasa basi, Bwana ahadi uliyoweka kuhusu mtumishi wako na nyumba yake na uithibitishe milele. Fanya kama ulivyoahidi,
24 Te dongah na ming te kumhal duela cak vetih pantai ni. “Israel Pathen tah Israel Pathen, caempuei BOEIPA,” a ti pai. Na sal David imkhui khaw na mikhmuh ah cikngae pai saeh.
ili ithibitike na jina lako litakuwa kuu milele. Kisha watu watasema, ‘Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, Mungu aliye juu ya Israeli, ndiye Mungu wa Israeli.’ Nayo nyumba ya mtumishi wako Daudi itafanywa imara mbele zako.
25 Kai kah Pathen namah loh a im sak hamla na sal kah hna he na vueh pah. Te dongah ni na sal loh na mikhmuh ah thangthui ham a hmuh.
“Wewe, Mungu wangu, umemfunulia mtumishi wako Daudi kwamba utamjengea yeye nyumba. Hivyo mtumishi wako amekuwa na ujasiri wa kukuomba maombi haya.
26 Pathen amah khaw BOEIPA namah coeng dongah ni hnothen he na sal ham na thui pah.
Ee Bwana, wewe ndiwe Mungu! Umemwahidi mtumishi wako mambo haya mazuri.
27 Na sal imkhui he yoethen sak ham neh na mikhmuh ah kumhal duela om sak ham na mulmet coeng. BOEIPA namah loh yoethen na paek dongah kumhal duela a yoethen.
Basi imekupendeza kuibariki nyumba ya mtumishi wako, ili idumu milele machoni pako; kwa ajili yako, Ee Bwana, umeibariki, nayo itabarikiwa milele.”

< 1 Khokhuen 17 >